10 Mar 2008

Weka kando (japo kwa muda) habari zinazovuma za ufisadi,kuna habari njema za warembo wetu wanaotufanya tuamini kuwa nasi tulipendelewa pia na Muumba kwa kutupatia mabinti warembo.Hao wote pichani wanavutia na kumeremeta,ingekuwa ni kuchagua nani bora zaidi ya mwenzie basi majaji wangelazimika kufumba macho na kuchagua kwa kugusa,yaani atakayeguswa kwanza ndio mshindi wa kwanza.Ila binafsi haiba,pozi na mvuto wa huyo model wa tatu kutoka kulia-mstari wa mabinti-vinanishawishi nimpe nambari wani (numero uno)...Yaani utadhani anakuita!!!Au wewe msomaji unaonaje?Big up to Dollywood na wadau wengine wa mambo ya urembo kwa kuvumbua vipaji
Picha kwa hisani ya foto-bloga tishio HAKI

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.