13 Oct 2008


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimefanikiwa kulidhibiti jimbo la uchaguzi la Tarime katika uchaguzi mdogo uliofanyika jana kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo,Chacha Wangwe.Kwa mujibu wa taarifa za uhakika kutoka huko nyumbani,Chadema imepata kura34,545 wakati CCM imepata kura 28,996.Licha ya ushindi huo wa jimbo,pia Chadema imefanikiwa kushinda uchaguzi wa kiti cha udiwani.

Wakati huohuo,Serikali imelifungia gazeti la Mwanahalisi kwa miezi mitatu kwa tuhuma za uchochezi.Uamuzi huo wa Serikali umetangazwa na Waziri wa Habari,Utamaduni na Utangazaji,Kapteni George Mkuchika.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.