22 Jan 2009

Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia wakifanya patrol hapo Mlimani (UDSM).Picha kwa hisani ya MICHUZI JR.

Nilimaliza ngwe yangu hapo Mlimani (UDSM) takriban miaka kumi iliyopita.Kuna yaliyobadilika kwa kipindi cha miaka mitatu niliyokuwa hapo,na kuna mengine yamebaki kama yalivyo.Kwa kifupi sana,katika miaka hiyo mitatu,sikumbuki kama kuna academic year iliyopita pasipo mbinde ya aina moja au nyingine kati ya wanafunzi na serikali.Na kila mara chanzo kilikuwa kilekile:FEDHA.

Binafsi nadhani chanzo cha matatizo ya migogoro kati ya wanavyuo na serikali ni mapungufu katika sera nzima ya uchangiaji gaharama za elimu ya juu.Kwa nchi masikini kama yetu,haihitaji busara kufahamu kwamba kuna wanafunzi lukuki wanaotoka katika familia ambazo kumudu gharama za maisha ya kila siku ni mgogoro,achilia uwezo wa kumudu gharama za kumsomesha mtoto chuo kikuu.Kwa mantiki hiyo,ajenda ya kulipa ada na gharama nyingine kwa silimia 100 ni suala lisilowezekana kwa wanafunzi wanaotoka familia za aina hii,ambao kwa hakika ni wengi zaidi.

Kinachohitajika ni usimamizi mzuri wa mikopo kwa wanafunzi wa aina hiyo.Hii ni investment nzuri kwa future ya taifa letu.Iwapo serikali itakuwa na nia ya dhati kuhakikisha kuwa wakopeshwaji wanarejesha fedha hizo,ni dhahiri itajitahidi kuwatengenezea mazingira mazuri ya ajira pindi watapohitimu masomo yao...kwa vile ajira hiyo ndio inayotarajiwa kuwawezesha kulipa mikopo hiyo ya serikali.

Kama tunaweza kuwakopesha wabunge mashangingi yenye thamani ya mamilioni ya shilingi,naamini kabisa kuwa kuwakopesha wanavyuo wetu ni swala linalowezekana pasipo kusababisha hizi mbinde za kila mwaka au muhula wa masomo.Tatizo sio sera ya uchangiaji gharama per se bali,kama ilivyo kwenye maeneo mengine mengi,ni utekelezaji wa sera hiyo.FFU wanaweza kutuliza ghasia chuoni hapo kwa muda lakini hawawezi kuwa ufumbuzi wa tatizo hilo.

1 comment:

  1. Hili tatizo nahisi kama linapuuzwa kiaina kwa jinsi linavyojirudia:-(

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.