25 Apr 2009



MZALENDO MMOJA AMENITUMIA UJUMBE UFUATO KWENYE E-MAIL,NAMI NAOMBA KUUWASILISHA KAMA ULIVYO:


Kuna habari kwamba mmoja wa wafanyabiashara aliyetajwa na Mkurugenzi wa IPP Bwana Reginald Mengi amenunua hisa nyingi za umiliki wa kituo cha kurusha matangazo ya Television.

Mfanya biashara huyo inasemekana ni yule aliyetumia mtindo huohuo kununua hisa za kampuni iliyokuwa inatoa gazeti lilikuwa maarufu kabla ya mwaka 2005 na sasa si maarufu tena.

Mfanyabiashara huyo ambaye ana hisa kwenye kampuni moja ya simu za mikononi inasemekana ana mpango wa kutumia minara ya kampuni hiyo ya simu ili kusambaza matangazo ya kituo hicho nchi nzima kwa urahisi na bila gharama kubwa.

Kwa vile kampuni yake ndiyo yenye mtandao mkubwa hapa nchini basi itakuwa ni rahisi kwake kusikika nchi nzima kuzidi vyombo vyote vya habari.

Iwapo mpango huo utatekelezwa basi mfanyabiashara huyo atakuwa anaongoza kusikika eneo kubwa nchini.

Bwana Mengi ina ITV na Redio zake tabidi avute bidii ya kasi kwa sababu yeye hataweza kuwa na mtandao mkubwa kama hiyo TV.

Wenu mtafuta habari

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.