29 May 2009

ILIKUWA SIKU,WIKI,MIEZI NA SASA UMETIMIA MWAKA TANGU BWANA ALIPOKUCHUKUA MPENDWA WETU MAMA ADELINA MAPANGO (Mama CHAHALI).PENGO ULILOTUACHIA HALITOZIBIKA MILELE.KINACHOTULIWAZA NI MAPENZI YA BWANA.JAPO SIE TULIKUPENDA,LAKINI YEYE ALIKUPENDA ZAIDI,NA NDIO MAANA AKAKUCHUKUA SAA4.30 USIKU WA TAREHE 29/05/2008.JAPO HAUKO NASI KIMWILI,LAKINI TUKO SOTE KIROHO.

KWA NIABA YA FAMILIA YA MZEE PHILEMON CHAHALI,NACHUKUA FURSA HII KUTOA SHUKRANI ZA DHATI KWA WOTE WALIOSHIRIKIANA NASI KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE KATIKA SALA/DUA WAKATI TUNAMUUGUZA MAREHEMU ADELINA,NA SAPOTI MLIYOTUPATIA KUTUFARIJI BAADA YA MSIBA.BWANA AWABARIKI SANA.

BWANA ALITOA,BWANA ALITWAA.JINA LAKE LIHIMIDIWE MILELE,AMEN.

PUMZIKO LA MILELE UMPE EE BWANA,NA MWANGA WA MILELE UMWANGAZIE.APUMZIKE KWA AMANI.AMEEN

4 comments:

  1. Apumzike pema!
    Poleni kwa kuondokewa na mpendwa wenu.

    ReplyDelete
  2. Mungu amlaze mahala pema Peponi AMEN

    ReplyDelete
  3. Kwa hakika ni vema kumkumbuka Mama ambaye mara zote umekuwa ukieleza mchango wake maishani mwako. Ni vema pia kuendelea kutekeleza yale aliyowekeza katika jamii kwa kuwaonesha ninyi ambao mnashirikiana nasi kwa maneno na matendo.
    Mama alitenda alilotakiwa kutenda na ndio maana wakati wake ulipofika akaondoka, na nashukuru kuwa unathamini kuondoka kwake kama alivyopenda yeye aliyemleta, nasi tukielekea huko aloki tuwe mfano bora na kuwa waelekezi kama alivyokuwa yeye ili wakati wetu ukifika, tuwe tumemaliza kazi yetu hapa tukapumzike naye kwa amani.
    Upendo na amani vitawale ndani mwenu katika kukumbuka maisha ya Mama Adelina

    ReplyDelete
  4. Jamani asanteni sana.Mungu awabariki kwa ujumbe wenu wa kuliwaza.

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.