4 Jul 2009












Michael Jackson mithili ya chura!?The Jacko mithili ya Bikira Maria!?Ukishangaa yanayohusu maisha na kifo cha the King of Pop basi hujakutana na "kazi za sanaa" zinazomhusu the Jacko.Picha za juu ni baadhi tu ya "kazi" hizo.Unajua,fani yenyewe ya sanaa imetawaliwa na ujanja ujanja wa namna flani.Kwa mfano nenda maeneo ya Msasani kwa wauza vinyago wa Kimakonde.Utakutana na kinyago cha Nyerere,kwa mfano,lakini zaidi ya ukweli kuwa kinyago hicho ni cha mpingo (kama alivyodai mchonga kinyago),the rest havifanani kabisa na Nyerere,unless uwe hujawahi kuona sura ya Baba wa Taifa.Pita pita mitaani,utakutana na wasanii wanaodai wanaweza kukuchora na wakikamilisha mchoro utadhani unajiangalia kwenye kioo.Of course,wapo wenye vipaji vya namna hiyo.Lakini kuna " wasanii" pia.Atakuchora,kisha akikupatia "picha yako" unaweza kuishia kutamani kumkaba loba (kabali) ya mbao!

Na kifo cha Michael kinaelekea kuwa dili la nguvu kwa WASANII kwa maana ya ARTISTS na WASANII kwa maana ya CONFIDENCE ARTISTS (con artists).Ama kweli kufa kufaana!

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.