19 Nov 2010


Pichani kwa hisani HAKI NGOWI

Suala ambalo limetawala maongezi ya Watanzania wengi kwenye social media kwa leo ni kitendo cha wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kususia hotuba ya Rais Jakaya Kikwete wakati anazindua Bunge jipya mjini Dodoma.Kwanza niweke wazi msimamo wangu kuwa naunga mkono uamuzi huo wa Chadema.Sifanyi hivyo kwa minajiki ya kukipenda chama hicho bali ni katika kuzingatia ukweli kuwa Chadema wametumia HAKI yao ya Kikatiba na kidemokrasia kuonyesha upinzani wak kwa vitendo.Nimeandika HAKI kwa herufi kubwa kwa vile neno hilo ni muhimu katika "kuwahukumu" Chadema.

Baadhi ya wenzetu wamekishutumu vikali kitendo hicho huku wengine wakikiita "utovu wa nidhamu wa hali ya juu".Lakini wakati wenzetu hao wanatumia HAKI zao za Kikatiba na kidemokrasia kuwalaumu Chadema,hawataki kutafakari japo kidogo kuhusu HAKI kama hizo kwa chama hicho,yaani HAKI yao ku-protest kwa amani dhidi ya mwenendo mzima wa uchaguzi uliopelekea Jakaya Kikwete kuwa Rais tena.

Inawezekana tukio hilo linaonekana sio la kawaida kwa vile ni mara ya kwanza kutokea nchini.Lakini kwa wanaojishughulisha kufahamu kinachoendelea sehemu nyingine duniani watafahaku kuwa hali hiyo imeshatokea kwenye mabunge mbalimbali,kwa mfano nchini Afrika Kusini,Gambia,Sudan, India,Pakistan na Iraki,to mention only a few.

Kwa namna moja au nyingine,vipengere dhalimu vya Katiba yetu vimewaacha Chadema na alternatives chache zaidi ya hatua kama hiyo ya leo kwa vile Katiba yetu inanyima uhuru wa kupinga matokeo ya ushindi wa Rais mahakamani hata kama ushindi huo umepatikana kwa njia zisizo halali.Leo mapungufu hayo makubwa kwenye Katiba yetu yanaweza kuonekana kama jambo dogo.Lakini yayumkinika kuamini kuwa inaweza tokea tukapata Rais dikteta ambaye ameshindwa kwa mabavu lakini tukajikuta hatuna njia ya kupinga "ushindi" wake kwa vile Katiba inamlinda.

Tatizo la Katiba nyingi katika "Nchi za Dunia ya Tatu" na hususan barani Afrika ni ile tabia hatari ya katiba hizo kutumika kwa mahitaji na maslahi ya watawala walio madarakani.Na kwa vile wengi wa watawala hao ni walafi na waroho wa madaraka,na kwa vile madaraka makubwa waliyonayo yanawapa uhuru wa kufanya lolote wapendalo,katiba hizo huwekwa viraka hapa na pale sio kwa minajili ya ustawi wa taifa husika bali kikundi kidogo cha watawala.

Laiti Katiba ingekuwa inaruhusu ushindi wa Rais kupingwa mahakamani basi ni dhahiri Chadema wangeshafungua kesi.Kuna wanaosema "sasa wakitoka nje ya Bunge ndio inasaidia nini?"Majibu ni mengi ila hapa nitatoa machache tu.Kwanza,ikumbukwe kuwa Chadema ndio chama kikuu cha upinzani bungeni.Pamoja na uchache wa idadi ya wabunge wao ukilinganisha na wale wa CCM,hadhi ya chama kikuu cha upinzani ni kubwa na muhimu ndani na nje ya nchi.Pamoja na mazingira na sheria kandamizi dhidi ya vyama vya upinzani,kwa nchi masikini kama Tanzania kuna kila sababu ya sote kuonekana tumeshikamana hata kama mshikamano huo ni wa kinafiki na unawanufaisha zaidi mafisadi.Ndio maana basi nchi wafadhili zilikuwa zikiwakalia kooni watawala wetu kuhusu upatikanaji wa suluhisho la kudumu huko Zanzibar,ambapo hatimaye CCM kwa shingo upande (na licha ya ngebe za akina Makamba) leo hii tunashuhudia serikali ya umoja wa kitaifa huko Zanzibar.

Of course,hali ya kutoelewana huko Zanzibar ilikuwa serious sana hasa kutokana na vurugu za uchaguzi zilizopelekea mauaji ya watu kadhaa,ukweli unabaki kuwa msimamo thabiti wa chama kikuu cha upinzani visiwani humo,yaani CUF,kutotambua matokeo ya chaguzi mbalimbali,sambamba na kelele walizopiga kwa jumuiya ya kimataifa ndivyo vilivyopeleka leo hii kuwepo serikali ya umoja wa kitaifa.

Kwahiyo wanaohoji umuhimu wa wabunge wa Chadema kususia hotuba ya Kikwete wanapaswa kuelewa kuea msimamo imara sambamba na matendo yanayothibitisha msimamo huo yanasaidia kuleta mabadiliko yanayokusudiwa.Leo pale Dodoma kulikuwa na wawakilishi wa nchi na jumuiya mbalinbali za kimataifa.Vyovyote itavyokuwa,wameguswa na tukio hilo ambalo kwa hakika limetia dola utawala wa Kikwete.Baadhi ya nchi hizo ni wafadhili ambao bila wao basi mambo yanakuwa si mambo.

Lakini jingine la muhimu ni kufikisha ujumbe kwa Kikwete na serikali yake (including vyombo vya dola na Tume ya Uchaguzi) kuwa zama za "ndiyo mzee" zimefika kikomo.Hata kama Katiba inaendelea kuhalalisha sheria dhalimu (kama hiyo inayonyima fursa ya kupinga ushindi wa rais mahakamani) mwanya mdogo wa uhuru wa kidemokrasia kupingana pasipo kupigana unawezesha Chadema kuzalisha harakati mpya za mapambano dhidi ya udhalimu lakini pasipo vurugu au umwagaji damu.Kwa tunaotaka kuona Tanzania yenye kuheshimu na kuzingatia haki na stahili za Watanzania,kitendo cha leo cha Chadema kinafungua ukurasa mpya wa matumaini.Kadhalika,kitendo hicho ni hatua kubwa na muhimu ya kukua kwa demokrasia yetu kutoka vyama vinavyokubali yaishe hata pale penye uthibitisho kuwa vimejumiwa kwenye chaguzi,kwenda kwenye zama ambapo uchakachuaji wa chaguzi unaharamishwa hadharani tena kwenye live tv.Message delivered!

Ni wazi kuwa tukio la leo limemgusa Kikwete na serikali yake kama ambavyo limewagusa Watanzania wengi na jumuiya ya kimataifa.Yayumkinika kuwa inawezekana nguvu kubwa iliyotumika kuchakachua matokeo ya uchaguzi uliopita sasa itaelekezwa katika kuihujumu Chadema ili idhoofike na hatimaye kuachana na msimamo wake wa kukataa kumtambua Kikwete.Zitafanyika jitihada za kuwqgombanisha viongozi wa chama hicho kama ilivyokuww kww NCCR-Mageuzi ya Mrema.Kuna uwezekano pia wa Dokta Wilbroad Slaa kuzushiwa zengwe zaidi ya lile ya maisha yake binafsi.Lakini hayo yanaweza kupita pasipo madhara makubwa kwani hata Baba wa Taifa na wenzake walipokuwa wanahangaikia ukombozi wa Tanzania kutoka himaya ya mkoloni walikumbana na vizingiti hivyo.Haya ni mapambano kati ya wenye uchungu na nchi yao dhidi ya wale wanaotaka kuigeuza nchi yetu kuwa "shamba la bibi" na makao makuu ya ufisadi.

Sie Wakristo tunaamini kuwa mwenye haki ataanguka saba mara sabini ( hapa simaanishi kuanguka kama kule kwa Kikwete pale Jangwani) lakini mwishowe atasimama.Kukubali uchakachuaji wa kura kutapelekea matokeo ya ain moja tu: uchakachuaji zaidi.Historia inatufundisha bayana kuwa kukubali kitu kibaya hakusaidii hata chembe kitu hicho kibaya kugeuka kizuri au athari zake kupungua.Wanaoshauri Dkt Slaa na Chadema "wakubali matokeo" hawana tofauti na wanaoweza kusema tuache mapambano dhidi ya malaria au ukimwi kwa vile magonjwa hayo yamekuwepo miaka nenda miaka rudi.

Laiti Nyerere na mashujaa wengine wa mapambano dhidi ya mkoloni wangepatwa na mawazo hayo ya "kukubali yaishe" leo hii tungeendelea kuwa chini ya mkoloni ( I know kuna watakaosema bora mkoloni kuliko fisadi.Mie nasema ukoloni na ufisadi ni mbaya kama ilivyo kwa kansa na ukimwi.Hakuna cha nafuu,wote ni maadui wanaostahili kuangamizwa).Na laiti Nyerere "angekubali yaishe pale Nduli Idi Amini alipotuvamia,basi huends leo tungekuwa sehemu ya Uganda chini ya dikteta Idi Amini au mrithi wake.

Giving up is not an alternative.Mapambano ya kudai haki (kwa amani) lazima yaendelee.Waingereza wana msemo kwamba kukubali kitu pungufu kwa minajili ya bora liende hatimaye hupelekea kupata kilicho pungufu zaidi ya kilichostahili kupatikana.Kadhalika,hatua zote za mabadiliko huanza kwa hatua chache na pengine ndogo lakini zenye impact na hatimaye kutengenrza mazingita mazuri kwa hatua kubwa zenye impact kubwa zaidi na pengine zenye kuweza kuandika historia mpya.Vilevile,actions speak louder than words.Na hiyo imethibitka leo kwani japo Chadema walishatangaza kuwa hawatomtambua Kikwete uzito wa tamko hilo haukuwagusa wengi kulinganisha na tukio la leo la kususia hotuba ya Kikwete.

And by the way,hotuba hiyo ilikuwa na tofauti gani na hotuba lukuki alizotoa wakati wa utawala wake 2005-2010?Hivyo vipaumbele sijui 13 (or were they 19) tulishavisikia kwenye kampeni za 2005 na zikarudufiwa kwenye kampeni za mwaka huu.Kama kuna yeyote aliyechukulia vimpaumbele hivyo seriously all I can say asubiri muda si mtefu atabaini "imekula kwake" as they say in the streets.




Video kwa hisani ya Mwanakijiji

2 comments:

  1. I think its peaceful way of showing disagreement on something, CUF walikuwaga wanagoma kuingia kabisa ka nakumbuka vyema.

    ReplyDelete
  2. Hii hotuba ya Dr Slaa imeonyesha ukomavu na uzalendo wa kweli nikilinganisha alichoongea JK jana...Kimsingi JK hakuonyesha katika hotuba yake iwapo NEC ni tatizo na pia Katiba viraka iliyopo ni tatizo pia...Yeye JK aliendelea na kauli za kejeli, maringo na majivuno kama kawaida yake anaposhindwa kuelewa mambo muhimu katika kulinda amani iliyopo kama siku zilizopita alipowadharau wafanyakazi kwa kauli za kijiweni na kihuni kabisa kukataa kuongoze mishahara.

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.