12 Feb 2011

Zoezi la ujenzi wa jarida kamili mtandaoni linaendelea vema.Lakini kama ilivyo pindi mtu anapohama kutoka sehemu moja kwenda nyingine,kuna vitu vinavyochukua muda kuwa timilifu.

Naomba nichukue fursa hii kuwashukuru wanahabari-mtandaoni wenzangu waliokubali ombi langu kwao kunitundikia katika blogu zao tangazo la mabadiliko ya anwani ya mtandao huu.Nawashukuru sana.Na pia nawakaribisha sana kushirikiana nami katika tovuti hii shirikishi.

Kwa wale niliowatumia ombi kama hilo lakini wakapuuza,sina maneno nao as such.Kuna baadhi yao ambao nina uhakika wa asilimia kubwa kuwa hawakuona barua pepe niliyowatumia.Nina uhakika huo kwa vile nawafahamu kuwa si watu wenye tabia ya dharau,jeuri au husda.Labda wako bize sana kiasi hawakuwa na muda hata wa kusoma barua-pepe iliyokuwa na ombi hilo.

Lakini kuna wengine ambao nadhani walikuwa na sababu zao "binafsi".Labda hawakupendezwa na uhamaji huu wa kutoka blogu kuelekea jarida kamili mtandaoni (wanasema ukitaka ufarakane na Waswahili basi piga hatua japo nusu).Au labda wao ni viumbe muhimu kabisa ambao hawakupaswa kubughudhiwa na ombi kama hilo.Na kwa baadhi ya waswahili,wanaamini dharau na maringo ni viungo (recipes) vya "umuhimu" wao katika jamii.

Enewei,natambua wametumia haki yao ya kikatiba na kidemokrasia lakini hio haiondoi ukweli kuwa walichofanya si uungwana.Na kwa vile binafsi naamini kwenye kuelezana ukweli,nimeona ni vema kuwashutumu japo naelewa fika haitobadili chochote.

Mwisho,nakaribisha maoni kuhusu tovuti hii hususan yaliyomo na mwonekano.Pia naomba wanahabari-mtandaoni ambao awali nilijumuisha anwani za blogu zao kwenye blogroll yangu lakini kwa sasa hazipo,wasifikiri nimewatelekeza.Naendelea na zoezi la kukusanya viungo vyote vya awali ambavyo kwa bahati mbaya vilifutika wakati wa uhamaji huu unaoendelea.

Tupo pamoja

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.