26 Mar 2011




Picha zote mbili zinahusu MAANDAMANO.Picha ya kwanza juu inahusu maandamano yanayotarajiwa kufanyika leo jijini London,na kushirikisha vyama mbalimbali vya wafanyakazi,lengo likiwa kuibana serikali ya hapa Uingereza kuhusu hatua zake za kubana matumizi (spending cuts).

Picha ya pili inaonyesha kikundi kidogo cha waandamanaji eneo la Kinondoni Mtambani wakiandamana kulaani mashambulizi ya Wamarekani,Waingereza,Wafaransa,na washirika wao dhidi ya majeshi ya serikali ya kidikteta ya Kanali Muamar Gaddafi.

Charity begins at home.Hivi wenzetu hawa walioandamana kumtetea Gaddafi hawaelewi kuwa hata huko Libya kuna maandamano ya kumng'oa dikteta huyo?Lakini, la muhimu zaidi,kama ni mdadi wa maandamano,kwanini basi waungwana hawa wasingeandamana kudai maisha bora....

Aliyesema "akili ni nywele kila mtu ana zake" wala hakukosea

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.