19 May 2011



Alfajiri ya leo nilikutana na comment ya msomaji mmoja aliyejitambulisha kama Andrew Blasio.Msomaji huyo alianza kwa kuhoji kama sijawahi kuona zuri lililofanywa na CCM.Mie nikamjibu kwa kifupi, "You tell me,sir" kwa maana kama yeye anayajua mema ya CCM basi anieleze badala ya kutegemea mie niyataje.

Akanijibu kuwa yeye haamini kuwa hakuna jema la CCM.HAAMINI.So what?Kwa vile yeye haamini kuwa hakuna jema la chama hicho basi imekuwa nongwa kwa mie kuandika yasiyo mema ya CCM.Akaendelea kunishutumu kuwa eti niko biased katika uandishi wangu,na pengine ni propaganda.Akadai mwandishi sharti awe fair na balanced,na kuhitimisha kuwa hajaona mwandishi anayehubiri uvumilivu wa kisiasa.KWA VILE YEYE HAJAONA BASI INAMAANISHA HAKUNA KITU KAMA HICHO!!!

Nikamjibu

 Sasa mbona wewe unayejua mema ya CCM hutaki kuyaweka hadharani?Na hiyo political tolerance kwako unaitafsiri vipi?Mafisadi wasikemewe?

Nikaongeza 

Unakosoa kuwa niko biased kwa vile hujaona nikiandika "mema" ya CCM.Je bado utaniona biased nikikwambia sijaona jema la kuandika?Na kwanini wewe mwenyewe usijione uko biased kwa kutarajia mema hata kama hayapo?Kukosoa ni rahisi kuliko kutenda jambo.Why not start writing objective,unbiased articles preaching all the good stuff CCM wanafanya?

Naye akanijibu 

Usinishambulie bosi! I'm trying to read " black and white"! kama huoni jema lolote lililofanywa na serikali ya CCM then that is your problem maana "Mwenye macho haambiwi tazama!". Being fair and balanced comes from "journalistic ethics & standard". it doesn't matter whether you are reporting news or you are penning opinions!

Nikahitimisha mjadala kwa kumwambia, 

To be honest with you,I dont write to please whoever reads my articles.I speak my mind supported with facts.As for "journalistics ethics&standards",I'm not a journalist by profession.Tell you what my friend,if you dont like what I write,or it's contrary to what you believe,best I could advise you is to avoid reading them.I dont take issues with constructive criticism,but I hardly pay attention to "people who are not happy with what I wrote just because it's contary to their points of view

Kimsingi,Bwana Blasio hapendezwi na msimamo wa makala zangu kuikosoa CCM,na angependa kuona ikipongezwa.Lakini kama ulivyoona kwenye malumbano yetu hapo juu,yeye mwenyewe hajaongea japo suala moja ambalo lingeweza kuifanya CCM ipongezwe.It doesnt make any sense kumshutumu mtu anayekemea jambo flani lakini wakati huohuo mtoa shutuma anashindwa kutoa japo mfano mmoja wa kuonyesha kuwa kukemea huko sio kwa haki.

Kwa Bwana Blasio na watu wengine wenye mtizamo kama wake,napenda kuwafahamisha kuwa siandiki makala kwa minajili ya kujikomba au kumpendeza mtu.Ninachoandika ni mawazo yangu binafsi,ambayo kama kawaida yangu hayatoki tu pasipo utafiti wa kutosha na wa kusapoti nisemacho.

Lakini la msingi zaidi ni hili.Kama kuna mtu anaona ninachoandika hakimpendezi,kwanini basi apoteze muda wake kukisoma?Si kwamba sipendi kukosolewa bali ninachoafiki ni constructive criticism na sio baseless and unfounded criticism.

Ni rahisi kulaumu makala ninazoandika lakini si rahisi kuandika makala mbadala.Na pengine njia mwafaka ya kupambana na hoja "potofu" kama zangu (kwa mujibu wa Bwana Blasio) ni kuandika makala inayoweza sio tu kujibu au kupinga hoja zangu bali pia kukata mzizi wa fitina kwa kuorodhesha mema ya CCM ambayo hayapatikani kwenye maandiko yangu.

NAREJEA TENA.SIANDIKI KUMFURAHISHA MTU BALI NINA-EXPRESS MAWAZO YANGU NILIYOYAFANYIA KAZI KWA UMAKINI KABLA YA KUYAWEKA HADHARANI.ASIYERIDHISHWA NAYO ANAWEZA KUYAPUUZA KWA KUKAA KIMYA AU KUTOYASOMA.MAWAZO MBADALA RUKSA LAKINI SHUTUMA ZISIZO NA KICHWA WALA MIGUU HAZINA FURSA.


0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.