12 Jul 2011


Ndugu zangu wapendwa,kwa niaba ya familia ya Chahali naomba kuwasilisha shukrani za dhati kwa wote ambao kwa namna moja au nyingine mmeungana nasi kwa maombi kwa baba Mzee Philemon Chahali ambaye hali yake bado ni mahututi kufuatia ajali ya kugongwa na pikipiki huko Ifakara,Alhamisi iliyopita.

Ningetamani sana kutoa shukrani kwa kutaja jina la kila mmoja wenu lakini naomba nitoe shukrani za jumla.Nawashukuru sana bloggers wenzangu ambao licha ya kunisaidia kuweka tangazo la maombi ya sala kwa baba mmekuwa mkinitumia meseji na barua pepe za kunipa moyo pamoja na sala/dua zenu.Katika kuonyesha upendo wa hali ya juu,dada yangu blogger wa hapa UK Rachel Siwa aliweka maombi kwenye misa ya Jumapili iliyopita huko Coventry.Tunakushukuru sana dada Rachel na Mungu akubariki.Bloga mwenzangu Miss Jestina naye amekuwa akitujulia hali ya Mzee mara kadhaa kwa siku,bila kuwasahau wadogo zangu Jackie Lawrence (La Princessa) na Faith Charles Hillary (Candy1World) ,na Mtakatifu Simon Kitururu,bloga Malkiory  Matiya na Nova Kambota

Huko Twitter nimekuwa nikipata sapoti ya kutosha tangu zilipojiri habari za ajali.Dada zangu Maria Sarungi na Lilly  Melody,pamoja na wasanii wetu mahiri kabisa Hamisi Mwinjuma (Mwana FA) na Joseph Haule (Profesa Jay) ni miongoni mwa wana-Twitter wenzangu ambao wamekuwa mstari wa mbele kunifariji.

Kwa bahati mbaya,ukweli mchungu kuhusu maisha ni kwamba mpaka upate tatizo ndio unaweza kufahamu upendo wa watu wanaokuzunguka.Kuna watu nilikuwa sifahamiani nao kabisa lakini baada ya kusikia habari za ajali iliyomkumba baba wamekuwa ni nguzo muhimu kutusapoti.Kwa kweli ninawashukuru sana na Mungu awabariki sana kwa upendo wenu.Ni imani ya familia yetu kuwa sala zenu na zetu zitamsaidia Mzee Chahali sio tu kupata nafuu bali kupona kabisa.

Kwa vile inaniwia vigumu kublog kutokana na tatizo linalonikabili,naomba pia kutumia fursa hii kuwashukuru wasomaji wote wa blogu hii na watu wengineo walionipigia kura katika Tuzo la Blogu za Kitanzania (Tanzanian Blog Awards) ambapo japo sikuibuka mshindi lakini nimepata matokeo ya kupigiwa mstari.Kwa kifupi,blogu hii imeshika nafasi ya pili katika categories za Best Inspiration Blog na Best News Blogs na imeshika nafasi ya tatu katika category ya Best Political Blog.Ukiangalia kwenye hizo categories mbili za mwanzo utagundua kuwa aliyeshika nafasi ya kwanza ni bloga ambaye blogu yake imeshatembelewa na wasomaji zaidi ya milioni 12 wakati blogu hii "inasuasua" na wasomaji 424538 hadi dakika hii.Kwangu hayo ni mafanikio makubwa sana lakini si mafanikio yangu pekee bali ya wadau wote wa blogu hii.Namshukuru kila aliyenipigia kura,na japo hatukuibuka washindi wa jumla,kushiriki kwenye tuzo hizo na kukamata nafasi za juu ni tuzo kubwa sana.

Naomba nimalizie kwa kurejea tena shukrani zangu na za familia yangu kwenue nyote mnaoshirikiana nasi kwenye maombi kwa ajili ya Mzee Philemon Chahali.Ni matumaini yetu kuwa Bwana anasikiliza sala/dua zetu na atamjalia baba uponyaji kwa vile Mungu ni mwema na mwenye upendo.

ASANTENI SANA

4 comments:

  1. Aaaaww! U r so welcome, n I'm so happy n thankful that Baba yetu kapona. Glory be to God in the highest. Stay blessed my dear. Tuko pamoja.

    ReplyDelete
  2. pole sana lakini yote ni kazi ya Mungu tutaendelea kumuombea baba na tunaamini Mungu hatasaidia poleni sana

    ReplyDelete
  3. Mungu aendelee kutubariki sote kaka yangu!Tuko pamoja katika maombi ya baba Mzee wetu Chahali.

    ReplyDelete
  4. Tuko Pamoja Mkuu katika maombi!
    Mzee Philemon Chahali tunakuombea upone haraka!

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.