30 Aug 2011



Raymond Kaminyoge
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), imeshusha bei ya mafuta kuanzia leo.Kwa hatua hiyo, bei ya ukomo ya petroli kwa Mkoa wa Dar es Salaam sasa itakuwa Sh2,070, huku dizeli ikiwa Sh1,999 na mafuta ya taa Sh1,980. Bei ya ukomo wa bidhaa hiyo itatofautiana kulingana na umbali wa maeneo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Haruna Masebu alisema hiyo ni kutokana na kushuka kwa bei ya bidhaa hiyo katika soko la dunia.Alisema ikilinganishwa na bei ya zamani, petroli imeshuka kwa Sh44.55 sawa na asilimia 2.11 huku dizeli ikishuka kwa Sh31.99 sawa na asilimia 1.57 na mafuta ya taa yakishuka kwa Sh25.62 sawa na asilimia 1.28.Mnamo Agosti 2, Ewura, ilishusha bei ya mafuta.

ZAIDI SOMA HAPA
Petroli ilishuka kwa Sh202.37 kwa lita ambayo ilikuwa ni sawa na asimilia 9.17, dizeli kwa Sh173.49 sawa na asilimia 8.32 na mafuta ya taa kwa 181.37, sawa na asilimia 8.70 hali iliyosababisha vurugu na uhaba wa bidhaa hiyo.

Lakini, siku 11 baada ya kushusha bei hiyo, Ewura ilipandisha tena bei ya mafuta kutokana na kile ilichodai kuwa ni kupanda bei katika soko la dunia na kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania na kusababisha Bodi ya mamlaka hiyo kubanwa na Baraza la Mawaziri.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.