8 May 2013

















Watakaosema Rasi Jakaya Kikwete ni miongoni mwa vyanzo vya matatizo ya udini yanayotusumbua sasa wanaweza kuwa sahihi. Mtandao ulioasisiwa mwaka 1995 kwa minajili ya kumwingiza Kikwete Ikulu na kufanya kazi kwa nguvu hadi mwaka 2005 ulichangia sana kuleta siasa za mifarakano. Nani aasiyejua jinsi Mtandao wa Kikwete ulivyofanikiwa kumchafua Dkt Salim Ahmed Salim hadi akaonekana kana kwamba ni adui wa Watanzani hususan huko Zanzibar?

Mwaka 2010 wakati Kikwete anawania kurejea Ikulu kwa mara nyingine, tulishuhudia kila aina ya uhuni ambapo vitu muhima kama dini vilitummika kwa minajili ya kisiasa, kubwa likiwa kumzuwia Dkt Willbrod Slaa asiingie Ikulu. CCM iliruhusu kuhususha kazi ya zamani ya Dkt Slaa, yaani upadre, ni uthibitisho tosha kuwa Cahdema ni chama cha Kikatoliki. Kikwete aliyafahamu hayo lakini akakaa kimya, kwani alijua yangemsaidia kumwingiza tena Ikulu.

Lakini tuweke lawama pembeni kidogo. Tatizo kubwa la Kikwete ni uzembe wa kuruhusu kuzungukwa na maharamia hatari kabisa kwa Tanzania yetu.Uzembe hauna excuse. Lakini kuna nyakati unaweza kuona picha halisi ya Kikwete pasi maharamia hao.Hebu msomaji angalia picha hizo hapo juu kwa makini.Yah, kuna wanaosema Kikwete ni msanii mzuri-yaani mtu anayejua kutumia fursa vizuri kufikisha ujumbe anaotaka yeye.

Honestly, katika picha hizo hapo juu ninamwona Mtanzania mwenzetu ambaye ana uchungu na ameguswa na yaliyowakumba hao aliokwenda kuwatembelea. The pictures are so genuine to an extent unaweza kujiuliza is this the same JK tunayemlaumu kila siku?

I know, kuna watakaohisi sifa hizi ninazompa JK ni kwa vile yupo na Wakristo. No.Mie ninaangalia utu wa huyu kiongozi wetu kama unavyojionyesha kwenye picha hizo.Wanasema picha zinaweza kuwakilisha maneno 1000.Mie nasema picha hizo hapo juu zimewakilisha maneno mengi sana...japo pia zinaweza kuzua maswali kwamba kama Kikwete ni mtu wa kujali kiasi hikli kwanini basi anaruhusu hao maharamia wanaomzunguka waipeleke nchi yetu kwenye korongo nene?




0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.