6 Mar 2014

 
Wanasayansi wanadai kuwa wamefanikiwa kuwadunga waathirika 12 wa Ukimwi viini vya kinga ambavyo vina uwezo wa kuzuwia virusi vya ugonjwa huo. Watafiti wanadai kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuelekea kwenye matibabu kamili ya Ukimwi, ugonjwa unaomlazimu mwathirika kutumia vidonge vya kupunguza makali kwa muda wote wa uhai wake.

"Hii inaimarisha imani yetu kwamba viini vya aina ya T (T cells) vilivyorekebishwa ni ufunguo muhimu katika kuondoa haja ya mwathirika wa Ukimwi kuhitaji dawa kwa muda wote wa uhai wake..." alieleza Dkt Carl H. June, Profesa wa Richard W. Vague katika tiba za kinga katika Idara Tiba na Matibabu na Dawa za Maabara , Shule ya Madawa ya Penn's Perelman huko Philadelphia nchini Marekani.

Watafiti walitumia teknolojia inayojulikana kama "zinc finger nuclease" (ZFN)- waliyoielezea kama 'mkasi wa kimolekyuli kurekebisha viini vya T katika mfumo wa kinga mwilini ili kuiga kuongezeka kwa CCR-5-delta-32, viini vinayofahamika kwa kuwafanya baadhi ya watu wasipate Ukimwi.

Soma habari kamili HAPA (na usisite kuwasiliana nami iwapo utahitaji tasfiri)

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.