9 Dec 2014


Nadhani mnakumbuka jinsi kikundi cha WANAHARAKATI kilivyoshikilia bango kuhusu kilichoitwa mradi wa treni za kisasa kati ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere na Mjini Kati Dar, ambapo aliyeitwa 'mwekezaji, ROBERT SHUMAKE, alidai yupo tayari kuuanza hata siku hiyohiyo uliposainiwa mkataba wa awali. Bonyeza  HAPA kusoma zaidi kuhusu suala hilo na ufuatiliaji wetu.

Hata hivyo, nadhani haitoshi tu kumtilia mashaka SHUMAKE Pasi kuchukua hatua dhidi ya wahusika. Ikumbukwe SHUMAKE bado ni Balozi wetu wa heshimu huko Marekani. Je kama anatiliwa mashaka katika suala hili haitoshi kumvua wadhifa huo aliopewa katika mazingira yasiyoeleweka? Kadhalika, je kwanini waliokurupuka kusaini mkataba wa awali na mbabaishaji huyo wasiwajibishwe? 

Tusipokuwa makini, mtu huyo 'mjanja mjanja' anaweza kuzua IPTL nyingine kwa kusaini mkataba kwa huduma isiyopatikana kisha kudai malipo asiyostahili.


0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.