18 Apr 2015


Kwa mujibu wa tovuti ya Bunge letu la Muungano, kama nilivyoi-access saa 11.02 alfajiri kwa saa za hapa Uingereza, marehemu wabunge hawa hapa chini wameendelea kuorodheshwa kwenye tovuti hiyo sio tu kama bado wapo hai bali pia ni wabunge katika majimbo husika.

Ninaamini kabisa kuwa taasisi muhimu kama Bunge ina fungu la kutosha kwa ajili ya huduma zake mbalimbali, ikiwa ni pamoja na tovuti yake. Na hata ingekuwa haina fungu, kufanya marekebisho kwenye tovuti hiyo ni jambo la dakika chache tu, na lisilo na gharama yoyote.

Hakuna ubaya kwa wabunge marehemu kuendelea kuwepo katika tovuti ya Bunge iwapo ukweli kwamba waheshimiwa hao sasa ni marehemu utabainishwa, hususan katika kipengele kinachoonyesha muda wa utumishi wao katika mhimili huo muhimu wa dola.

Pengine hili ni suala dogo lakini kwa hakika Bunge ni moja ya vitambulisho vya taifa letu, na tovuti yake ni njia rahisi kwa Watanzania na wasio-Watanzania kupata habari na taarifa zinazoihusu taasisi hiyo. 

Licha ya kasoro hiyo, nilipofanya search ya majina ya baadhi ya wabunge, hakukuwa na matokeo yoyote.Ukitaka kuhakikisha, tafuta jina la Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete, kwa mfano.








Ni matumaini yangu kuwa Ofisi ya Bunge letu itarekebisha kasoro hii haraka iwezekanavyo

CHANZO: Screenshot za picha kutoka tovuti ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.