8 May 2015

Jana Uingereza ilipiga kura katika Uchaguzi wake Mkuu, na matokeo yalianza kupatikana jana usiku muda sio mrefu baada ya vituo vya kupigia kura kufungwa majira ya saa nne usiku.

Hadi muda huu, chama cha Conservatives kinazidi kufanya vizuri, na hadi muda huu ninapoandika makala yhii, wameshajikusanyia viti 250, chama cha Labour kina viti 212 na Liberal Democrats viti 6. Chama cha kibaguzi cha UKIP kimepata kiti kimoja tu hadi muda huu, na ubashiri unaonyesha kitapata viti viwili tu, huku kiongozi wake Nigel Farage akiwa katika hatihati ya kushindwa.

CChama tawala hapa Uskochi, Scottish National Party (SNP) kimepata mafaniuko makubwa mno, ambapo katika viti 59 kimeshapata viti 55 na kimepoteza kiti kimoja tu.

Kuna kila dalili kuwa Waziri Mkuu David Cameron ataendelea kuwa Waziri Mkuu lakini ni mapema mno kufahamu iwapo ataunda serikali kwa kushirikiana na chama gani. Kuhusu kiongozi wa Labour, Ed Miliband, tayari kuna tetesi kuwa huenda akalazimika kujiuzulu kabla ya mwisho wa siku hii ya leo baada ya chama chake kufanya vibaya. Kuhusu chama cha Liberal Democrast, huenda kiongozi wake, Naibu Waziri Mkuu, Nick Clegg, nae akalazimika kujiuzulu kufuatia matokeo mabaya mno kwa chama hicho. 

Matokeo kamili yatafahamika hapo baadaye. 

Kwa coverage ya usiku mzima kuhusu uchaguzi huo, tembelea ukurasa wangu wa Twitter hapa @chahali

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.