21 Jun 2015

Ni kitu gani?

Summer Solstice, kwa lugha nyepesi, ni siku yenye mchana mrefu zaidi kuliko zote katika mwaka. Neno 'mchana' hapa linamaanisha muda wa mwanga wa jua. Ni siku mbapo baadhi ya sehemu, kama hapa Uingereza, zina masaa mengi zaidi ya mchana (mwanga wa jua) kuliko usiku (muda wa kiza).
Pengine ni muhimu kufahamu kwamba kwa hapa Uingereza, kwa mfano, maana ya mchana na usiku ni tofauti na huko nyumbani, kwa kiasi flani. Kwa mfano, Ukikutana na mtu saa 6 alfajiri, salamu huwa 'Good morning' kwani kwa wenzetu hawa, asubuhi inaanza rasmi saa 6 kamili 'usiku.' (0000 midnight). Vilevile, katika msimu wa baridi ambapo jua huzama mapema na kuchelewa kuchomoza, si ajabu ukiagwa kwa 'Good night' saa 11 jioni, kwa sababu muda huo tayari jua limeshazama.
Neno 'Solstice' linatokana na neno la Kilatini  'solstitium' linalomaanisha meaning ‘jua kusimama’.

Kwanini inatokea?

Kwa wenye kumbukumbu ya somo la Jiografia, Summer Solstice hutokea pale mhimili wa sayari yetu 'unapoegemea' zaidi kuelekea kwenye jua.
Kinyume cha tukio hili,  Winter Solstice, hutokea pale mhimili wa dunia 'unapoelemea' mbali zaidi na jua, na kusababisha muda mfupi zaidi wa jua katika siku, yaani mchana - kwa maana ya mwanga wa jua- unakuwa mfupi mno kuliko usiku.

Inatokea lini?

Summer solstice hutokea kati ya Juni 20 na 22.
Kwa mwaka huu ni leo Jumapili Juni 21.
Kwa hapa Glasgow, jua litachomoza saa 10 na dakika 31 asubuni (takkriban saa moja tangu muda huu ninapoandika makala hii) na kuzama  saa 4 na dakika 6 usiku


0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.