3 Jul 2016

Mwanadada Mtanzania mkaazi wa hapa Uingereza, Karrima Carter (kushoto pichani juu) jana alifanya harambee huko Norwich kwa ajili ya kusaidia makundi mbalimbali yenye mahitaji nchini Tanzania. Karrima, amekuwa akijibidiisha kutoa misaada mbalimbali huko nyumbani ambapo kwa sasa anahudumia vituo kadhaa ya yatima jijini Dar es Salaam, sambamba na kutoa misaada ya vifaa vya elimu kwa shule mbalimbali za msingi.

Tangu aanze jukumu alilojipachika la kupeleka misaada huko Tanzania, ameshatuma makontena manane yenye vifaa anavyokusanya huku Uingereza na ambavyo vina mahitaji kwa makundi mbalimbali huko nyumbani. Cha kuvutia sana ni kuwa anafanya hivyo kwa gharama zake, akiamini katika kutumia kipato liachonacho kuwasaidia wengine wenye mahitaji.

Chini ni baadhi ya picha za kwenye tukio hilo la jana





























1 comment:

  1. ameonyesha mfano mzuri wa kuigwa. Mungu amzidishie tele.

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.