Showing posts with label APRIL FOOLS' DAY. Show all posts
Showing posts with label APRIL FOOLS' DAY. Show all posts

1 Apr 2015


Kuanzia leo April Mosi, Watanzania wanaokuja hapa Uingereza hawatahitaji viza kufuatia uamuzi uliotolewa jana na kutangazwa na 'Wizara ya Mambo ya Ndani' ya hapa (Home Office) Hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa Uingereza kushirikianana nchi kadhaa za jumuiya ya madola, ikiwemo Tanzania, katika maeneo kadhaa ya kiuchumi.

Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA

1 Apr 2013


Well, unless wewe msomaji ni mgeni wa Tanzania yetu, na unless hufahamu kuwa April Mosi ni siku geni, tunaweza tu kutamani kusikia Rais wetu akichukua hatua kali dhidi ya wazembe waliopelekea vifo kadhaa vya Watanzania wenzetu.

Ni hivi, kama ilivyokuwa kwa milipuko ya mabomu Mbagala naGongo la Mboto, na kama ilivyokuwa kwa mtukio ya kusikitisha ya kutekwa na mateso kwa Dkt Ulimboka na Kibanda, na mauaji ya mwandishi Mwangosi, zitaundwa tume, wajumbe wa tume watatafuna fedha za bure, na hatimaye karatasi zitakazotumika kuchapisha ripoti za tume itakayoundwa kufuatia ajali hiyo mbaya kabisa ya kuporomoka jengo zitaishia kufungiwa maandazi kama si chapati au vitumbua.

Hii ndio Tanzania yetu, na leo ni April Fool's Day

Samahani kama kichwa cha habari hii kimekupa matumaini hewa.

1 Apr 2010

Katika hali isiyotarajiwa,Baba Mtakatifu Benediktini wa 16 ametangaza kujiuzulu wadhifa huo kufuatia tuhuma zinazoliandama Kanisa Katoliki kuhusu kashfa za ngono na ulawiti. Uzushi tu wala hajajiuzulu.Leo ni Siku ya Wajinga Duniani.Je wewe ni miongoni mwao (at least kwa leo)?

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.