Showing posts with label BIZARRE STUFF. Show all posts
Showing posts with label BIZARRE STUFF. Show all posts

14 Jul 2010

Nimekumbana na swali hili tangu udogoni:Alianza kuku,au lilianza yai?Kama alianza kuku,alitoka wapi ilhali sote twajua kuku anatoka kwenye yai?Na kama lilianza yai,lilitoka wapi wakati tunafahamu kuwa yai hutagwa na kuku?Baada ya kukosa jibu lenye mantiki niliamua kuachana na swali hali maana kujihangaisha kutafuta jibu ilikuwa kazi bure.Nahisi hata nawe msomaji umeshakumbana na swali hilo mara kadha wa kadha.

Lakini hatimaye kitendawili hicho kimepata ufumbuzi.Kwa mujibu wa gazeti la bure la Metro,watafiti wa Kiingereza wanasema kuwa kuku ndiye aliyeanza kabla ya yai kwa vile yai linaweza kupatikana tu kwa chembechembe za protini zinazopatikana katika mifuko ya uzazi ya kuku.

"Imekuwa ikidhaniwa kwa muda mrefu kuwa yai ndilo lililoanza kabla ya kuku lakini sasa tuna ushahidi wa kisayansi kuwa kwa hakika alianza kuku kabla ya yai",alisema Dakta Colin Freeman kutoka Chuo Kikuu cha Sheffield,aliyeshirikiana na watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Warwick.

"Protini hiyo ilitambuliwa kabla na ilihusishwa na uzalishaji wa yai lakini kwa kuchunguza kwa undani tumegundua namna gani protini hiyo inavyowezesha hatua hiyo (ya kutengeneza yai).

Protini hiyo-inayofahamika kitaalam kama ovocledidin-17 (OC-17) inafanya kazi kama kichocheo (catalyst) kuharakisha maendeleo ya yai.

Wanasayansi hao walitumia kompyuta yenye uwezo wa hali ya juu (supercomputer) ifahamikayo kama HECToR,ambayo ipo jijini Edinburgh,Scotland, kukuza (zoom) hatua zinazoonyesha jinsi yai linavyozalioshwa.

Ilibainika kuwa OC-17 ni muhimu katika kuanzisha kukomaa (crystallization)-hatua ya awali katika uundwaji wa gamba la yai.Protini hiyo hugeuza calcium carbonate kuwa chembechembe za calcium (calcite crystals) ambazo ndizo zinazounda gamba la yai,huku zikitengeneza gramu 6 za gamba katika kila masaa 24.

Profesa John Harding,pia kutoka Chuo Kikuu cha Sheffield,alisema kuwa ugunduzi huo unaweza kuwa na matumizi mengine pia."Kufahamu namna gani kuku wanatengeneza mayai ni jambo la kupendeza lakini pia linaweza pia kutupatia vidokezo katika namna ya kutengeneza vitu vipya".

Imetafsiriwa kutoka gazeti la Metro toleo la leo.

10 Mar 2009

The winner of a pancake-eating contest has dropped dead while accepting his prize for gorging on 43 of the banana and cream stuffed desserts. Boris Isayev, 48, from west Russia died on stage moments after winning the competition to mark the end of Butter Week.

The contest, which took place in the town of Chernyakhovsk, was part of festivities to celebrate Maslenitsa, the last week before the period of Lent starts. According to local traditions, meat, fish, dairy products and eggs are forbidden during Lent, as well as dancing and parties.Witnesses described Mr Isayev as "the most active participant in the contest" adding that he "ate all the types of pancakes on offer and won fairly".

The witness added: "He had really enjoyed the pancakes but then he started foaming at the mouth and went down like a sack of stones.

"People have fainted during the contests before."

Medics tried to revive Mr Isayev after he collapsed while collecting his prize on stage. The exact cause of death is not clear but doctors believe he choked after a piece of pancake got lodged in his throat. Celebrations are said to have continued after Mr Isayev's body was taken away in an ambulance.


SOURCE: Sky News

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.