Showing posts with label DAR IN PICS. Show all posts
Showing posts with label DAR IN PICS. Show all posts

3 May 2008

Hivi karibuni,eneo la Mlimani (UDSM) liligeuka Baghdad kwa muda kufuatia ghasia kubwa kati ya wanafunzi na vyombo vya dola.Hali sasa ni shwari,na majuzi walifanya uchaguzi wa viongozi wapya wa DARUSO japo inasemekana kwamba turnout ilikuwa ndogo sana.Ni kutokana na ushwari huo ndipo nami nilibahatika kuwatembelea wanazuoni flani hapo,na kufanikiwa kunyaka picha hii inayoonyesha eneo la Ubungo kama sijakosea,japo halionekani vema sana.

Miongoni mwa maeneo ya hapa jijini yanayotuwezesha kuendeleza libeneke la bloggin-japo nyakati nyingine kwa kusuasua-ni cafe moja iliyopo Millennium Tower.Kuna jamaa kanidokeza kuwa yeye huwa mwenyeji sana eneo hili kwa ajili ya kuangalia MIGONGO!Well,inawezekana alikuwa anazungumzia mgongo wa Twiga huyu,jirani na mwanga wa taa,ambaye ni kivutio mwanana!

6 Apr 2008

Pata burudani ya picha zaidi kutoka Bongo
Lounge ya hoteli ya Kempinski

Kempinski kwa ndani,kwa hakika wanastahili pongezi kwa namna palivyoboreshwa.
Msikiti wa Kichangani Magomeni.Jirani na msikiti huuu,kuna makutano ya barabara za Morogoro na Kawawa.Eneo hilo ni maarufu sana kwa vibaka wababe wanaopora madereva.Ni zaidi ya kosa la jinai kusimamisha gari eneo hilo huku kioo kikiwa chini au nusu.
Makutano ya barabara za Morogoro na Bibi Titi.
Kasi ya majengo mapya ni kubwa katika maeneo mengi ya Dar.Hata hivyo,wananchi wengi wanalalamika kuwa hali ya maisha inazidi kuwa ngumu.
Sehemu hii inapendeza.Kwa muda nilijiskia kama niko Scotland vile.Hapa ni Kilimanjaro Hotel Kempinski.

Kempinski

Hakuna sheria muhimu ya uendeshaji gari mitaa ya Kariakoo zaidi ya ubabe.Ukifuata taratibu za usalama barabarani utaishia kugongwa,kuporwa au kulala hapohapo.
Mbinde za driving mitaa ya Kariakoo
Leo ni Jumapili na foleni katika barabara nyingi ni pungufu
I wish kila siku barabara zingekuwa nyeupe namna hii.
Msikiti wa Kichangani Magomeni
Millennium Towers.Eneo hili kuna internet cafe ambayo ni kimbilio la wengi wanaotegemea wireless connection.Pia ni mahala unapoweza kugongana na jamaa mbalimbali mliopoteana kutokana na kwenda nje kusaka hili au lile
Hii joint inaitwa "SAMAKI SAMAKI".The name tells it all...it's all about fish,fish and even more fish...Jana tulipewa ofa ya bure ya dagaa wa kukaanga.Yaani.... ndio mambo ya home sweet home hayo!However,dont let these nice pics fool you,mapambano ya maisha hapa yanataka ujasiri...na ukiwa jijini hapa inaweza kuwa rahisi kufahamu kwanini UFISADI unashamiri.The going seems to be getting tougher and tougher,forcing some folks to try to make the tough get going.
Barabara nyeupe
Barabara nyeupe pyee
Mitaa ya Kariakoo







Wakati unasubiri batch nyingine ya picha kutoka hapa,hebu pata burudani kutoka kwa Common featuring Dwelle katika track ya The People

5 Apr 2008

Zoezi la kuleta picha za Bongo linaendelea.I'm not trying to become a photoblogger of some sort,hiyo wanaiweza magwiji WA FANI kama rafiki yangu HAKI.Hapa chini kuna kiji-collection kidogo ca picha nilizodhani zinaweza kukupendeza wewe msomaji. Zote zimepigwa kwa kutumia Samsung Armani,na naamini quality ya picha inaridhisha.If not,let me know,plz!















Foleni za magari bado ni tatizo sugu kama Ufisadi.Hapa ni junction ya maeneo ya Namanga.Halafu jana kulikuwa na mvua si utani.Breaking news niliyopata jana mchana ni kuwa maji yalikuwa yanalazimisha kuingia ndani ya "mansion yetu" huko Ifakara (well,kwa level ya kijiji chetu,nyumba ikipigwa lipu nje,na vikorombwezo flani na geti la kizushi basi inapata hadhi ya kuitwa "mansion")

















Hapa ni HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI.Jana nayo ilikuwa imeelemewa na maji.Tatizo la Hospitali hii ni kwamba mazingira ya nje hayaridhishi,ya ndani ni ya kusikitisha na huduma ndani ni za kuvunja moyo. It's like a hospital from hell.



















Niliamua kuwanasa kwa picha hawa wageni waliokuwa wanafanya nini sijui hapo Mbuyuni,barabara ya Ali Hassan Mwinyi.Lilikuwa sio kundi kubwa as such lakini kama ujuavyo Bongo hakuna jambo dogo,muda si muda kukawa na lundo la watu wanawashangaa hao jamaa...I could swear I saw someone cancelling his trip to work just ku-join the party ya kushangaa... More pics hapo chini




















STAY TUNED FOR MORE PICS.

2 Apr 2008

Dar kuna tatizo kubwa sana la foleni.Na kwa kasi magari yanayoingizwa kila siku jijini hapa,nadhani kimeo cha foleni kitaebndelea kwa muda mrefu sana.Na inavyoonekana,hakuna mipango ya kuboresha barabara ili ziweze kumudu wingi wa magari.Sijui quality ya picha hizi ikoje.Ni majaribio ya Samsung Armani kwenye poor light (mida ya saa 12).Location ni Millennium Towers.Will keep on bringing more pics for you guys.






Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.