Showing posts with label Katy Perry. Show all posts
Showing posts with label Katy Perry. Show all posts

24 Jan 2015

Siku ya mwaka mpya nilitangaza huko Twitter kuhusu dhamira yangu ya #ProBono yaani kuwahamasisha watu wenye uwezo, vipaji au nafasi mbalimbali kuisadia jamii bure. Kimsingi, huku nchi za Magharibi, sekta ya kujitolea pasi malipo imekuwa na msaada sana kwa jamii. Ninaamini kwamba nasi tukijaribu, itakuwa na msaada mkubwa sana hasa tukizingatia jinsi umasikini unavyowakwaza wanajamii wengi.

 So far, mwitikio umekuwa wa kuridhisha. Tayari, mwanasheria mmoja mahiri huko nyumbani anashughulikia bure kesi ya mwanajamii mmoja huku akiridhia kupelekewa kesi nyingine inayohusu mirathi. Pia gwiji mmoja wa fani ya PR na Marketing amekubali kumsaidia mwanajamii mmoja kuingia kwenye fani hiyo. Vilevile, designer mmoja wa kimataifa huko nyumbani amekubali kumsaidia desgner mchanga aliyekuwa anahitaji mwongozo katika fani hiyo.Kadhalika, dada mmoja mtaalam wa mambo ya fedha amekubali kutoa msaada wa ushauri wa kifedha bure, sambamba na wasanii wawili maarufu wa huko nyumbani, mmoja wa Bongoflava na mwingine wa Bongo Movies.


Lengo la makala hii sio kuzungumzia kuhusu #ProBono bali muda mfupi uliopita, nilikutana na habari ambayo kwa namna flani inahusiana na suala hilo la #ProBono. Hivi unawakumbuka TLC? Ni kikundi cha akinadada watatu wa Marekani ambao walivuma sana miaka ya nyuma katika fani ya R&B.

Labda kabla ya kwenda mbali, niamshe kumbukumbu yako kwa mmoja wa nyimbo zao maarufu, Red Light Special (TAHADHARI: Hii ni 'dirty version.')




Kwa bahati mbaya, Aprili 25, 2002 kundi hili la akinadada watatu lilipatwa na mkosi wa kuondokea na mwenzao aliyekuwa maarufu zaidi, Lisa Lopez au maarufu kama 'Left Eye, (pichani chini) aliyefariki kwa ajali ya gari akiwa mapumzikoni nchini  Honduras.


Kifo cha mwenzao huyo kililiathiri sana kundi hilo, kwa sababu zilizo wazi.

Hata hivyo, katika jitihada zake za kurejea tena katika anga za muziki, wasanii wawili waliobaki katika kundi hilo, Rozonda 'Chilli' Thomas na Tionne 'T-Boz' Watkins, waligeukia wazo la ujasiriamali linalotamba sasa katika nchi za Magharibi hasa Marekani, linalofahamika kama 'crowdfunding' (kuomba jamii ikuchangie fedha) kupitia jukwaa la kufanya hivyo linalojulikana kama KICKSTARTER

T-Boz (kushoto) na Chilli

Habari njema ni kwamba siku nne tu baada ya kuanzisha kampeni yao ya Kickstarter kuwapatia dola za kimarekani 150000 kwa ajili ya kutengeneza albamu yao mpya, na ya kwanza baada ya miaka 10 ya ukimya, wamefanikiwa kupata michango zaidi ya kiwango walichokusudia.Hadi kufikia juzi, walikuwa wameshachangiwa Dola za kimarekani 180000, ikiwa ni Dola 30000 zaidi ya kiwango walichokusudia.

Kilichowapa moyo zaidi ni pale walipotembelea ukurasa wao wa Kickstarter


na kubaini kuwa msanii mahiri wa Pop, Katy Perry (pichani chini), ameahidi kuwachangia dola 5000. Kadhalika, kundi maarufu la zamani la New Kids on the Block limeahidi kuwachangia wanadada hao dola 20,000

Baada ya kusoma habari hiyo nikakumbuka wazo langu la #ProBono na kujiuliza, hivi haiwezekani kuwasaidia wanajamii mbalimbali, kwa mfano wasanii wetu, katika namna hiyo kundi la TLC linasaidiwa na jamii kutimiza lengo lao la kutengeneza album mpya?

Jibu ni kwamba inawezekana, japo si rahisi sana kuwashawishi watu wachangie fedha kwa ajili ya mafanikio ya mtu mwingine. Hata hivyo, cha muhimu hapa ni moyo wa kujitolea. Kwahiyo basi, ushauri wangu, hasa kwa kuanzia na wasanii, mfanye moja kati ya haya mawili:

Kwanza, aidha mjaribu bahati zenu huko Kickstarter, kama wanavyofanya TLC japo yaweza kuwa vigumu kwa msanii asiye maarufu

Au pili, tumieni mpango wa #ProBono kama nilivyoueleza ambapo kwa pamoja tutahamasisha upatikanaji wa mahitaji mbalimbali kwa ajili ya utengenezaji na uzinduzi wa kazi ya msanii husika. 

Sharing is always caring!



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.