Showing posts with label MWENGE WA UHURU. Show all posts
Showing posts with label MWENGE WA UHURU. Show all posts

31 May 2010


Nafahamu unaweza usinielewe kwenye post hii lakini naomba niweke bayana kuwa niko radhi kutofautiana nawe msomaji wangu mpendwa.Kwa tutakaoafikiana,all I can say is POA.Nimeguswa na habari kuwa jana Makamu wa Rais,Dkt Shein, amezindua mbio za mwenge.Lengo la makala hii ni kuibua mjadala kuhusu suala hili la MWENGE WA UHURU.

Zamani hizo,mwenge ulikuwa na maana kubwa kwa kila mahali ulipopita.Lakini ni dhahiri kwamba mbio za mwenge kwa sasa hazina tofauti na ngonjera kuwa "Tanzania ni nchi ya Kijamaa" au kaulimbiu kwamba "Maisha Bora kwa Kila Mtanzania Yanawezekana".

Hili dude linalokula mamilioni ya shilingi katika gharama za kununua mafuta ili liendelee kuwaka,sambamba na posho kwa wanaolizungusha nchi nzima lina umuhimu gani kwa sasa?Maana zamani hizo mwenge ulikuwa na madhumuni ya KUMULIKA lakini sote tunafahamu kuwa kwa muda mrefu sasa mwanga wa mwenge huo unamulika vichochoroni tu huku ukishindwa kuwaangazia macho mafisadi wanaotafuna nchi yetu kama mchwa.Natambua kuwa kuna miradi mbalimbali inayozinduliwa wakati wa mbio za mwenge lakini hilo linafanyika hata wakati mwenge umezimika.Kwa maana nyingine,mwenge uwake usiwake bado wananchi wataendelea kujikusanya (pamoja na uchovu wao) kujitafutia maendeleo yao wenyewe.

Tatizo kubwa la sie Waafrika ni kuendeleza "mila na desturi" hata pale zilipopitwa na wakati.Hivi fedha zinazotumika kuzungusha mwenge nchi nzima zinaweza kujenga zahanati,shule na barabara ngapi?Kwa hakika ni nyingi tu.

To cut the story short,mie nina mtizamo kuwa mbio za mwenge zimepitwa na wakati.Naamini kuwa gharama zinazotumika katika mbio za mwenge zinaweza kutumika vizuri zaidi kwenye maeneo mengine ya msingi.Mwenge unakimbizwa kila mwaka lakini umasikini wa Watanzania unazidi kuongezeka (puuza kauli za Mkulo kuwa uchumi unazidi kukua kwani analipwa mshahara kusema 'lolote'),ujambazi ndio usiseme,na mafisadi wanazidi kulindwa na chama tawala.Sasa hili dude linalokula mafuta kama halina akili nzuri bado lina umuhimu kweli kwa mazingira ya Tanzania ya sasa?

Karibu uchangie

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.