Showing posts with label Mahusiano. Show all posts
Showing posts with label Mahusiano. Show all posts

25 Jan 2012



Tim Gunn reveals he hasn't had sex in 29 years, but doesn't feel like 'less of a person' for it 

The 'Revolution' host says he's been celibate since the end of a 'very intense relationship'

Wednesday, January 25 2012, 12:10 PM

 Fashion consulant Tim Gunn arrives for the finale of the Bravo TV reality show "Project Runway" at the Tribeca Grand Hotel.

JAMES KEIVOM/NEW YORK DAILY NEWS

Tim Gunn revealed his celibacy Tuesday, but added, 'I don't know what's around the corner.'

Tim Gunn made it very clear Tuesday that nothing will be off limits on his new daytime talk show, "The Revolution" — including himself.
The "Project Runway" mentor opened up about his nearly 30-year sexual dry spell on the show, but said he had nothing to be ashamed of.
"I haven't had sex in 29 years," he revealed. "Do I feel like less of a person for it? No. Not even remotely."
Gunn, 58, explained that a former lover had so scarred him in all matters intimate that he just hasn't had a sexual relationship since.
"I was in a very intense relationship for a long time and my partner ended it, saying quite frankly that he was impatient with my sexual performance," he said. "It was at the cusp of AIDS, and I think a lot of people simply retreated because they were concerned about their health.
"I'm a perfectly fulfilled person ... but it's very psychological," he said.
Gunn, who is openly gay, added that just because he has gone nearly three decades without sex doesn't mean he isn't open to possibilities down the line, however.
"I have feelings. It's not as though I am some barren forest," he said. "I don't want to imply to anyone that I have a mandate that says no sex. I don't know what's around the corner.
"I'm happy to be healthy and alive, quite frankly."
SOURCE: NYDaily News


21 Sept 2011

Kama kuna hoja inayotawala zaidi kuliko nyingine kwenye blogu na maandiko mengi ya wengi wa mabloga wa kike wa Kitanzania ni hii ya hisia kwamba WANAUME WA KITANZANIA SI WAAMINIFU KWENYE MAHUSIANO.Ninaposema inatawala simaanishi kuwa huo ndio mtizamo wa mabloga hao bali ni kitu kinachojitokeza mara nyingi pengne zaidi ya vitu vingine,hususan kwenye sehemu za kutolea maoni (comments).

Utakuta dada mmoja anaomba ushauri kwa wenzie kuhusu mwenza wake ambaye aidha anamhisi kuwa si mwaminifu au amemsaliti kwenye uhusiano wao.Ukiweka kando ushauri atakaopewa,wengi wa wachangiaji wa kike hukimbilia kuhitimisha kuwa tatizo la msingi ni "ukweli kwamba wanaume wa Kibongo si waaminifu",huku wengine wakienda mbali zaidi na kudai "wanaume wetu wa Kibongo wanatembea wakiwa na zipu zao wazi-kwa maana ya kuwa tayari kukamata chochote kile kitakachokatiza mbele yao".

Katika hatua hii siwezi kusema hisia hizo ni sahihi au la ila nisichokubaliana na hitimisho la jumla (blanket conclusion) kwamba WANAUME WOTE WA KITANZANIA SI WAAMINIFU.Sijui kama wanaohitimisha hivi huwa wanajaribu angalau kutafakari kidogo kuhusu baba zao,maana nao pia ni wanaume wa Kitanzania.Hatari kubwa ya kuhitimisha jambo jumla jumla ni kuwaingiza hata wale wasiohusika.Wengi wetu tunafahamu jinsi baba zetu walivyo waadilifu kwa mama zetu hadi kufanikiwa kutufikisha hapa tulipo.Japo si wote lakini kwa kiasi kikubwa baba zetu-hususan wale waliokula chumvi nyingi-wamejitahidi kadri wawezavyo kuwa waaminifu kwa mama zetu.

Kwa vile mada hii ni ndefu na ili kuijadili kwa ukamilifu inahitaji kitabu kizima basi niifupishe kwa,kwanza,kuangalia sababu za kitaaluma kwanini watu wana-cheat.Naomba ieleweke kuwa hata kwenye kusaka sababu kwenye masuala mengine ni nadra kupata sababu timilifu kabisa kwa sababu kuna vigezo vingine vinavyoathiri kila sababu,kwa mfano mazingira,umri,uchumi,malezi,nk

Hata hivyo,tafiti mbalimbali za mahusiano ya kimapenzi zinataja sababu zifuatazo kuwa 'maarufu' zaidi katika kuelezea kwanini watu wana-cheat

KULIPIZA KISASI:

Sie Wakristo tunafundishwa kwenye Agano Jipya kuwa ukipigwa kofi shavu la kushoto basi geuza na shavu la kulia.Hii inapigia mstari umuhimu wa kutolipiza kisasi.Lakini hata kwenye Maandiko hayo Matakatifu haikuwa hivyo siku zote.Katika Agano la Kale,mafundisho yalikuwa ni JICHO KWA JICHO na JINO KWA JINO.Kwenye stadi za dini inafahamika kama 'sheria ya kulipiza kisasi' (law of retaliation) na 'sheria ya mapatano' (law of reconciliation).Katika poetic justice 'jino kwa jino' inaweza kulinganishwa na kile kiitwacho adhabu ya kioo (mirror punishment),yaani-kwa kifupi-malipizi kwa kutenda kosa.Msingi hapa ni kwamba tendo jema huzawadiwa na tendo baya huadhibiwa.

Kwa hiyo,kwa vile mwenza wa kiume au wa kike ame-cheat basi yule aliyekuwa cheated anaamua kulipiza kisasi kwa ku-cheat pia.Jino kwa jino,au tit-for-tat.Lakini hitimisho la kisomi ni kwamba mara nyingi kulipiza kisasi hakusaidii sio tu kuleta ufumbuzi wa tatizo bali pia hata kuondoa maumivu ya kusalitiwa kwenye penzi.

Unajua kuna tofauti kati ya kufanya jambo pasipo msukumo wowote na kufanya jambo kwa vile kuna msukumo flani.Mwanaume au mwanamke anayeamua tu ku-cheat kwa vile anajiskia kufanya hivyo ana tofauti na yule aliyelazimika ku-cheat kwa sababu tu anataka kumkomoa flani.Tofauti hii ni sawa na ile ya binti anayefanya ukahaba kama hobby na yule anayefanya kwa vile anahitaji fedha au hana njia nyingine ya kipato zaidi ya kuuza mwili/utu wake.Kufanya jambo kwa uhuru ni,well,kuwa huru (hata kama ni makosa) wakati kufanya jambo kutokana na kusukumwa ni sawa na utumwa.

Anyway,hapa tunataja sababu za ku-cheat na sio kuhukumu kuwa anaye-cheat kwa sababu flani yuko sahihi au la.Twende sababu ya pili

KAMA KIPO KITUMIE

Kuna wenzetu wanaoamini kwamba kama nyama iliyopo kwingineko ni ya kupendeza,tamu,isiyo na sumu,na inapatikana,then kwanini isiliwe?Watu wa aina hii wanaamini kuwa wanachofanya ni kula kilicho bora,na ambacho kinapatikanika (available/accessible).Hawana uchungu kwa kufanya hivyo kwa vile wanaamini kuwa maridhio ya nafsi ni muhimu zaidi kuliko uhalali au ukosefu wa uhalali wa tendo husika.

Nadhani ushaskia misemo kama 'cha muhimu ni kupata fedha,jinsi ilivyopatikana sio muhimu'.Au wengine wanakwenda mbali zaidi na kudai kuwa watu wenye kuifaidi zaidi dunia ni wale waisoongozwa na 'hiki ni halali na hiki si halali'.Ishu kama uadilifu,uaminifu,nk sio muhimu kwao.

Katika kundi hili kuna wale tunaoweza kuwaita waathirika wa Columbus Syndrome (tafsiri ya Kiswahili ni ngumu lakini turahishishe kwa kuita 'ugonjwa wa kiu ya uvumbuzi kama Christopher Columbus.Yaani tamaa ya kujua mambo zaidi ya maelezo sahihi yanavyoelezea mambo hayo).Unakuta mwanaume 'anafukuzia sketi' kwa vile tu anataka kuonja sehemu za siri za mwanamke huyo.Haijalishi kama ana mwenza au hana,bali la muhimu kwake ni kwamba A sio B,na nyama ya mbuzi si ya ng'ombe,na japo maharage na kunde zote ni mboga lakini maharage si kunde.Hawa wapo katika kile kinachoitwa kwa kimombo kama taste-testing (kujaribu ladha).

Kwenye kundi hili pia kuna wale wanaotaka kupima kama ujuzi wao wa kufukuzia sketi bado upo,licha ya ukweli tayari wana wenza nyumbani.Kwa akina dada,inawezekana ni kupima kama "kama nilimudu kum-cheat yule bwege mwaka juzi na hakujua mpaka tunaachana kwanini nisijaribu tena safari hii?"Ni sababu zinazoweza kuonekana kama za kupuuzi lakini kumbuka kuwa mara nyingi wanaofanya upuuzi hawana muda wa kutafuta sababu.Na hata ukiwahoji wakupe sababu basi majibu watakayokupa yanaweza kukutibua kuliko upuuzi waliofanya.

Kufupisha maelezo,wanao-cheat kwa mujibu wa sababu hii wanafanya hivyo kwa vile,well,kama kipo kitumie.

WASIOTOSHEKA

Unakumbuka ule wimbo wa zamani wenye maneno "ee jamani mwanadamu hatosheki,hata ukimpa nini milele hataridhika...ukimpa kumi atataka mia..."Well,si kweli kwamba kila mwanadamu hatosheki bali ukweli ni kwamba kama ilivyo kuna wenzetu ni wepesi kutosheka,wenzetu wengine kamwe hawatosheki.Tuchukulie mifano halisi.Katika kusaka ufumbuzi watatizo la rushwa katika Mamlaka ya Mapato Tanzania ikashauriwa mishahara minono na marupurupu mazuri inaweza kusaidia kuondoa vishwawisho vya watumishi wa taasisi hiyo kudai na kupokea rushwa.Seriakli ikaridhia kufanya marekebisho katika muundo wa mishahara ya watumishi wa taasisi hiyo.Sihitaji kukwambia kuwa TRA ni miongoni mwa taasisi zilizobobea kwa rushwa,pengine mara dufu ya ilivyoluwa zama za mishahara kiduchu.

Kwanini watu hawa waendelee kudai na kupokea rushwa ilhali wanalipwa mishahara minono kabisa?Well,jibu rahisi ni tamaa.Lakini jibu jingine linaweza kuwa mazowea.Kuna msemo wa Kiingereza usemao "vyovyote utakavyomtunza,mbwa mwitu hawezi kuwa mbwa".Nenda porini,kamata mbwa mwitu,mpe kila aina ya matunzo kama mbwa wa kawaida,lakini kama hatoishi kukung'ata basi atatoroka na kurejea porini.Wanasema kunguru hafugiki,na samaki yake maji.Ukimtoa samaki majini,basi umemuua.Period.

Kwahiyo kama ambavyo kuna watu hawatosheki na fedha wanazopata (kwa mfano mafisadi serikalini ambao wanalipwa mishahara mikubwa kuliko mahitaji yao) basi pia kuna watu hawatosheki na tendo la ndoa.Hata mkewe/mwenza wake ampe uroda kiasi gani bado atahitaji nyongeza.Na kuna akinadada hata apewe-ashakum si matusi- 'mabao' mangapi bado atahitaji zaidi.

Katika sababu hii kuna marejeo ya sababu iliyopita ya 'kama kipo tumia' kwa maana ya kama una njaa na chakula kipo basi kula,na kama ukienda kwingine na bado unajiskia hamu ya kula endelea kula.Ma-Tiger Woods hawa wa kike na kiume wanahitaji zaidi na zaidi just like wale wala rushwa wa TRA.

Kwa wengine hili ni kama tatizo la kiafya linalohitaji tiba za kisayansi.Kabla ya tiba hiyo,dawa pekee ya kukabiliana na 'hamu isyoisha ya kula au kuliwa uroda' ni 'kula au kuliwa uroda' zaidi na zaidi.Ni mithili ya walevi ambao njia pekee ya kumudu maisha ni pombe.

Kwa bahati mbaya,watu wa kundi hili wanaweza kujikuta matatizoni zaidi ya kuharibu mahusiano na wenza wao.Yaleyale ya simba akikosa nyama anaweza kula majani,basi si ajabu kwa watu wa kundi hili kujikuta wakiamua liwalo na liwe na kudiriki hata kufanya tendo la ndoa na watoto wadogo,watu wa jinsia moja na wao,kubaka aua hata kufanya tendo la ndoa na midoli.Kwao,tendo la ndoa ni sawa na oksijeni,pasipo hiyo ni kama wanaelekea kukata roho.

Namkumbuka kijana mmoja enzi hizo za ujana,mitaa ya Kinondoni.Kila wikiendi alikuwa anakwenda Ambassador Plaza (Gogo Hotel) 'kukamatia',na kwa vile sehemu hiyo ilikuwa inapendelewa na mashoga basi alipokuwa akikosa binti wa kulala naye basi 'anakamatia' shoga.Na huyu kijana alikuwa na girlfriend mrembo kupita maelezo.

Na kuna mama mmoja niliyewahi kufanya nae kazi sehemu fulani ambayo mshahara,posho na fedha kwa ujumla ilikuwa sio tatizo.Lakini licha ya kuwa na mume mwenye uwezo wa kifedha na mwenye haiba ya kutamanisha mwanamke yeyote yule,mama huyo alikuwa yuko radhi kulala hata na wafagizi hapo ofisini,baada ya kuwamaliza mabosi wenzie na wafanyakazi wa kada ya kati.Wambeya walikuwa wanadai kuwa mama huyo 'alipokuwa kwenye siku zake' alilazimika kufanya tendo la ndoa kinyume cha maumbile alimradi akidhi addiction yake.

KITULIZA ROHO

Wakati mwingine mwenza hujikuta anashawishika ku-cheat kutokana na mapungufu yanayozidi kuathiri mahusiano yake na mwenzie.Naomba tuelewane hapa.Sio kama nahalalisha ku-cheat bali natoa moja ya sababu zinazoweza kumfanya mtu a-cheat.Ikumbukwe kuwa wizi ni wizi tu,hakuna wizi halali.Mtu anayekutwa na hai ya kuua,kwa mujibu wa sheria zetu,adhabu yake ni kunyongwa hadi afe.Hakuna tofauti kati ya aliyeua mtu mmoja na aliyeuwa watu 10,wote ni wauaji.

Kadhalika,anaye-cheat kwa vile mumewe/mkewe hamridhishi,hana tofauti na yule wa kundi la kwanza au la pili au la tatu hapo juu.Wote wame-cheat,na kama kuna adhabu dhidi ya ku-cheat,wote wataadhibiwa kama cheaters,period!

Inaelezwa kuwa baadhi ya wanawake wanapoolewa wanaweza kujikuta wanajisahau kuhusu vitu vilivyofanya waume zao watamani kuwaoa in the first place.Matokeo yake ndoa inakuwa dull,tendo landoa linakuwa kama kutimiza wajibu tu kama sio kutokuwepo kabisa.Nasisitiza kuwa ku-cheat sio ufumbuzi lakini kwa mhusika hiyo ni excuse tosha ya kwenda nje ya uhusiano.

Wanaume pia,iwe kwenye ndoa au mahusiano tu kati ya boyfriend na girlfriend,wanadaiwa kuwa wakati mwingine wakishapata wanachohitaji wanawachulia wenza wao for granted.Zawadi za 'enzi za kutongozana'-maua,perfume,kadi,sim/sms mfululizo,nkzinaanza kufifia kadri umri wa uhusiano unavyozidi kuongezeka.

Again,naomba kusisitiza kuwa hii sio kwenye kila uhusiano bali hutokea,wewe na mimi tumeshaskia simulizi za aina hii mara kadhaa.

Mwenza anajikuta yupo kwenye uhusiano ambao ni 'uhusiano jina',hakuna mahaba,hakuna msisimko,na pengine kibaya zaidi,hakuna tendo la ndoa,au hata kama likiwepo ni la 'kizushi' tu.Kuna wanaoanza kwa kutishia ku-cheat-si kwa maneno bali vitendo.Kwa mfano,binti ambaye baada ya kuwa na mwenza wake alianza kubadilisha uvaaji wake 'wa utatanishi' (kwa lengo la kuepusha wasumbufu mtaani) anaamua kurejea kwenye uvaaji huo ili kumpelekea ujumbe mwenza wake kuwa 'kama ulinitamani uliponiona katika mavazi haya siku hizo,basi hata sasa naweza kutamaniwa na wengine'.Kwa bahati mbaya,'tisha toto' hii inaweza kupelekea madhara yasiyokusudiwa.Kwamba akajitokeza mdau akaonyesha interest ya kutosha na hatimaye mwanadada akashawishika kutembea naye 'mara moja tu' (na hatimaye mara moja hiyo kuzaa mara ya pili na kadhalika na kadhalika).

Kuna wengine hawana hata muda huo wa kufikisha ujumbe na huamua kuingia kwenye hatua ya ku-cheat moja kwa moja.Hoja ya msingi kwao ni kwamba kama huwezi kunipa ninachohitaji basi kuna wengine w3anaweza kunipa.Na kwa vile mie na wewe sio dada na kaka basi sioni umuhimu wa kuishi na mwanaume au mwanamke ambaye hanitimizii mahitaji yangu ya kimahusiano.

Kama nilivyaondika awali,ningependa sana kuingia kwa undani na kujadili njia mwafaka za kusaka suluhisho kwa kila sababu ya ku-cheat niliyotaja hapa lakini kwa leo naomba niishie kwenye kutaja sababu tu,kabla ya kuhamia kwenye mada ya msingi ambayo ni hoja ya wanawake wengi kuwa Wanaume wa Kitanzania si waaminifu.

UCHAMBUZI

Kwa kifupi kabisa,naomba nikuachie msomaji uondoe MWANAUME WA KITANZANIA kwenye kila sababu niliotaja hapo juu na uweke MWANAUME WA KIKENYA,KIMAREKANI,KIINGEREZA au MWANAUME WA NCHI YOYOTE ILE.Kisha angalia kama kuna mwanaume wa uraia flani hawezi ku-fit kwenye sababu hizo hapo juu.

Kisha jaribu tena kuondoa MWANAUME (awe wa KITANZANIA au wa nchi nyingine) na uweke MWANAMKE WA KITANZANIA.Je hakuna mwanamke wa Kitanzania anayeweza ku-cheat kwa sababu tu ANALIPIZA KISASI (at least according to her)?Je hakuna mwanamke wa Kitanzania anayeweza ku-cheat kwa sababu tu anaamini KAMA KIPO KITUMIE?Au je hakuna mwanamke wa Kitanzania anayeweza ku-cheat kwa vile tu HATOSHEKI na anachopewa na mwenza wake?Na mwisho,je hakuna wanawake wa Kitanzania wanaoweza ku-cheat kwa minajili ya KUTULIZA ROHO kutokana na mapungufu yanayokabili mahusiano na wenza wao?

HITIMISHO:

Kwa kuangalia sababu hizo za kitaaluma as to kwanini wenza wanaweza ku-cheat,ni wazi kuwa,kwanza si mwanaume tu anayeweza kuwa na sababu (hata kama haikubaliki) ya ku-cheat.Na pili,si wanaume wa Kitanzania tu wanaoweza ku-apply sababu hizo wanapo-cheat,au kwa lugha nyingine,si wanaume wa Kitanzania tu wanao-fit explanations/sababu nilizobainisha hapo juu kuhusu kwanini watu wana-cheat.

Kwahiyo basi,natumaini makala hii inaweza kutoa jibu kwa niaba ya Wanaume wote wa Kitanzania wanaotuhumiwa kuwa si waaminifu katika mahusiano.Jibu ni kwamba si wanaume wa Kitanzania pekee,na si wanaume pekee,wanaoweza kuwa nasababu moja au nyingine ya ku-cheat.Makala hii haijaribu kwa namna yoyote kuhalalisha cheating kwa vile kama nilivyobainisha hapo mwanzo,ku-cheat si ufumbuzi wa tatizo lililopelekea mtu a-cheat.Faraja ya muda mfupi-iwe ni kulipa kisasi,kukidhi utafutaji ladha mbadala nje,kutibu kiu ya ngono au kujiliwaza-haiwezi kuwa ufumbuzi wa kukarabati uhusiano unaokwenda mrama.

Siku ya siku nitajadili njia mwafaka za kuboresha uhusiano na kuondoa fursa ya ku-cheat.

Inatosha kwa leo

20 Sept 2011


Kama ilivyozoeleka,blogu hii inaelemea zaidi katika masuala ya siasa.Lakini kuna nyakati ninajaribu kuangalia nyanja nyingine za maisha katika jamii.Na kwa bahati nzuri kabla ya kuzamia kwenye Siasa kitaaluma nilikuwa mwanafunzi wa Sosholojia (ndio mchepuo niliosoma katika Shahada ya Kwanza hapo Mlimani).

Ninajaribu kuanzisha utaratibu ambapo angalau mara moja kwa wiki nitajadili mada ya kijamii,hususan masuala ambayo ni ya kibinafsi zaidi kama vile mahusiano,mapenzi,nk.Nakaribisha michango na maoni kutoka kwa wasomaji.

Leo ninaanza na jinsi mwanaume anavyoweza kukabiliana na kuvunjika kwa uhusiano kati yake na mwanamke.Karibu sana.

JINSI YA MWANAUME KUDILI NA KUVUNJIKA KWA UHUSIANO NA MWANAMKE

Pointi tatu muhimu za kuzingatia:

  • Kwanza unapaswa kufuta kumbukumbu zote za uhusiano uliovunjika
  • Jaribu kutumia muda mwingi kuwa karibu na watu 'uliowapuuza' wakati ukiwa 'bize' na mwandani wako.Watu hao wanaweza kuwa familia yako,ndugu zako au marafiki zako
  • Kisasi kikubwa dhidi ya aliyekubwaga ni mafanikio.Kwahiyo hamasika kupata mafaniko ili 'ulipe kisasi.'
Hakuna anayeweza kubisha kwamba moja ya mambo magumu kwa manaume yoyote yule (na kwa wanawake pia) ni pale uhusiano na mwenza wako unapovunjika.Mara nyingi wanaume wengi wanapokumbwa na tatizo hilo hujipa matumaini potofu kwamba maisha yataendelea kama kawaida licha ya ukweli kwamba mioyoni mwao wanaumia vya kutosha.Wengi huendelea kujifariji na matumaini 'feki' kuwa wenza waliowabwaga watarejea.

Matokeo ya matumaini hayo 'feki' ni mithili ya mkuki wa kukataliwa wenye makali pande zote (double edged sword of rejection).Kwanza ni maumivu yanayotokana na ukweli kwamba umebwagwa,na kisha ukweli mwingine unaofuatia baadaye kuwa matarajio feki kuwa mwenza atarejea,well,yalikuwa feki.Mwenza wako ndio ameondoka moja kwa moja,na hatorejea (hapa tunazungumzia kubwagana ambako hakuna dalili wala uwezekano wa suluhu).

Lakini maumivu haya yanaweza kufupishwa kwa aliyebwagwa kutambua kuwa hali ndio hiyo-ameshabwagwa na hakuna uwezekano wa kurejea katika hali ilivyokuwa awali.Kuendelea kusubiri na kutarajia miujiza ni sawa na kujifungia kwenye mzunguko wa mateso usio na mwisho (endless circle of turture).

Kwahiyo ili kumudu kuendelea na maisha yako ya kawaida baada ya kubwagwa (au hata kubwagana) jaribu kufuata njia zifuatazo:

ACHA KUJILAUMU

Mara nyingi sie wanaume tumejenga tabia ya kuwa mithili ya watoto wakubwa (big babies) ambapo hatuachi kujilaumu.Kubwagwa ni kama kunaongeza ukubwa wa tabia hii.Kuna wanaochukulia kubwagwa kama mwisho wa dunia,yaani kana kwamba kuondoka kwa mwenza wako maishani mwako ni kama ameondoka na sababu ya wewe kuendelea kuishi.

Lakini ukijaribu kidogo tu kujiuliza "Niliishije kabla sijakutana na huyu aliyenibwaga?" utagundua kuwa ulikuwa ukiishi kama kawaida,na kama binadamu wengine.Kwahiyo,huu ni ushaidi tosha kuwa kama uliwahi kuweza kuishi bila mwenza aliyekubwaga ni dhahiri unaweza kuishi pia baada ya mwenza huyo kuondoka maishani mwako.Acha kujilaumu,jipange upya,na endelea kuishi.

FUTA KUMBUKUMBU

Kama nilivyoandika hapo juu,wengi wa wanaume wanaobwagwa huendelea kuwa na matumaini 'feki' kuwa mwenza aliyeamua kuondoka atarejea.Kwamba labda ni tisha toto tu,au anatikisha kiberiti tu.Mara nyingi wanaume tunapobwagwa hatupendi kukiri hadharani kuwa inatuuma.Wengi wetu hujifanya jasiri mbele ya 'washkaji' zetu tukijigamba kuwa 'ahh yule demu anadhani mimi nitababaika kwa vile tumeachana' (actually huwa tunakwepa kutumia neno 'kanibwaga').

Kiasili,katika mahusiano wanaume wengi wanapenda kuwa ndio walioshika usukani.Kwahiyo hata wanapobwagwa bado watajaribu kudanganya umma kuwa wao ndio waliokuwa wa kwanza kubwaga.Lakini kimsingi huko ni kujidanganya kwa sababu hao unaojaribu kuwaaminisha ujasiri wao hawajali sana (na pengine nao wana ishu zao binafsi zinazowanyima nafasi ya kujihangaisha na ishu zako).

Penigne una picha za mwenza aliyekubwaga,au zawadi mbalimbali alizokupatia wakati wa uhusiano wenu.Licha ya kubwagwa,unaweza kuogopa kuzitupa kwa hofu kuwa labda atarejea na akikuta azawadi alizokupatia hazipo atakasirika na kuondoka tena.Tumia akili yako vizuri.Ameondoka jumla,hatorudi.Usijaze bure nafasi kwenye albamu yako au kwenye sehemu unapoweka zawadi/kumbukumbu zako kwa matarajio hewa.

Uwepo wa kumbukumbu hizo (picha, zawadi,nk) ni sawa na uwepo wa mwenza aliyekubwaga kiroho japo si kimwili.Kila utakapoziona utaendelea kumkumbuka na kutamani awepo au arejee maishani mwako.Ukweli ni kwamba hatorejea.Cha kufanya basi ni kuteketeza kila kumbukumbu ya huyo aliyekubwaga.Hufanyi hivyo kwa ajili ya hasira bali ni kujipa nafasi ya kuendelea na maisha yako kama yalivyokuwa kabla hujakutana naye.Kumbuka,utakapopata mwenza mwingine hutazihitaji kumbukumbu hizo,sio tu kwa vile tayari una mwingine lakini pia itamsaidia mwenza wako mpya kupata uhakika kuwa wewe ni wake peke yake.

JIREJESHE KWA ULIOWATELEKEZA

Wengi wetu tunafahamu jinsi mapenzi motomoto yanavyoweza kutuweka mbali na watu wetu wengine wa karibu.Si kwamba tukiwa kwenye mapenzi tunawasahau watu hao lakini mara nyingi ni maotkeo ya kuweka akili na nguvu zaidi kwenye mahusiano yetu na wenza wetu,na hivyo kupata fursa finyu ya kuwa karibu na watu wetu wa karibu (kwa mfano wanafamilia wenzetu,ndugu,jamaa na marafiki).

Kufanya kosa si kosa bali kurejea kosa.Na alimradi wakati uko na mwenza wako hukuwafanyia dharau watu wako wa karibu basi ni dhahiri utakaporejea kwao (na pengine kuwafahamisha bayana kuwa umebwagwa) watakuwa radhi kukupokea.Kuwa karibu na watu wako wa karibu kutakusaidia sana kukarabati maisha yako,hasa kwa vile walikuwa nawe hata kabla hujakutana na huyo aliyekubwaga.

Kumbuka,mara nyingi hawa ni watu wanaokupenda kwa dhati- aidha kwa vile ninyi ni damu moja au ni watu uliopitia nao kwenye milima na mabonde.Kwa wanafamailia na ndugu,hawa kiasili ni watu ambao tunapaswa kuwa nao kwa vile tofauti na uchaguzi tunaokuwa nao kudeti mtu fulani au la,sheria za kibinadamu hazitupi fursa ya kuchagua nani tuzaliwe naye au atuzae.Ukaribu na watu wako wa karibu utasaidia kukukumbusha nani mwenye umuhimu wa kweli katika maisha yako.

USIKURUPUKE 

Hapa unaonywa usikurupuke kutaka kuanzisha uhusiano mwingine kuziba pengo la yule aliyekubwaga.Uzoefu unaonyesha kuwa mara nyingi jitihada za haraka haraka kutaka kuziba pengo hilo huishi kwenye maumivu/majonzi zaidi kuliko mafanikio.Tatizo kubwa hapa ni kwamba katika papara ya kutaka kuziba pengo hilo,unaweza kukosa muda wa kumwelewa vyema huyo 'unayemfukuzia.' Mara nyingi jitihada hizo huelemea zaidi kwenye kupata 'demu bomba zaidi ya yule aliyenizingua.' Lakini kama wasemavyo waswahili,usione vyaelea vimeundwa.Huyo 'demu bomba' anaweza kuwa na mwenza wake au ana 'pozi nyiiingi' ambazo sana sana zitaishi kukuumiza tu.

Suluhisho ni 'kutuliza boli.' Vuta pumzi.Angalia sababu zilizopelekea ukabwagwa au mkabwagana na mwenza aliyetangulia.Ukishaelewa chanzo/sababu itakupatia nafasi nzuri ya sio tu kuepuka kurejea makosa ya awali bali pia kujenga uwezekano wa kupata mtu aliye bora zaidi ya aliyetangulia.

JIHAMASISHE

Wengi wetu tunapobwagwa tunakuwa mateka wa hasira.Na katika hasira hizo baadhi yetu hujikuta tukifanya vitu vya kitoto,kijinga na visivyo na maana kabisa.Si ajabu kuona mtu akibwagwa akakimbilia kwenye waal ya Facebook profile ya aliyembwaga na kutundika 'madudu' yenye lengo la aidha kumuumiza mhusika au kujaribu kumshawishi arejee.Unaweza kukidhi mahitaji yako kwa dakika au siku chahe lakini mara nyngi matokeo ya 'upuuzi' wa aina hiyo huwa sio mazuri hasa pale utakapobaini kuwa 'kujigonga' kwako hakujafanikiwa kubadili msimamo wake.

Kumbuka,aliyekubwaga anaweza kuwa anafuatilia kwa karibu namna unavyodili na uamuzi wake.Matarajio ya wengi wanaobwaga wenza wao ni kuwa aliyebwagwa ataumia,atakonda,atateseka au,kwa hakika,ataaanza kubembeleza.Hiyo ni attention seeking.Na hakuna dawa mwafaka kwa attention seekers kama kuwapuuza.Kuendelea na maisha yako kana kwamba hakuna lililotokea sio tu itakuwa kama kumwadhibu attention seeker aliyekubwaga (ie kuvunja matumaini yake kuwa amekuumiza na labda utambembeleza) bali pia utakuwa unajisaidia wewe mwenyewe kuendelea na maisha yako kama kawaida.

Kisasi kikubwa kabisa kwa aliyekubwaga ni kwa wewe kupata mafanikio.Yaani badala ya wewe kuonekana umekondeana kwa mawazo ya kubwagwa,siku ya siku unakutana na aliyekubwaga na kukuona ukiwa mwenye furaha na mafanikio.Na kwa vile 'what goes around always comes around' si ajabu aliyekubwaga kwa wakati ho atakuwa anajutia kwanini alichukua uamuzi huo-lakini hawezi kukubembeleza mrejeane kwa sababu yeye ndiye aliyeamua bila kulazimishwa kuwa mwachane.

Pata picha,baada ya kubwaga unaelekeza nguvu zako kwenye kujiendeleza kimaisha (kitaaluma au kikazi),unatumia muda wako kujenga mwili wako kwa mazoezi, na kwa vile Mungu humjalia kila anayejituma,unafikia mafanikio yanayoweza kugeuza shingo za watu (ya kutamanisha).Mafanikio ni sawa na sumaku,lazima yatakusaidia kuongeza nafasi zako za kupata mwenza bora,pengine bora zaidi ya yule aliyekubwaga.Sasa siki ua siku,mwenyewe umenawiri vyema kutokana na kazi inayolipa vyema,na pembeni una mwenza bora,kisha unakutana na aliyekubwaga awali akiwa kachoka kimaisha na pengine akiwa na mwenza wa ovyo ovyo.Anashindwa kujizuia na kujikuta anakuuliza "hey fulani uko wapi siku hizi...naona mambo si mabaya..."Usiwe na haraka ya kujibu bali jitahidi kadri uwezavyo kuachia kicheko cha dharau....na badala ya kujibu swali lake mkebehi kwa kurejea swali lilelile na pigiria msumari kwa "hata wewe naona mambo si mabaya"...na kicheko kingine..Hiyo inaitwa kushinda vita bila kwenda vitani.

AMKA NA ENDELEA NA SAFARI

Vyovyote utakavyofanya huwezi kumzuia mwenza aliyedhamiria kukubwaga.Pengine amepata mtu aliye bora zaidi yako,pengine ameamua tu.Kama binti anatamani kuwa na mtu mwenye uwezo mkubwa kifedha kuliko wewe,kuendelea kumbembeleza mwendelee kuwa pamoja kutakuingiza kwenye vishawishi vya ufisadi,au matendo mengine mabaya ambayo si ajabu badala ya kukusaidia kumridhisha mwenza wako yakaishia kukupeleka jela.Naamini umeshaona au kuskia stori kibao za watu waliolazimika kujiingiza kwenye uhalifu ili kupata fedha za kuwaridhisha wenza wao.

Of course,mwenza wako ana haki ya kutaka kilicho bora.Lakini hiyo sio sababu ya kutaka uurefushe mkono wako zaidi ya uwezo wake.Mwneza wako ana haki ya kukupa changamoto za koboresha maisha yako/yenu lakini sio kwa namna ya kukusukuma uhatarishe maisha yako kwa ajili yake.Kumbuka,kama maisha yake ni muhimu,yako ni muhimu pia.Kama anakupenda kwa dhati atakubaliana na hali yako alimradi isiwe hali yako ni matokeo ya uvivu au uzembe wako au uoga wako kijituma.

Kwa hiyo badala ya kuendelea kuifanya hali ngumu (kubwagwa) kuwa ngumu zaidi,futa machoz yako,amka na endelea na maisha yako.Katika saikolojia kuna imani kwamba mengi ya tunayoyaita matatizo ni matokeo ya fikra zetu tu.Njaa,kwa mfano,si lazima imaanishe mahitaji ya mwili (tumbo) bali ni fikra kuwa tumbo linahitaji kitu fulani.Tamaa ni hali ya kutamani usichokuwa nacho hata kama si cha muhimu.Badala ya kujipa moyo kuwa mwenza wako atarudi aua atajilaumu kukubwaga,kwanini usielekeze fikra zako kwenye masuala mengine ya muhimu katika maisha yako?Kumbuka wewe ndiye nahodha ya maisha yako,kumkabidhi mtu mwingine jukumu hilo sio tu kunaondoka uhuru wako wa kukufikisha unakotaka kwenda bali pia kuna hatari ya kupotezwa.

Kwa leo inatosha!

MAKALA HII IMEANDALIWA KUTOKANA NA VYANZO MBALIMBALI MTANDAONI HUSUSAN MTANDAO WA AskMen 

MAKALA IJAYO ITAZUNGUMZIA IMANI ILIYOJENGEKA MIONGONI MWA MABINTI/WANAWAKE WENGI WA KITANZANIA KUWA WANAUME WA KITANZANIA NI MAHIRI KWA KU-CHEAT,AU KUNUKUU KIUSAHIHI, "OVYO KABISA", "BURE KABISA", "CHU*I MKONONI", NA KAULI KAMA HIZO.KICHANGAMSHA UBONGO: JE TABIA YA MWANAUME (AU MWANAMKE) INA MAHUSIANO YOYOTE NA URAIA WAKE?

HADI MUDA HUO,NAKUTAKIA SIKU NJEMA


18 Aug 2011



 Mimi ni Mtanzania halisi niliyezaliwa miaka 38 iliyopita jijini Arusha maeneo ya Sanawari. Niliamia hapamiaka 5 iliyopita baada ya kuonana na mme wangu kupitia njia kama hii (Cyber-love). Nina motto 1 na ninaishi maisha tu ingawa ni ya kawaida. Hivyo nimeona ni vyema nikatoa nafasi kama kwa watanzania wengine ambao wangependa vilevile kuonana na marafiki wengine popote duniani kupitia blog hii ya WabongoMeet.

Wabongomeet ni blog ya Kitanzania inayotoa mwanya kwa watanzania mahali popopo kujitafutia marafiki, wachumba mume/mke ulimwenguni kote. Mnakaribishwa bila ubaguzi wowote. 

AKINA DADA MNAKARIBISHWA NAWAPA MOYO ZAIDI KUTEMBELEA HAPA http://wabongomeet.blogspot.com
Kwa wale wote ambao watapenda kuweka picha pamoja na info zao tafadhali tuma kwa kupitia email [email protected], Pia nakaribisha maoni yenu.


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.