Showing posts with label Muziki na burudani. Show all posts
Showing posts with label Muziki na burudani. Show all posts

9 Nov 2014

Embedded image permalink
Gazeti la The Citizen la Tanzania linamwita 'lulu iliyofichika' (hidden gem, kwa kimombo). Huyu ni Leo Mkamia, msanii wa Kitanzania na mwanzilishi wa aina ya muziki ujulikanao kama 'Swahili Blues.'

Siku chache zilizopita, Leo alirekodi wimbo wake mpya uitwao 'Pamoja.' Miongoni mwa yatakayoonekana katika video ya wimbo huo ni performance ya kihistoria ya msanii huyo katika moja ya vyuo vikuu vikubwa hapa Uingereza, Nottingham University, ambapo Leo alifanikiwa kuwaimbisha Kiswahili baadhi ya wahadhiri na wanafunzi wa chuo hicho kikuu. Katika shughuli hiyo, Leo aliimba na kwaya ya Nottingham Academy.

Kinachomfanya Leo kuwa msanii wa kipekee kutoka Tanzania kuwa na fursa kubwa ya kutawala anga za muziki kimataifa ni ukweli kwamba amefanikiwa kuanzisha kitu kipya- muziki aina ya Swahili Blues- na ambao tayari umeanza kukubalika kimataifa.

Mtaji mkubwa wa Leo ni ukweli kwamba anatoka familia ya muziki.Unamkumbuka mkongwe wa gitaa Henry Mkanyika? Basi huyo ni baba mzazi wa Leo, ambaye alianza kucharaza gitaa akiwa na umri wa miaka minane tu.

 

Kwa sasa Leo ni miongoni mwa wasanii wachache mno, sio tu wa Tanzania, bali Afrika nzima kwa ujumla, ambao sura na sauti zao sasa 'zimezoeleka kwenye vituo vya radio na televisheni vya kimataifa kama BBC. Na katika kuthibitisha hjilo, Leo alihojiwa na BBC mara baadha ya performance hiyo ya kihistoria huko Nottingham.



Pamoja na kufanya vizuri kimataifa, Leo bado anathamini asili yake. Kama video ya pili inavyoonyesha, Leo alifanya mahojiano na mtandao mkubwa na maarufu wa burudani Tanzania na Afrika kwa ujumla wa Bongo5. Kadhalika, msanii huyo anapata sapoti kubwa kutoka kwa mmoja wa waasisi wa muziki wa Hip-Hop nchini Tanzania, lejendari @XamiaSiku4Saa4 wa kundi maarufu kabisa la Kwanza Unit. Ieleweke kwamba katika shughuli za muziki, kupata 'endorsement' ya mkongwe wa muziki ni uthibitisho kuwa msanii husika anafanya kazi nzuri mno.

Kama Watanzania, tuna wajibu na kila sababu ya kumuunga mkono Leo, kwani sio tu anaitangza Tanzania yetu bali pia anautambulisha utamaduni wetu-kwa maana ya lugha ya Kiswahili- kupitia muziki wake wa Swahili Blues.

Unaweza kufuatilia maendeleo yake ya kimuziki kwa akaunti zake mbalimbali za mitandao ya kijamii: Twitter na Facebook  na katika tovuti yake sambamba na ukurasa wake wa YouTube









13 Sept 2014

Happy birthday @ommydimpoz one of the most down-to-earth superstars I have ever known…his common sense always ahead of fame, his humility always infront of his celebrity status: respectful, wise and simply a good guy! God loves us all, but He loves good people even more. May Allah bless you with all the best He offers to sie viumbe wake…and keep on being the good&humble person you always are. Enjoy your big day!
Leo ni siku ya kuzaliwa ya mmoja ya wasanii maarufu kabisa huko nyumbani na hata duniani, Ommy Dimpoz. Nilifahamiana na Ommy kupitia Twitter, na tangu wakati huo sijawahi hata siku moja kujilaumu kufahamiana nae. Tofauti na hisia zilizotapakaa katika jamii kuwa watu maarufu mara nyingi huwa 'watu wa kujiskia,' kwa Ommy ni tofauti kabisa. Katika mawasiliano tuliyowahi kuwa nayo kupitia Twitter ameonyesha ni kijana mstaarabu, mwenye heshima na ni vigumu kuamini kuwa ni mmoja wa watu maarufu kabisa kwa sasa huko nyumbani na nje ya mipaka ya nchi yetu.

Na sio Ommy Dimpoz pekee. Kitu kimoja nilichojifunza katika kufahamiana na wengi wa ma-celeb wetu ni utu wao. Orodha ni ndefu lakini kwa uchache tu, nilichokutana nacho kwa Ommy Dimpoz ndicho nilichokutana nacho kwa Mwana FA, Profesa Jay, AY, Fid-Q,Solo Thang,Lameck Ditto, Cindrulz,Grace Matata,Mkoloni, Albino Fulani na hata wakongwe wa fani ya Bongoflava kama @XamiaSiku4Saa4 wa waasisi wa Bongoflava Kwanza Unit, na wengineo wengi.Tumekuwa tukiheshimiana tangu siku ya kwanza 'tulipofahamiana' mtandaoni.

Lakini si kwa Bongoflava tu kwani hata mastaa wengine kama Sinta, Flaviana Matata, Sporah Njau, Batuli, Seki, Masanja Mkandamizaji, Sheria Ngowi, Michael Mlingwa Masudi Kipanya na wengineo wengi ni watu ambao kwa hakika sijawahi kujutia kufahamiana nao kwenye mitandao ya kijamii.

Na kwenye 'anga' nyinginezo VIPs kama Mawaziri Lazaro Nyalandu, Januari Makamba, wanasiasa kama John Mnyika, Faustine Ndugulile, Halima Mdee, Hamis Kigwangalla, William Ngeleja na Lawrence Masha, sambamba na waheshimiwa wana-Afrika Mashariki Shyrose Bhanji na Abdullah Mwinyi, hali ni hiyo hiyo, unafahamiana na watu mtandaoni na wanakuwa kama 'asset' muhimu maishani kwa aidha kujifunza kutoka kupitia mafanikio yao au ustaarabu walionao mtandaoni.

Makala hii haitoshi kuwataja watu wote maarufu niliofahamiana nao kupitia mitandao ya kijamii, lakini ninachoweza kubainisha bayana ni ukweli kwamba kuwa-follow watu maarufu kunapunguza sana usumbufu kwenye mitandao ya kijamii. Pengine ni kwa sababu wanatunza heshima yao lakini pengine ni ukweli kwamba mafanikio ni mwalimu mzuri wa maisha, na wengi waliofanikiwa watakwambia kuwa moja wa mitaji mikuu ya mafanikio ni kuwaheshimu watu wengine kama wanavyokuheshimu.

Lakini ninaomba nibainishe waziwazi kwamba kama ilivyo katika maisha halisi 'mtaani' au duniani, heshima haihitaji mtu awe maarufu au wa kawaida. Kwa mantiki hiyo, ninachopigia mstari hapa si kwamba watu wote nilofahamiana nao mtandaoni nimaarufu, au watu wasio na umaarufu hawana faida. Hapana. Kuna maelfu ya watu 'wa kawaida tu' ambao kwa hakika wamenisaidia sana kuwa mtu bora zaidi ya nilivyokuwa kabla ya kufahamiana nao.

`Binafsi, moja ya vitu ninavyovithani ni mno ni utu na unyeyekevu. Kwa bahati mbaya (au pengine bahati nzuri) nilikulia katika familia isiyo na uwezo mkubwa. Sijisifu, lakini laiti nisingekuwa na akili ya darasani basi hata kuhitimu kidato cha nne ingekuwa mgogoro kwani wazazi wangu hawakuwa na uwezo wa kumudu gharama japo kiduchu za wakati ninasaka elimu maana hata ada ya elimu ya O'Level ikuwa mgogoro japo mwanzoni ilkuwa Shilingi 1,500 tu. Kubwa lililonisaidia ni kuishi na watu vizuri, unyenyekevu na heshima kwa kila mtu.

Lakini kibaya nilichojifunza katika maisha yangu mtandaoni ni ukweli usiopendeza kwamba  wengi wa wasumbufu mtandaoni ni wale wasio na moja la kujivunia: wenye umaarufu kutokana na mambo ya ovyo ovyo kama matusi na bullying, na wengine ni wenye kamera zenye IQ kubwa kuliko wao wenyewe  lakini wanahangaika kusaka umaarufu kwa kuwachafua watu waliowazidi kiakili/uwezo kuliko ukoo wao mzima.

Japo yawezekana kuwapo kwa watu maarufu wenye tabia zisizopendeza (japo sijawahi kukutana nao mtandaoni, na hata ningetakana nao ningewakwepa kwa sababu kanuni yangu kuu ni kuthamini utu wa mtu na si vitu alivyonavyo), lakini kwa hao niliofahamiana nao wamewezesha maisha yangu mtandaoni na katika dunia halisi kuwa ya amani na furaha. Uzoefu waonyesha kuwa watu wasumbufu sana, hususan mtandaoni, ni wale wasio na kitu chochote cha maana lakini wanajaribu kuihadaa dunia kuwa 'nao wamo.' Ushauri wangu mwepesi ni huu: kamwe usifuatane na mtu asiye na mwelekeo unless awe mtu anayejielewa kuwa mtaji wake mkubwa licha ya 'kutokuwa na kitu' ni utu wake.

Basi nimalizie makala hii maalum kwa ndugu yangu Ommy Dimpoz kwa kumtakia kila la kheri maishani nikitaraji watu wengine 'wenye majina' watajifunza mengi kupitia unyenyekevu wake ambao nina hakika unachangia sana katika mafanikio yake makubwa. Ninamwombea aendelee kuwa mfano kwa watu wengine maarufu kwa kujali utu kuliko vitu, kuendelea kuwa mnyenyekevu hasa kwa vile unyenyekevu una mvuto zaidi kuliko nyodo, mapozi na tabia nyingine zisizopendeza. 

Na kwa wasumbufu wanaosaka umaarufu kwa kuwasumbua wenzao, sina maneno mazuri wala ushauri wa busara wa kuwaeleza zaidi ya kuwakumbusha kuwa huwezi kumwangusha mtu mwema/bora. Kujuana na watu maarufu hakukufanyi nawe kuwa maarufu. Na hata kama watu maarufu watakuwa karibu nawe kwa 'upuuzi wako' basi ni wazi kuwa umaarufu huo utabaki kuwa kama mapovu, muda si mrefu hupasuka.

Happy birthday Ommy Dimpoz na shout out kwa kila mtu maarufu anayejali utu, mwenye heshima, mnyenyekevu na anayetambua kuwa mtaji mkubwa wa binadamu ni watu- marafiki- kuliko maadui.



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.