Showing posts with label NYOTA. Show all posts
Showing posts with label NYOTA. Show all posts

18 Jan 2011


Jana niliona mahala flani kuwa nyota (star signs) zimebadilika.Sikujali.Lakini leo katika pitapita zangu mtandaoni,nimebaini kuwa sio tu kuwa nyota zimebadilika bali pia nyota yangu imekumbwa na mabadiliko.Nilizaliwa Desemba 9,hivyo nyota yangu ilikuwa Mshale au Sagittarius,kama inavyojulikana.Sasa baada ya kuongezeka alama nyingine ya nyota,nimejikuta nikiwa katika alama nyingine ya nyota,OPHIUCHUS.Grrrrr!!!!

Najua imani yangu ya dini inakemea mambo ya unajimu.Lakini,siku za nyuma nili-develop interest kwenye masuala ya nyota baada ya kuanzisha safu kwenye lililokuwa  gazeti maarufu la SANIFU,kabla sijahamishia safu hiyo kwenye gazeti la KASHESHE.Naamini kwa walikuwa wafuatiliaji wa magazeti ya "manyang'unyang'u" waakuwa wanakumbuka tangazo la Anko J Julius Nyaisanga akiwaasa wasomaji kutokosa safu ya USTAADH BONGE.Hiyo ilikuwa mika ya 1997-2000.

Naam,Ustaadh Bonge huyo ndiye mie,truly yours Evarist Chahali.Kuna waliokuwa wanaamini nyota hizo za "kizushi".Nakumbuka wakati huo ambapo nilikuwa mwanafunzi hapo Mlimani (UDSM) kuna baadhi ya watu walifikia hatua ya kuomba "msaada" wangu kuhusu fate zao kinyota.

Na safu hiyo ikaniacha na monikers kama "Ustaadh", "Bonge" au "Ustaadh Bonge",ambayo kwa baadhi ya marafiki zangu,ndio pekee wanayofahamu kuhusu mie.

Looking back,I can't help but just laugh.Good old days za "Kijiweni" nyuma ya ATB "tulipokuwa tunahudhuria masomo kwa kile tulichokiita correspondence" ie mtu mmoja atakaeingingia kwenye mhadhara (lecture) ndiye atakayesambaza contents za kilichofundishwa"!!!However,when the UEs came,we all managed to smash them.
"KIJIWENI" ni kulia kwa picha hii ie nyuma ya ATB

Missing you guys,Ghetto Boy (sasa ni bosi mahala flani), "Dogo" Baraka (naye pia ni bosi katika kampuni moja ya kigeni),Adam Mkula,Busa Musika,Aden,Iku, "Sospiere",Chrisant, Swedi Mlanzi, Bitebo,Manzi,Eric (wape hi Skandinavia), "Queen Latifa",Faith Msina,Belinda,Leila,Kassim,na wengineo.You made our days at the uni one experience that I will never ever forget!!!!

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.