Showing posts with label PALM TREO 650. Show all posts
Showing posts with label PALM TREO 650. Show all posts

9 Nov 2007

Ukurasa wa mbele wa gazeti la RAIA MWEMA



Makala kamili bonyeza hapa
----------------------------------------------------------------------------------------------------------------
SHUGHULI YA 50 CENT NDANI YA ABERDEEN

Jana kulikuwa na burudani ya aina yake hapa Aberdeen.Rapa mahiri kutoka USA,50 Cent alifanya concert "la kufa mtu" katika ukumbi wa AECC ambapo maelfu ya mashabiki walijitokeza.Baada ya kupelekeshana na shule yangu,niliona ni wazo zuri kwenda kupumzisha akili maeneo hayo,pamoja na kupata picha mbili tatu za ku-share nanyi wasomaji wa blogu hii.

Baada ya kusota kwenye foleni ndeeefu,hatimaye nilitia mguu ndani ya ukumbi.Kwa bahati mbaya mie ni mzembe flani linapokuja suala la "namba" (hesabati) na hivyo nashindwa hata kukadiria idadi ya watu waliojazana ukumbini humo.Lakini nadhani kulikuwa na makumi ya maelfu ya watu,may be 10,000 may be 50,000.Labda nituie "njia za uswahilini" kuelezea urefu wa foleni ili kukupa idea ya watu waliojitokeza .Nilipofika eneo hilo kulikuwa na "mnyororo wa watu" kwa umbali sawa na kuanzia kituo cha basi cha Morocco hadi Mkwajuni (kwa makadirio ya chini).Kwa bahati mbaya sikubahatika kupata picha ya foleni hiyo.

Warming up ya ukumbi ilifanywa na DJ maarufu WHOO KID,


ZAIDI KUHUSU DJ WHOO KID CHEKI HAPA

Concert lilifunguliwa na rapa mwingine mahiri FABOLOUS.Roho yangu ilisuuzika vilivyo pale rapa huyo alipopiga kibao ambacho nimekisevu kwenye collection yangu katika Palm Treo yangu (bado natumia Treo 650-chuma cha pua hicho).Kibao hicho kinaitwa Breathe.Nilikirekodi lakini memory kwenye simu yangu ikanifanyia uhuni,ikajaa kabla wimbo haujaisha.



Baada ya burudani nzito ya FABOLOUS,ilifuatia zamu ya 50 CENT akishirikiana na LOYYD BANKS.Nachosikitika ni kwamba nilifanya uzembe wa kutosoma manual ya kiji-Casio Exilim EX-Z75 changu kabla sijaondoka maskani kwangu.Nikiri kuwa jana nilikuwa naitumia kamera hiyo kwa mara ya kwanza,na baada ya memory ya simu kujaa,nilitaraji ningerekodi sehemu kubwa ya concert hiyo kwa kutumia kamera hiyo.Ah wapi,kila nikibonyeza hiki inakuwa vile,basi mwishowe nikaamua kupiga picha tu badala ya kurekodi video.Picha zenyewe ndio hizo (nilifanya uzembe mwingine wa kutotumia anti-shake setting ya kamera ndio maana picha zenyewe haziko clear sana.Anyway,wakati mwingine tunajifunza kutokana na makosa).Hebu ngoja niache picha hizo zizungumze zenyewe.


SHUGHULI INAANZA KUCHUKUA KASI

BURUDANI

50 CENT NA LOYYD BANKS

KWENYE HUO MSITU WA HAWA WHITES NI VIGUMU KUDHANI NA SIE WENGINE TULIKUWEPO

MIKONO JUU....

NI MAPENZI KWA 50 CENT AU KUKUBALIKA KWA HIP-HOP BEYOND HIMAYA YA BLACKS?

PEOPLE WERE ASKING WHERE IS YOUNG BUCK?WHERE'S TONY YAYO?

WASKOTISHI WALICHENGUKA SI MCHEZO

MATAA

50 CENT NA LOYYD BANKS

LOYYD BANKS AKIWAKILISHA

50 CENT AKIRUSHA SNEAKERS ZAKE ZA G-UNIT KAMA KUMBUKUMBU KWA MASHABIKI

50 CENT AKIJIANDAA KURUSHA T-SHIRT YAKE YA G-UNIT KWA MASHABIKI

MAMBO YA MEGA SCREEN HAYO
VINNI VIDDI VICCI

Nimalizie kwa burudani hii ya 50 CENT katika video ya Piggy Bank (huyu jamaa hajambo kwa "kuponda") na hii ya FABOLOUS ya So Into You (I hope you take note of my favourite video vixen KD Aubert).Talkin of Video Vixens,I can't stop looking at the way these ladies dance in the background,and so is huyu vixen aliye kati katika in most scences.Kwa kumalizia,ni huyu innocent looking vixen na message ya Skinnyman katika soundtrack ya movie Kidulthood.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.