Showing posts with label PRAHLAD JANI. Show all posts
Showing posts with label PRAHLAD JANI. Show all posts

11 May 2010

Inaelekea habari kwamba raia mmoja wa India ameweza kuishi kimiujiza kwa kwa kutokula au kunywa chochote kwa miaka 70 sio fiksi bali ni kweli kabisa.Prahlad Jani ameimshangaza timu ya wanajeshi waliokuwa wakimchunguza kwa wiki 2 sasa kuthibitisha madai hayo.

Mtu huyo amekuwa chini ya uangalizi katika hospitali moja katika jimbo la Gujarat huku madaktari wakifuatilia kila jambo kwa kutumia kamera na CCTV.Kwa muda wote huo,hajawahi kula au kunywa chochote wala kwenda msalani.

"Bado hatufahamu ni namna gani anaweza kustahimili",anasema mtaalam wa mfumo wa fahamu Sudhir Shah alipoongea na waandishi wa habari baada ya uchunguzi huo."Bado ni muujiza usioweza kuelezeka kisayansi".

Prahlad,mwana-Yoga (Yogi) mwenye nywele ndefu na madevu aliwekwa hospitalini ili kuchunguzwa na taasisi ya utafiti na maendeleo ya ulinzi ya India (DRDO),ambapo ilitarajiwa kuwa matokeo ya uchunguzi huo yanaweza kusaidia kuwasaidia wanajeshi kumudu kuishi bila kula au kunywa chochote (kwa mfano wanapokuwa vitani),wanaanga na hata kuokoa maisha ya wengi yanapotokea majanga ya asili.

"Muda pekee Jani aligusa kimiminika ni wakati anasukutua na kuoga kwa vipindi maalum wakati wa uchunguzi huo",anasema G. Ilazavahagan,mkurugenzi wa taasisi ya ulinzi ya saikolojia na stadi shiriki (DIPAS).

Mtu huyo sasa amerejea kijijini kwake Ambaji,kaskazini mwa Gujarat,ambako ataendelea na taratibu zake za Yoga na uwazo (meditation).Anasema alipata karama alizonazo udogoni  kutoka kwa 'mungu wa kike' na tangu wakati huo amekuwa na uwezo wa ajabu.

Katika uchunguzi huo wa siku 15 uliohitimishwa Alhamisi iliyopita,madaktari walichukua vipimo (scans) vya viungo,ubongo na mishipa ya damu pamoja na vipimo (tests) vya moyo,mapafu na uwezo wake wa kufikiri.Matokeo zaidi ya uchunguzi wa vinasaba (DNA analysis),molekyuli za kibiolojia na vipimo vya homoni zake,enzymes na uzalishaji nishati mwilini (energy metabolism)  utatolewa hapo baadaye.

"Kama Jani hazalishi nishati ya mwili kutoka kwenye chakula na maji basi anapata nishati hiyo kutoka vyanzo vingine vinavyomzunguka kama vile mwanga wa jua",anaeleza Shah."Kama wataalam wa utabibu hatuwezi kufumbia macho uwezekano wa kuwepo vyanzo vingine vya nishati ya mwili zaidi ya kalori".

Habari hii imetafsiriwa kutoka AFP.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.