Showing posts with label Pharma-Plant. Show all posts
Showing posts with label Pharma-Plant. Show all posts

20 Jul 2011



Majaribio yameanza ya kinga inayotokana na mimea kutumika kama kinga dhidi ya virusi vinavyosababisha upungufu wa kinga ya mwili (UKIMWI).Kinga hiyo inatengenezwa kwa kutumia majani ya tumbaku iliyozalishwa maabara,ikitarajiwa kuwa ufanisi wake utapunguza gharama ya dawa za kurefusha maisha ya waathirika wa ugonjwa huo,na kwa muda mrefu kupata tiba ya kudumu ya ugonjwa huo.

Vidonge vilivyotengenzwa kutokana na mimea vinafanyiwa majaribio kwa kundi la wanawake hapa Uingereza,hasa kuangalia ufanisi wake.Watengenezaji wa vidonge hivyo wanategemea vitasaidia kupatikana kwa kinga dhidi ya maambukizo ya virusi vinavyosababisha ukimwi lakini mafanikio makubwa yanatarajiwa kwenye ukweli kwamba molekyuli zinazotarajiwa kuwa na ufanisi ni nafuu zaidi kwa minajili ya gharama.

Majaribio hayo katika miili ya binadamu yameidhinishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Madawa na Huduma za Afya ya hapa Uingereza,na inafanyika huko Guildford katika taasisi ya utafiti wa afya ya Chuo Kikuu cha Surrey.

"Pharma-Plant" ni mradi ulioanzishwa miaka saba iliyopita ukiwa na lengo la kutumia mimea iliyozalishwa maabara kupunguza gharama ya uzalishaji wa vidonge kwa ajili ya tiba mbalimbali.Wanasayansi wanadhamiria kutengenza madawa yenye ufanisi lakini kwa gharama nafuu,na kuzisaidia nchi masikini duniani.

Habari hii imetafsiriwa kutoka katika gazeti la Guardian.Kwa habari kamili soma HAPA

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.