Showing posts with label SILVIO BERLUSCONI. Show all posts
Showing posts with label SILVIO BERLUSCONI. Show all posts

24 Jun 2009

Pichani,Berlusconi akijifuta jasho baada ya kutwanga swali kwenye mahojiano na kituo kimoja cha runinga kuhusu tuhuma zinazoweza kuotesha nyasi ndoa yake na mkewe anayeonyeshwa kwenye background.

Waziri Mkuu wa Italia,Silvio Berlusconi,amekanusha madai kwamba alinunua huduma ya tendo la ndoa kwa changudoa mmoja,Patrizia D'Addario.Kiongozi huyo machachari na mwingi wa vituko,anakabiliwa na shinikizo la kisiasa kufuatia madai hayo ya kujimwayamwaya na kimada aliyekuwa miongoni mwa waliohudhuria pati iliyoandaliwa na Berlusconi.

Hadhi ya mwanasiasa huyo tajiri imekumbwa na migogoro lukuki,na hivi karibuni alikuwa na tuhuma za kuvunja amri ya sita na binti wa miaka 18,Noemi Letizia (pichani chini)


Kwa jeuri,Berlusconi amekanusha madai ya kununua ngono huku akikisitiza kwamba "Sijawahi kuona raha ya kununua ngono badala ya ujasiri wa kutongoza".
Vyama vya upinzani pamoja na Kanisa Katoliki wanamtaka Berlusconi kujieleza kuhusiana na skandali hiyo iliyoibuliwa na tume moja ya kuchunguza rushwa huko Italia ya kusini,ambapo inaelezwa kwamba kimada mhusika (kushoto,pichani chini) aliieleza tume hiyo kuwa alilipwa na Berlusconi ili kumpa huduma ya ngono na ana mkanda uliorekodi tukio hilo.

Yote haya yanajiri wakati mke wa Waziri Mkuu huyo akiwa kwenye taratibu za kuomba talaka huku akimtuhumu mumewe kwamba anapendelea sana dogodogo.

CHANZO: itn

Na sie tungekuwa na uhuru wa kuweka ishu kama hizi hadharani,sijui nani angesalimika among vingunge wetu!

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.