Showing posts with label Tabia za Binadamu. Show all posts
Showing posts with label Tabia za Binadamu. Show all posts

11 Oct 2011



Ubinafsi hauwezi kukusaidia kutengeneza marafiki wengi lakini inaelekea utakusaidia kupata mafanikio kazini.

Utafiti mpya umebaini kwamba watu wasio wabinafsi na wenye roho nzuri ndio wanaopendwa zaidi lakini wakati huohuo wameonekana kama wasiofaa kufukiriwa kwa ajili ya kupandishwa vyeo makazini.

Utafiti huo umeonyesha kuwa ujeuri na kiburi ni ishara za uwezo (nguvu) ilhali upole na wema unachukuliwa kama dalili za udhaifu.

Utafiti uliofanywa na Chuo cha Utawala ya Kellogg,Chuo cha Masomo ya ngazi ya juu ya Biashara cha Stanford na Chuo cha Biashara cha Tapper katika Chuo Kikuu cha Carnegie Mellon ulilenga kuchunguza aina ya maisha ya mtu tunayoihusisha na uongozi.

Katika mlolongo wa majaribio matatu,watafitiwa waliwekwa kwenye makundi,kisha watafiti walichambua tabia zao katika matumizi ya ishara zilizotumika kama fedha; jinsi gani baadhi waliamua kubaki na ishara hizo kwa ajili yao binafsi huku wengine wakiziingiza ishara hizo kwenye hazina ya kundi.

Wale wenye tabia za kibabe walionekana kama wenye tabia 'alpha' (alpha personalities).

Mhariri mwenza wa ripoti ya utafiti huo, Rober Livingston wa Chuo cha Biashara cha Kellog alieleza, "Kuwa mbinafsi kunafanya mtu aonekane anatawala,na kuonekana unatawala kunakufanya uonekana unafaa kuwa kiongozi,hususan pale penye ushindani."

"Akilini,watu wanalinganisha wema kuwa sawa udhaifu."

Dr Livingston anaamini kwamba tabia hii ya kuhusisha ubabe na uongozi inaweza kutoa maelezo kwani tunakuwa na rushwa.

"Watu wenye maadili,wema na wapenda watu wana nafiasi finyu ya kuteuliwa kushika majukumu ya uongozi," alisema msomi huyo.

"Hiyo inaongeza uwezekano wa rushwa na utendaji kazi kinyume cha sheria kwa sababu tunakuwa na watu wasiofaa kwenye nafasi za uongozi."

Lakini Bob Kaplan,Makamu Mwenyekiti wa Zamani wa taasisi ya fedha ya Goldman Sachs,na sasa Profesa wa kanuni za utawala katika Chuo Kikuu cha Harvard haafikiani na hoja ya utafiti huo.

Aliieleza tovuti ya Today.com kwamba maadili mema ndio kigezo kinachoweza kushauri kuhusu kiongozi anayefaa.

"Sisemi kwamba ili kuwa bosi lazima uwe mtu 'poa' lakini nadhani inabidi uwe na maadili,uadilifu na kushirikiana vema na watu, na kuwajenga watu," alisema.

CHANZO: Tafsiri isiyo rasmi kutoka gazeti la Daily Mail


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.