Showing posts with label Umoja wa Mataifa. Show all posts
Showing posts with label Umoja wa Mataifa. Show all posts

13 Jul 2012


Takriban wiki moja baada ya Naibu Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Dkt Asha-Rose Migiro, kurejea nyumbani Tanzania baada a kukitumikia chombo hicho cha kimataifa kwa kipindi cha miaka mitano, vyanzo vya habari ndani ya Umoja huo vinadokeza kuwa utendaji kazi dhaifu na kushindwa ku-fit katika 'taasisi hiyo kubwa na ngumu' ndio sababu zilizopelekea Mtanzania huyo kunyimwa fursa ya kurefusha mkataba wake wa kazi.

"Wadhifa wa Naibu Katibu Mkuu ni mgumu na wenye mahitaji mengi; unahitaji mtu mwenye uzoefu wa kuongoza Sekretariaeti (ya Umoja huo).Changamoto kubwa kwake ilikuwa kutofahamu siasa za chombo hicho na kutengeneza 'marafiki' (alliances)," kilieleza chanzo kimoja kwa Vox Media kupitia maongezi ya simu.

Imefahamika kuwa Dkt Migiro alijaribu kulishawishi Kundi la Afrika (Africa Group),linalounda asilimia 28 ya wanachama wote wa Umoja wa Mataifa,kuomba limsaidie 'kumpigia debe' ateuliwe tena,ombi ambalo lilikataliwa.

"Hakuwa maarufu miongoni mwa wanadiplomasia, kwahiyo hakuna aliyemsikliza. Pia ukumbuke kuwa uteuzi wake ulipingwa sana," kilieleza chanzo hicho.

Jijini Dar es Salaam, mjumbe mwandamizi wa zamani wa Sekretarieti ya chama tawala CCM  aliyewahi kufanya kazi na Dkt Migiro kabla hajateuliwa kushika wadhifa huo wa Umoja wa Mataifa alieleza kuwa uteuzi huo katika chombo hicho cha kimataifa ulitokana na ukaribu wa Dkt Migiro na Rais Jakaya Kikwete.

Inafahamika kuwa Rais Kikwete na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon walijenga urafiki katika kipindi wote wawili walipokuwa mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa mataifa yao.

Ilipofika wakati kwa Ban Ki-moon kuomba kura kushika wadhifa wake wa sasa, Tanzania ilikuwa mstari wa mbele kumsapoti,na kura ya Kikwete ilisaidia Migiro kuteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu.

Lakini Ki-moon alipoamua hivi karibuni kufanya mapitio ya timu yake nzima kwa minajili ya kukabiliana na upinzani mkubwa dhidi ya timu hiyo, ililazimika Dkt Migiro 'atoswe' kutokana na "utendaji kazi dhaifu na ukosefu wa uzoefu unaohitajika kwa watendaji wa ngazi za juu katika Umoja wa Mataifa."

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka Vox Media.Shukrani za pekee kwa mdau @mactemba kwa kunitumia kiungo (link) cha habari hii.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.