Wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiwa wamejilaza tayari 'kusulubiwa na gari la upupu' la FFU.Kosa lao ni kufuatilia haki na stahili zao. |
Wazee wetu wakipiga swala.Hivi Kikwete angewakalia kooni mafisadi wa Kagoda na wana-EPA wengine kisingepatikana japo kiasi cha mboga kuwatuliza wazee wetu hawa? |
Katika moja ya hotuba zake Bungeni,Kikwete alikumbushia umuhimu wa haki za kinadamu za mafisadi.Vipi kuhusu haki za msingi za wazee hawa wasio na hatia? |
Picha ya juu na chini: Wazee wetu wakijipoza kwa mlo baada ya awamu nyingine ya danadana za kupata haki zao.Natumaini wazee hawa wanafahamu nani ni kikwazo cha ufumbuzi wa tatizo lao.Haya ndio Maisha Bora aliyowaahidi Kikwete mwaka 2005.Na hiyo ndio Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya ya kutatua kero zenu.Bado mnatafuta sababu za ziada za kumnyima kura?
Picha kwa Hisani ya MICHUZI JUNIOR (Jiachie).Maelezo ya picha ni yangu binafsi.