4 Jul 2009



KWANZA Merged

Picha kwa hisani ya KENNEDY

Wanasema siasa ni mchazo mchafu.Lakini siasa katika bara letu la Afrika ni zaidi ya mchezo mchafu.Ni mchanganyiko wa kanyaboya,songombingo,mbinde,usanii,ufisadi na what have you.Hiyo sio kumaanisha kuwa siasa katika maeneo mengine,kama Ulaya na kwingineko ni safi kihivyo.Lakini angalau hawa wenzetu check-and-balance mechanism zinafanya kazi kwa kiasi kikubwa.Sie tunazo lakini aidha wenye majukumu ya kuzitumia wako bize sana na posho au nyumba ndogo au hawajui kwa nini wapo mahala panapopaswa kufanya hiyo check na balance.

Hivi CCM walikuwa wanafikiri nini mwaka 2005 kuahidi kuwa wangeshughulikia uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi?Binafsi sina tatizo na uanzishwaji wa mahakama hiyo as long as suala hilo linafanywa kwa uangalifu.Sio priority kwa sasa lakini kwa vile ni haki kwa Waislamu,then hakuna budi kuangalia uwezekano huo.Kwahiyo,CCM hawakufanya kosa "kukubali" kuanzisha Mahakama ya aina hiyo baada ya uchaguzi mkuu wa 2005.Hawakufanya kosa kwa vile wazo hilo sio baya au la hatari kama baadhi ya watu wanavyofikiria.Nitatafuta wasaa mwafaka siku nyingine kuelezea kwanini Waislam wako sahihi kudai mahakama hiyo na kwanini uanzishwaji wake hauna madhara kwa wasio waislam.In fact,suala sio "kuanzisha" bali "kurejesha" kwa vile mahakama za aina hiyo zilikuwepo wakati wa ukoloni na muda mfupi baada ya uhuru.

Kosa la jinai (yes,ni jinai) la CCM ni kutoa ahadi nyeti kama hiyo wakati inafahamu fika kwamba haina muda wa kuishughulikia.Ni kosa pia kwa vile pamoja na ahadi hiyo ya kuanzisha mahakama ya kadhi tayari chama hicho kilikuwa kimeshatoa ahadi nyingine lukuki kana kwamba kinaomba kutawala kwa miaka 100 na sio mitano (2005-2010)!Kulikuwa na ahadi za kuwakalia kooni wala rushwa,kushughulikia kero za Muungano,kuboresha maisha ya Watanzania,na ahadi nyingine kedekede.Si tu kwamba wakati tunaelekea mwishoni mwa miaka hiyo mitano rushwa imeshamiri na ku-mutate into ufisadi (kumbuka,neno hili limejitokeza katika kipindi hiki),kero za Muungano sio tu kuwa bado zipo ila tumeshuhudia "kibiriti kikitikiswa mpaka kinataka kulipuka",na hayo maisha bora kwa kila Mtanzania sanasana yamewezekana kwa mafisadi na washirika zao....

Hili la kuahidi kushughulikia masuala yanayogusa imani (ya kiroho) ilhali hakuna dhamira au uwezo wa kufanya hivyo ni jambo hatari mno.Dini ni hatari zaidi ya ukabila kwani inahusisha uhai na kifo (mtu akifa kwa ajili ya dini ni martyr,at least dini nyingi zinaamini hivyo).

Kauli za viongozi kuhusu suala hili sio tu zimekuwa za kujichanganya bali zimechangia kukuza tatizo hilo.Mara mchakato unaendelea,mara sheria za kiislam zitaingizwa kwenye sheria za mahakama za sasa (hicho tayari kinafanyika),mara hili,mara lile.Kama kawaida,wahusika wanasubiri lilipuke ndio watafute chanzo cha mlipuko.Unfortunately,milipuko mingine ikianza hata huo muda wa kutafuta chanzo hautokuwepo.Waulize Nigeria!

Tuiombee nchi yetu.

1 comment:

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.