8 Mar 2010


Blogu yako inaendelea kuja na mabadiliko ya hapa na pale lengo likiwa kukupatia wewe msomaji mpendwa 'ile kitu roho inapenda'.Katika kutekeleza azma hiyo,blogu hii inatarajia kuwaleta mahojiano na watu mbalimbali ambao kwa namna moja au nyingine wana mchango katika kulitangaza jina la nchi yetu. Kadri mambo yatakavyokwenda sawa,walengwa wa mahojiano hayo ni pamoja na wasanii wetu,wanasiasa (hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu),wanamichezo,pamoja na makundi mengine ya kijamii

Kwa vile blogu hii ni yako wewe msomaji mpendwa,na mimi ni mtumishi wako tu,basi nakaribisha maoni ya nani ungependa kuona anafanyiwa mahojiano.Mimi nitajaribu kutuma maombi ya mahojiano hayo,na nikifanikiwa,nitayatundika hapa bloguni.Ili kutoweka ubaguzi wa aina yoyote,blogu hii inakaribisha pia Mtanzania yeyote anayeona kuwa kwa nafasi yake na popote pale alipo anaiwakilisha Tanzania yetu kwa namna moja au nyingine.

Mahojiano hayo yatakuwa katika mfumo wa maandishi japokuwa mipango ya muda mrefu ni kuwa na mahojiano ya sauti pia,na ikiwezekana,mahojiano ya video.Kwa watakaotumiwa maombi ya mahojiano,au kwa wanaotaka kuhojiwa,hii inaweza kuwa fursa nzuri kwao kutangaza vipaji vyao au shughuli zao hususan nje ya Tanzania.Kadhalika,mahojiano hayo yatakuwa aidha kwa Kiswahili au Kiingereza kutegemea maafikiano na mhojiwa.Baadhi ya mahojiano hayo yatafanyika kwa Kiswahili na kutafsiriwa kwa Kiingereza ili kutoa fursa sawa kwa wasomaji wa blogu hii ambao hawafahamu Kiswahili.

Stay tuned, more to come in 2010.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.