20 Jan 2012



Unaweza kusema "aah,"kwani wasomaji laki tano ni wengi?Mbona kuna blogu kadhaa zimeshafikisha wasomaji milioni na ushee?" You could say that again,lakini kwangu haya ni mafanikio makubwa.Ni kweli kwamba blogu hii imekuwa hewani kwa takriban miaka 6 sasa,na pengine ingetarajiwa kuwa ingeshakuwa imetembelewa na idadi kubwa zaidi ya wasomaji kuliko hao laki 5 waliokwishatembelea hadi sasa.Ukweli mchungu ni kwamba Watanzania wengi si wapenzi wa habari zisizo za watu binafsi,au zile zisizoambatana na picha za "flani kafanya hiki,kavaa kile,kafumaniwa,kampora flani,nk."

Kuendesha blogu ya habari,uchambuzi na maoni kunataka moyo hususan iwapo bloga husika anatamani kuona wasomaji wengi wanatembelea blogu yake.Moja ya mambo ninayojivunia ni ukweli kwamba tangu ianzishwe,blogu hii ime-focus kwenye malengo yaleyale ya awali pasipo kushawishika kuingia kwenye nyanja nyingine kwa minajili tu ya kupata wasomaji wengi.Kinachonifariji zaidi ni uwepo la wasomaji waaminifu,yaani watu ambao angalau mara kadhaa kwa wiki ni lazima waipitie blogu hii hata kama haina post mpya.Ninafahamu kuhusu hilo kupitia michanganuo mbalimbali ya takwimu za wasomaji wa blogu inayoonyesha mahali walipo wasomaji  (kwa mfano Google Analytics,Stat Counter,nk).

Na kwa vile tangu mapema leo asubuhi "kaunta" ilikuwa inaonyesha kila dalili ya kutimia idadi hiyo ya wasomaji,niliamua kuongeza "feature" mpya ambapo sasa msomaji anaweza kuisoma blogu hii katika mionekano (sura) mbalimbali kama zinavyoonyesha picha zifuatazo.

Mwonekano wa CLASSIC

Mwonekano wa FLIPCARD

Mwonekano wa MAGAZINE

Mwonekano wa MOSAIC

Mwonekano wa SNAPSHOT

Mwonekano wa TIMELINE

Mwonekano wa SIDEBAR
Ili kwenda kwenye minekano hiyo,cha kufanya ni kubonyeza maandishi  mekundu "yanayotembea" kama inavyoonyesha picha ifuatayo


Utahamishiwa kwenye ukurasa utakaokupa uchaguzi wa kuamua unataka kuisoma blogu hii kwa mwonekano upi kati ya mionekano iliyotajwa hapo juu.Ukitaka kurejea kwenye mwonekano wa asili wa blogu hii (kama unavyoonekana katika picha ifuatayo),cha kufanya ni kurejesha nyuma ukurasa kwa ku-click kimshale ←
 ambapo utarejeshwa ukurasa wa awali hadi hatimaye kurejea kwenye ukurasa wenye mwonekano wa asili/kawaida wa blogu hii


NAOMBA KUTOA SHUKRANI NYINGI KWA KILA MMOJA WENU ANAYEKUMBUKA KUTEMBELEA BLOGU HII.NAWASHUKURU PIA WALE WOTE WANAONITUMIA MICHANGO KWA NJIA YA MAONI NA NINAWAKARIBISHA WASOMAJI WOTE KUTUMA MAONI.

WAKATI TUNAINGIA AWAMU YA PILI KUELEKEA WASOMAJI MILIONI MOJA,NINAPENDA KUWAHAKIKISHIA UBORA WA HALI YA JUU WA CONTENTS NA MWONEKANO WA BLOGU HII,SAMBAMBA NA MAREKEBISHO MBALIMBALI YENYE LENGO LA KUBORESHA BLOGU YENU HII.

ASANTENI SANA NA MUNGU AWABARIKI

1 comment:

  1. Hongera kwa kufikisha kilele hicho cha wasomaji na kazi yako nzuri unayoifanya ya kutuhabarisha

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.