4 Jul 2012


Hatimaye ninyi wasomaji makini wa blogu hii mmeitembelea mara MILIONI MOJA.Japo kuna blogu kadhaa za Kitanzania zilizopita idadi hiyo,binafsi najiskia faraja kubwa hasa kwa vile nimemudu kufikisha idadi hii ya watembeleaji pasipo msaada wa picha.Kimsingi,blogu za uchambuzi/habari pekee hazipati watembeleaji wengi kwani wengi wa Watanzania wanapendelea zaidi picha kuloko maneno.

Nawashukuru sana kwa kutumia muda wenu muhimu kufika hapa.Sina cha kuwalipa zaidi ya kuwaahidi kuwatumikia kwa uadilifu zaidi na kufanya marekebishi kila inapobidi.

MUNGU AWABARIKI SANA 

1 comment:

  1. Hongera mwanaharakati kwa kufikisha wasomaji milioni moja. Bila shaka huu ni mwanzo tu. Kila la heri !!!

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.