14 Feb 2013


Blogu hii inawatakia heri na baraka kwa siku hiimaalum kwa wapendano (Valentine's Day). Hapo juu nimedai Valentine wangu ni HUYU...Guess what? Si mtu bali ni social media. Siku kama leo, miaka mitano iliyopita (Februari 14, 2008) nilijiunga na mtandao wa kijamii wa TWITTER. Kwahiyo wakati wapendwa wasomaji wa blogu hii mnasherehekea Valentine's Day yenu, mie nina sherehe ya ziada: KUTIMIZA MIAKA MITANO KATIKA TWITTER.

Twitter imeniwezesha kufahamiana na watu wa kila aina, na hadi muda huu ninaposti makala hii nina followers 2,239.Natambua kuwa mie si mwepesi sana wa ku-follow back lakini ninaamini kila anayeni-follow atakubaliana nami kwamba hawaoni tofauti yoyote ya kuwa followed au kutokuwa followed nami kwani nipo interactive na kila mtu: SIBAGUI SICHAGUI. Na si kama ninajisifu lakini kwangu kila binti ninamu-address kama DADANGU na kwa wanaume wenzangu ninapenda kuwa-address kaka MKUU.

Kama nilivyobainisha hapo awali, Twitter imeniwezesha kufahamiana na watu wa kada mbalimbali, kutoka bankers wa kimataifa kama @chiume hadi wasanii kama @MwanaFA, kutoka Waheshimiwa kama @JMakamba hadi viongozi wa makampuni makubwa ya kimataifa kama @Makambas, na kutoka wanaharakati kama @YerickoNyerere na @MariaSTsehai hadi supamodo kama @FlavianaMatata na @Mariadkinawa , kutoka kwa wazalendo kama @dgtlUbun2 hadi wanasiasa kama @nape_nnauye na @shyrosebhanji, na kutoka kwa marafiki waliopo kama @kundaelyjr na @nanyaro_ na 'lost friends' kama @annieTanzania hadi wajasiriamali kama @AfricanGenesis na @IddaKabendera bila kumsahau 'rafiki mrembo' @bootyferrari360 na  mdogo wangu wa dhati @iMalaika....orodha ni ndefu,na kama sikukutaja haimaanishi kuwa huna umuhimu kwangu.

WAKATI NINAADHIMISHA MIAKA MITANO TANGU NIJIUNGE NA TWITTER NAOMBA KUWATAKIA VALENTINE'S DAY NJEMA KWENU NYOTE. TUENDELEE KUPENDANA

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.