Showing posts with label TWITTER. Show all posts
Showing posts with label TWITTER. Show all posts

19 May 2016


Kuna msemo wa Kiingereza unaoweza kutafsiriwa hivi, "thamani ya fedha ni matumizi." Pesa isiyoweza kutumika haina thamani, inabaki kuwa karatasi tu lenye picha ya kiongozi au alama fulani. Vivyo hivyo, thamani ya elimu/uelewa ni katika kushirikisha watu wengine. Ukiwa na elimu ya kutosha au uelewa mkubwa lakini ikabaki kichwani mwako tu bila kutumiaka basi haina umuhimu. Ni katika mantiki hiyo, sie wengine tumekuwa waumini wakubwa wa filosofia isiyo rasmi ya 'Sharing Is Caring' ambayo mara nyingi huandikwa #SharingIsCaring.

Leo ningependa ku-shea nawe msomaji mbinu muhimu ya ku-post kitu mtandaoni ili kioneknaje au kusomwa na watu wengi. Yaani hapa nazungumzia kuhusu ku-update status yako Facebook iwe ya maneno au picha, au ku-tweet huko Twitter, au ku-post picha yako hujo Instagram.

Tuanze na Facebook. Muda mwafaka wa ku-update status yako ili iweze kusomwa na watu wengi zaidi ni kati ya saa 3 asubuhi hadi saa 1 usiku, lakini muda bora kabisa ni saa 7 mchana hadi saa 9 alasiri.  

Kwa upande wa Twitter, muda mwafaka wa ku-tweet kitu kinachoweza kusomwa na watu wengi zaidi ni saa 6 mchana na kati ya saa 11 jioni na saa 12 jioni.

Kwa Instagram, muda mwafaka ni alfajiri, kwa maana watu wakiamka na kuingia kwenye app hiyo wakutane na picha yako.Lakini mtandao huu ni kimeo na jipu kwa Tanzania. Kwahiyo hata kuelezea kanuni zake ni sawa na kupoteza muda. Mtandao huu umetawaliwa na vitu vichafu na visivyopendeza. Binafsi japo bado ni memba huko lakini siutumii kwa sababu umesheheni kila aina ya maovu.

Maelezo hayo juu ni maalum kwa watu wenye ratiba zao nyingine lakini wanapenda kuwasiliana na jamii kwa kutumia mitandao ya kijamii. Maelezo hayo hayana maana kwa wenzetu ambao wapo mtandaoni kutwa kucha. Yes, kuna wenzetu wapo mtandaoni muda wote.

Kadhalika, maelekezo hayo ni ELEKEZI tu, kwa maana kwamba sio lazima usubiri muda huo mwafaka ndio uposti kitu chako. Muda huo elekezi ni mwafaka kwa minajili ya kuwafikia watu wengi zaidi.

Pichani chini ni infograph kuhusu nilichoeleza hapo juu



Endelea kutembelea blogu hii kwa mada mbalimbali za teknolojia, sambamba na makala zangu za kila wiki katika jarida la Raia Mwema, mada mbalimbali za intelijensia, burudani na michezo, maisha, na kadhalika. Karibuni sana

17 May 2016


"Hello world!" ndio ilikuwa tweet ya kwanza baada ya Idara ya ushushushu ya Uingereza inayohusika na kunasa mawasiliano, GCHQ (Government Communications Headquarters)  kujiunga na mtandao huo wa kijamii. 

Hawa jamaa, ambao makao yao makuu ni hayo pichani juu, ndio wenye jukumu la kusoma barua-pepe zetu, kusikia simu zetu na kutegesha vinasa sauti pale inapobidi, wamebobea kwenye hacking...kwa kifupi ukitaka kuwaelewa vema, m-Google yule jamaa anaitwa Edward Snowden..amewazungumzia vya kutosha, wao na washirika wao wa Marekani, wanaoitwa NSA.

Sasa hawa jamaa wameingia rasmi katika mtandao wa kijamii wa Twitter.



Hiyo tweet yao ya kwanza ya "Hello world" iliyoambatana na picha ya ndani ya ofisi yao, ina umuhimu wa aina yake kwa sababu ni programu ya kwanza kujifunza kuandika wakati mtu anapojifunza kundika kwa lugha ya ku - code katika  vile Java, Python, C, PHP, na Ruby.

"Kwa kujiunga na mitandao ya kijamii, GCHQ inaweza kutumia sauti yake yenyewe kuongea  kuhusu kazi muhimu tunayofanya kuiweka Uingereza salama," alisema Andrew Pike, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa taasisi hiyo ya kishushushu.

Taasisi hiyo ya kishushushu imeeleza kuwa inataka kufikika (accessible) na kuufahamisha umma kuhusu shughuli zake. Kadhalika, inataka majadiliano na watu wenye ufahamu wa teknolojia hususan katika maeneo ya teknolojia, hisabati, usalama mtandaoni na mada nyinginezo.




3 Sept 2014

Miongoni mwa vyanzo vya 'matatizo' katika matumizi ya mitandao ya kijamii ni uelewa mdogo wa wengi wanaoitumia mitandao hiyo. Ni vigumu kubainisha sababu moja inayochangia uelewa huo mdogo lakini yayumkinika kuhisi kwamba baadhi ya wenzetu hawapendi kujishughulisha kusaka maarifa/ uelewa.

Lakini pengine kikwazo kikubwa zaidi katika kupata uelewa, si tu kwa matumizi ya mitandao pekee bali kila kitu, ni 'kiburi' cha aidha kutotaka kuuliza pale mhusika haelewi au kufinya anaelewa ilhali haelewi, au kibaya zaidi, kuwavunja moyo wale wanaojitahidi kueneza uelewa wa masuala mbalimbali (mara nyingi huitwa 'wajuaji' kana kwamba kujua kitu na kuki-share ni kosa la jinai).

Tuliopitia JKT twafahamu 'kanuni ya kwanza unapowasili kambini,' yaani kufahamu mahali pa kujisaidia (kichekesho ni kwamba mara nyingi kambi za porini - na nyingi ya kambi za JKT enzi hizo zilikuwa maporini- hazina vyoo, na vikiwepo ni kwa matumizi ya maafande tu. Makuruta hupaswa kutengeneza vyoo katika muda wao binafsi).

Kadhalika, japo ni jambo linalopuuzwa na wengi, ni muhimu kwa kila mtumiaji wa mtandao wa kijamii, na kwa hakika mtandao wowote ule, kujibidiisha kufahamu japo kanuni na taratibu za msingi za mtandao husika, hususan haki na wajibu wake na wa mwenye mtandao. Uelewa huu si tu ni muhimu kwa kurahisisha 'maisha yetu mtandaoni' bali pia waweza kumsaidia mtumiaji kuepuka matatizo ya kisheria pindi akikiuka taratibu na kanuni hizo.

Kwa mtandaoni, kila mtandao, uwe wa kijamii au 'wa kawaida,' una kanuni na taratibu zake. Moja ya taratibu muhimu ni pamoja na haki za mtumiaji na wajibu wake. Miongoni mwa haki hizo ni pamoja na 'taarifa za mtumiaji' wa mtandao husika. Ndio maana ikitokea mtandao ukaweka hadharani anwani ya mtumiaji pasi ridhaa yake, unaweza kufunguliwa mashtaka kwa kukiuka haki za mtumiaji.

Kadhalika, mtandao ukiruhusu (makusudi au kwa bahati mbaya) mtu asiye na mamlaka kisheria kuweka taarifa 'nyeti' za mtu mtandaoni pasi ridhaa ya mhusika, unaweza kujiingiza katika matatizo makubwa ya kisheria

Sasa nimeona huko katika mtandao wa Twitter 'harakati' zinazofanyika kuhusu haja ya kufungwa kwa akaunti ya Twitter ya ndugu yetu, marehemu Betty Ndejembi, aliyefariki hivi karibuni.

Na pengine harakati hizo zinaisaidia jamii kuonyesha umuhimu wa HARAKATI japo kuna baadhi ya wenzetu wanaotafsiri uana-harakati kama kosa la jinai.Binafsi nadhani tatizo la watu wa aina hii ni kuzowea mno kufanyiwa mambo na serikali, taasisi au watu wengine (kwa mfano wanasiasa) kiasi kwamba wanapoona mtu binafsi anachukua msimamo katika suala flani wanamtafsiri ndivyo sivyo. Harkati chanya ni kitu kizuri kwa jamii kwani zaondoa haja ya utegemezi kwa taasisi kama serikali na kuwezesha 'nguvu ya umma.'

Harakati hizo za kutaka akaunti ya marehemu ifungwe zimehusisha ombi kwa mwanasiasa mmoja maarufu ashughulikie suala hilo. Binafsi sina tatizo na waliotoa ombi hilo bali laiti wangejihangaisha japo ku-Google 'how to request Twitter to close a deceased account' (jinsi ya kuiomba Twitter ifunge akaunti ya mtu aliyefariki) wasingehitaji kutuma ombil hilo kwa mwanasiasa huyo. Naomba ieleweke kuwa si dhambi kuomba msaada kwa mtu yeyote yule, let alone mwanasiasa. Lakini kuna masuala ambayo yapo ndani ya uwezo wetu ila tatizo ni uelewa mdogo au kutokuwa na uelewa.

Taratibu za kuiomba Twitter ifunge akaunti ya mtu aliyefariki ziko hivi (tafsiri ya Kiswahili ni yangu):

"Kuwasiliana na Twitter kuhusu mtumiaji aliyefariki...

Kinapotokea kifo cha mtumiaji wa Twitter, twaweza kushirikiana na mtu mwenye mamlaka ya kushughulikia mali (estates) za marehemu au mwanafamilia aliyethibitishwa wa marehemu kuwezesha kufunga akaunti ya marehemu.

Ili kutuwezesha kushughulikia kufunga akaunti (ya marehemu), tafadhali tupatie taarifa zifuatazo:

1. Jina (username) la marehemu katika akaunti yake ya Twitter, yaani katika ishu ya marehemu Betty itakuwa @BettyNdejembi au twitter.com/BettyNdejembi 
2. Nakala ya cheti cha kifo cha marehemu. 
3. Nakala ya kitambulisho kilichotolewa na serikali (kwa mfano leseni ya udereva au hata hati ya kusafiria)
4. Tamko (statement) lililosainiwa linalojumisha vitu vifuatavyo-Jina la kwanza na la mwisho la anayetuma ombil la kufungwa kwa akaunti ya marehemu-Barua pepe ya mwombaji-Mawasiliano (simu, anwani,nk)-Uhusiano wa mwamobaji na marehemu au mali za marehemu (estate)-Dhima ya ombi kwa Twitter (kwa mfano ; ninaomba Twitter ifunge akaunti ya marehemu')-Maelezo mafupi ya kuthibitisha kuwa akaunti husika ni ya marehemu, iwapo jina lililopo kwenye akaunti hiyo halifanani la lililopo kwenye hati ya kifo cha marehemu)-Kiungo (link) cha tanzia (obirtuary) au nakala ya tanzia kutoka gazetini (sio lazima-optional) 
5 Tafadhali tutumie nyaraka hizo kwa faksi au barua-pepe kwa anwani ifuatayo: 
Twitter, Incc/o Trust & Safety1355 Market St., Suite 900San Fransisco, CA 94103Fax: 1-415-865-5405 
Zingatia: Hii ni namba ya Marekani, kwahiyo hakikisha ina namba sahihi ya kipiga simu za kimataifa (international dialing code) iwapo unatuma kutoka nje ya Marekani. 
Tunafanya mawasiliano yetu yote kwa kutumia barua-pepe, iwapo tutahitaji taarifa nyingine, tutawasiliana nawe kwa anwani ya barua-pepe uliyotupatia. Iwapo una swali lolote, waweza kuwasiliana nasi kwa [email protected]

Sasa, kwa kuangalia tu utaratibu huu, hutoshindwa kutambua kuwa hili ni suala la kifamilia zaidi kuliko lenye kuhitaji mwanasiasa ashughulikie, unless mwanasiasa husika ni mwanafamilia ya marehemu.

Kuna kitu twaweza kujifunza hapa. Kwa wenzetu huku nchi za Magharibi, kufanya maandalizi ya 'nini kifanyike baada ya kifo changu' ni jambo la kawaida. Licha ya huduma kama bima ya kifo, kuna taasisi mbalimbali zinazojishughulisha na huduma za maandalizi baada ya kifo kama vile kushughulikia maiti yako utapofariki ikiwa ni pamoja na mahali utapozikwa, usimamizi wa mirathi, nk.

Lakini pia kuna huduma mbalimbali za bure mtandaoni kuhusu hatma yetu mtandaoni baada ya vifo vyetu. Kimsingi, mada ya 'kifo na mtandao' (Death and the Internet) ina maingizo 242,000,000 katika tovuti ya kutafutia taarifa (search engine) ya Google

Ninatambua kuwa kwa mujibu wa mila na desturi mbalimbali za Kiafrika, kuchukua hatua hizi za maandalizi ya baada ya kifo kwaweza kutafsiriwa kama 'uchuro,' licha ya ukweli kwamba siku moja kila mmoja wetu atakuwa marehemu kwani kifo haikiepukiki.

Nimalizie kwa kutanabaisha kuwa lengo la makala hii sio kudhihaki harakati za wanaotaka akaunti ya marehemu Betty ifungwe (hasa nikiwa natambua uwepo wa 'uhuni usiopendeza hata chembe' wa baadhi ya watu wanaojifanya ku-tweet kana kwamba ni marehemu mwenyewe ana-tweet "kudai atendewe haki" japo tweet husika haikutoka katika akaunti ya marehemu) bali ni kuelimisha kuhusu utaratibu wa kuomba akaunti ya Twitter ya mtu aliyefariki ifungwe, suala ambalo kwa wenye uelewa  ni la kifamilia zaidi kuliko kuhitaji 'msaada' kutoka kwa wanasiasa. 

Ushauri wangu kwa wanaotaka kuona akaunti hiyo ikifungwa ni kuwasiliana na familia ya marehemu na kuwafahamisha utaratibu husika (iwapo hawafahamu). Ikumbukwe kuwa akaunti ya marehemu, iwe Twitter au katika mtandao wowote ule, ni mali ya marehemu, kama ilivyo akaunti yake ya benki, hati yake ya kusafiria, hati ya kiwanja, au mali yake yoyote ile. Ili, kwa mfano kuweza kufunga akaunti yake benki, ni lazima ipatikane ridhaa ya wenye mamlaka na marehemu, kwa mfano maelekezo katika wosia wake au maamuzi ya famili yake. Kadhalika, ili akaunti yake ya Twitter iweze kufungwa, ni lazima kupata ridhaa ya marehemu kupitia wosia wake au uamuzi wa wanafamilia yake.

Mungu amlaze marehemu Betty mahala pema peponi, Amen.


14 Feb 2013


Blogu hii inawatakia heri na baraka kwa siku hiimaalum kwa wapendano (Valentine's Day). Hapo juu nimedai Valentine wangu ni HUYU...Guess what? Si mtu bali ni social media. Siku kama leo, miaka mitano iliyopita (Februari 14, 2008) nilijiunga na mtandao wa kijamii wa TWITTER. Kwahiyo wakati wapendwa wasomaji wa blogu hii mnasherehekea Valentine's Day yenu, mie nina sherehe ya ziada: KUTIMIZA MIAKA MITANO KATIKA TWITTER.

Twitter imeniwezesha kufahamiana na watu wa kila aina, na hadi muda huu ninaposti makala hii nina followers 2,239.Natambua kuwa mie si mwepesi sana wa ku-follow back lakini ninaamini kila anayeni-follow atakubaliana nami kwamba hawaoni tofauti yoyote ya kuwa followed au kutokuwa followed nami kwani nipo interactive na kila mtu: SIBAGUI SICHAGUI. Na si kama ninajisifu lakini kwangu kila binti ninamu-address kama DADANGU na kwa wanaume wenzangu ninapenda kuwa-address kaka MKUU.

Kama nilivyobainisha hapo awali, Twitter imeniwezesha kufahamiana na watu wa kada mbalimbali, kutoka bankers wa kimataifa kama @chiume hadi wasanii kama @MwanaFA, kutoka Waheshimiwa kama @JMakamba hadi viongozi wa makampuni makubwa ya kimataifa kama @Makambas, na kutoka wanaharakati kama @YerickoNyerere na @MariaSTsehai hadi supamodo kama @FlavianaMatata na @Mariadkinawa , kutoka kwa wazalendo kama @dgtlUbun2 hadi wanasiasa kama @nape_nnauye na @shyrosebhanji, na kutoka kwa marafiki waliopo kama @kundaelyjr na @nanyaro_ na 'lost friends' kama @annieTanzania hadi wajasiriamali kama @AfricanGenesis na @IddaKabendera bila kumsahau 'rafiki mrembo' @bootyferrari360 na  mdogo wangu wa dhati @iMalaika....orodha ni ndefu,na kama sikukutaja haimaanishi kuwa huna umuhimu kwangu.

WAKATI NINAADHIMISHA MIAKA MITANO TANGU NIJIUNGE NA TWITTER NAOMBA KUWATAKIA VALENTINE'S DAY NJEMA KWENU NYOTE. TUENDELEE KUPENDANA

25 Feb 2012

4 Feb 2012


Are you sitting on just a handful of followers? Have you never had a re-tweet? Do people tweet at you with the hashtag #pleasestoptweetingyoumakemewanttostabmyeyes out?
Well you need the sweet tweet tips from US researchers, who have scanned 1500 Twitter users to deliver their top nine ideas for effective tweeting.
Their research, reported by The Telegraph, says that the majority of Tweets go unread or irritate people.
The research, by University of Southampton, Massachusetts Institute of Technology (MIT) and Georgia Institute of Technology asked Twitter users to anonymously rate their friends' tweets.
Michael Bernstein, PhD student at MIT, said in a statement: "Analysing the negatively rated tweets, and the consensus that forms around them, will help us understand the emerging approved or accepted norms in these new forms of online communication."
In layperson's speak, that means, see what others do badly, and avoid it.
Some of these tips are plain common social media sense, but someone people just need telling in a sciencey way to get the point across.
The researchers' top nine tips for Twitter are:
1.Old news is no news. Twitter is fast moving so information gets stale quickly so don't repeat links that have already been repeated several times.
2.Contribute to a story rather than just comment on it. Which means add your own opinion or a new fact or don't bother.
3.Keep it short. Even 140 characters can be too long for some people's rambling comments.
4. Limit the syntax. Do not overuse hashtags, @mentions and abbreviations.
5.Don't tell everyone where you are all the time. Twitter users particular hate Foursquare check-ins
6.Don't just link to a blog or a photo without giving readers a reason why they should click on it.
7.Don't whine. Negative sentiments and complaints were disliked.
8.Be a tease. If you want someone to go onto your website, don't give away the whole story in a tweet but use it as a way of hooking the reader.
9.Celebrities - the tiniest detail of your daily routine is not any more interesting because you are famous. People want your professional insights, not to know what you like in a sandwich.

25 Oct 2011

30 Jul 2011


Mitandao ya jamii ya Facebook na Twitter imetengeneza kizazi kinachoendekeza umimi kupita kiasi kiasi kwamba watu hawajali masuala mengine huku wakiwa na tamaa kama watoto wadogo kuona watu wanasema mazuri kuhusu wao,picha zao,wanayoandika kwenye mitandao hiyo,nk.

Kuendelea kuwepo kwenye mitandao hiyo kwa muda mrefu kunamwacha mtumiaji akiwa na mgogoro wa kujitambua (identity crisis),tamaa ya kutambulika katika namna ileile mtoto mdogo anamwambia mzazi wake, "Mama,nimefanya hivi."

Baroness Greenfield,profesa wa taaluma ya madawa (pharmacology) katika Chuo Kikuu cha Oxford,anaamini kuwa kukua kwa urafiki wa mtandaoni-sambamba na matumizi makubwa ya michezo ya kompyuta-vinaweza kupelekea kuuchanganya ubongo.

Hii inaweza kusababisha upungufu kwenye kukazani mambo ya muhimu,hitaji la kutamani kusifiwa na uwezo mdogo wa mawasiliano yasiyohitaji kutumia maneno (non-verbal communication) kwa mfano kumwangalia mtu usoni wakati wa maongezi.

Zaidi ya watu milini 750 duniani wanatumia mtandao wa Facebook kuonyeshana picha na video na mara kwa mara hubandika maelezo kuhusu mienendo na mawazo yao.

Mamilioni pia wamejiunga na mtandao wa Twitter ambao huwawezesha watumiaji kusambaza ujumbe mfupi na picha kuhusu wao wenyewe.

Baroness Greenfield,mkurugenzi wa zamani wa taasisi ya utafiti ya Royal Institution alisema, "kinachonipa wasiwasi ni ile hali ambapo unaweza kutarajia mtu atawaza au kusema nini ambayo ni hali ya kawaida huko Twitter."

"Kwanini mtu ahitaji kujua umekula nini wakati wa kifungua kinywa?Inanikumbusha jinsi mtoto mdogo anavyosema, 'mama angalia ninachofanya' "

"Ni kama mgogoro wa kujitambua.Kimsingi,hali hii inaufunga ubongo kwenye kuhusisha wakati/muda"

Mwanataaluma huyo alidai kuwa baadhi ya watumiaji wa Facebook wanajisikia wanapaswa kuwa "watu maarufu wadogo wadogo" (mini celebrities) ambao wanaangaliwa na kunyenyekewa na watu wengine kila siku.

"Wanafanya vitu vinavyoendana na Facebook kwani njia pekee wanayoweza kutumia kujitambulisha kwa umma ni kwa kuwafahamisha watu wengine kuhusu kinachoendelea kwenye maisha yao."

"Ni kana kwamba watu wanaishi katika dunia isiyo halisi bali dunia ambayo kinachomata ni nini watu wanafikiria kuhusu wewe au kama wanaweza kubonyeza kwenye picha au ulichoandika," alisema Profesa huyo.

"Fikiria kuhusu madhara kwa jamii ikiwa watu wanajali zaidi kuhusu nini watu wengine wanafikiria kuhusu wao kuliko nini wanachofokiria kuhusu wao wenyewe."

Mawazo ya mwanazuoni huyo yaliungwa mkono na Sue Palmer,mtaalam wa fasihi andishi na mtunzi wa vitabu,ambaye alisema kuwa wasichana hususan wanaamini wao ni bidhaa ambayo lazima iuzwe kwenye Facebook.

Alisema: 'Watu walizowea kuwa na picha ya kuchora (zinazowaonyesha wao) lakini sasa tunaweza kujichora wenyewe mtandaoni.Ni kama kuwa mshiriki kwenye shoo yako mwenyewe ya TV ambayo umeiunda na kuiweka hadharani kwa dunia kuiona.'

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka gazeti la Daily Mail


28 Jun 2011

Pichani ni jengo la "Tanesco ya Senegal",Senelec,lililoshambuliwa na waandamanaji wenye hasira kuhusu kukatika umeme mara kwa mara jijini Dakar.Akina sie tunashambulia kwa matusi,lawama,na manung'uniko huko Twitter na Facebook!!!

Sio siri kwamba upole wa Watanzania ni miongoni mwa sababu kuu za mabaya mengi yanayotokea huko nyumbani.Na kama kuna suala linalosikitisha kuhusu mwamko wa Watanzania kudai haki zao ni tatizo la mgao wa umeme sambamba na ubabaishaji wa hali ya juu wa serikali na Tanesco katika kushughulikia tatizo hilo.

Sasa hivi,mitandao ya jamii ya Twitter na Facebook imetawaliwa na malalamiko ya Watanzania wengi kuhusu mgao.Wengine wanaishiwa na uvumilivu na kuishia kuitukana Tanesco,kana kwamba matusi hayo yatarejesha umeme.Wengine wamekuwa wakipeana taarifa kuhusu maeneo ambayo "Tanesco wameshachukua umeme wao".Kwa kifupi,kinachosikika zaidi ni manung'uniko,lawama,vilio na hata matusi.Cha kusikitisha ni kwamba hakuna dalili yoyote kutafsiri malalamiko hayo into vitendo.

Sio kama nawasimanga ndugu zangu.I really feel you lakini ukweli mchungu ni kwamba kelele zenu haziwezi kumaliza tatizo hilo.Kinachohitajika ni kudai haki kwa nguvu.By "nguvu" simaanishi vurugu bali kuchukua hatua za makusudi kuhakikisha serikali na Tanesco wanawajibika.Mgao utaendelea milele iwapo Watanzania wataishia kulalamika tu.Hakuna miujiza katika kuleta mabadiliko.Either watu wajitoe muhanga kudai haki yao kama walipakodi au waendelee kuteswa na mgao.

Bahati nzuri,wenzetu nchini Senegal wanatuonyesha namna gani matatizo yanayoathiri nchi yanavyoshughulikiwa na umma.Nisieleze kwa maneno yangu bali naomba usome habari ifuatayo:

Associated Press

DAKAR,Senegal: Maelfu ya waandamanaji wameingia mitaani katika mji mkuu wa Senegal kupinga kukatika umeme mara kwa mara.Maandamano hayo ni tukio la tatu la vurugu nchini humo ndani ya wiki.

Wananchi wenye hasira walivamia ofisi za shirika la umeme la Senelec,jijini Dakar baada ya maandamano ya kupinga kukatika kwa umeme kwa muda mrefu.

Watu kadhaa walishambulia majengo ya serikali hapo jana.Wanadaia kuwa baadhi ya maeneo yamekuwa yakikosa umeme kwa masaa 24 au zaidi.

Kama ilivyo kawaida kwa vyombo vya dola barani Afrika,askari wa kikosi cha kutuliza ghasia walipambana na waandamanaji kwa kutumia maji na mabomu ya machozi.Msemaji wa polisi hakuweza kuthibitisha idadi ya waliojeruhiwa katika ghasia hizo.

Alhamisi iliyopita,vurugu kubwa ziliibuka kupinga mpango wa mabadiliko ya katiba ya nchi hiyo

Uchaguzi ni wenu Watanzania wenzangu.Mwendelee kulalama huku Serikali na Tanesco wakiendelea kuwasanifu (mgao wa umeme hauwagusi kwa vile aidha wana jenereta zinazojazwa mafuta na hela yako mlipakodi au maeneo wanayoishi hayakatwi umeme kutokana na unyeti wake) AU muige mfano wa wenzetu wa Senegal.Hakuna njia ya mkato katika kutatua matatizo sugu yanayosababishwa na watendaji wasiotimiza wajibu wao.It's now or never!

13 Sept 2010

Je wajua kuwa licha ya mgombea wa CCM Jakaya Kikwete kukacha mdahalo na wagombea wa vyama vingine anapatikana kirahisi mtandaoni ambapo "anauza" sera zake na "mafanikio" yake?Kama ulikuwa hufahamu basi nenda Twitter kisha tafuta @Kikwete2010 au nenda Facebook kisha tafuta Jakaya Kikwete.

I know siasa za chama kimoja zimeacha kasumba ya kufurahia kugusana mabega na watawala.No wonder kuna wenzetu muda huu wanakenua meno yote thelathini na kitu kwa vile wamepokea ujumbe kama huu "Kikwete2010 is following you..." au "Salma Kikwete is Following you..." 

Si ajabu kuna wenzetu wamefotokopi meseji za aina hiyo wakiamini kuwa Kikwete na mkewe Salma wanawajali saaaana hadi wameamua kuwa-follow up huko Twitter au kuungana nao hapo Facebook.KALAGABAHO!Kwanini hujiulizi WHY NOW?Kikwete na mkewe walikuwa Ikulu tangu Desemba 2005 na HAWAKUKUTAFUTA.Hushangai kwanini leo wanataka urafiki nawe?Well,sio kosa kuwa rafiki na rais au mkewe lakini urafiki huu hauna tofauti na ule wa mtenda tendo la ndoa na kondomu.Zana hiyo (kondom) huwa na umuhimu wa kipekee (kwa wale wanaojali) kabla na wakati wa tendo la ndoa,lakini pindi shughuli ikimalizika kondom huwa ni uchafu usiovumilika.ANGALIA,usijetumika kama kondomu: Kikwete akuone muhimu sasa kwa vile anahitaji kura lakini akakusahau (kama alivyokusahau 2005-till now) baada ya kurejea Ikulu.

Badala ya ku-retweet kila anachoandika,tumia haki yako kama Mtanzania kuhoji masuala mbalimbali yanayolikabili taifa.Twende mbali zaidi ya kupongeza na kuona sifa "kugusana mabega" na watawala.Sio kosa kushabikia lakini ushabiki wenye maana ni ule unaombatana na matumizi sahihi ya akili.

Now you-in case you didn't.Muulize Kikwete,je ile kauli aliyotoa mwaka 2006 kuwa anawafahamu wala rushwa kwa majina ila anawapa muda wa kujirekebisha imefikia wapi?Je wameshajirekebisha?Je anaweza kututajia majina ya waliojirekebisha na waliogoma kufuata ombi hilo la kichovu?

Muulize pia kwamba kabla ya sakata la Richmond aliahidi kuwa tatizo la umeme lingebaki kuwa historia.A few months later,matapeli wa Richmond wakaingia kwenye picha.Today,tatizo la umeme ni as sugu as ufisadi.Mkalie kooni na kumhoji,kama huko nyuma alitoa ahadi ya kutupatia ufumbuzi wa umeme na hakutimiza,kwanini tumwamini sasa?

Muulizie pia kama bado anaamini kuwa mimba za wanafunzi wa kike zinasababishwa na kimbelembele chao.Yah,muulize swali hilo kwa vile hadi sasa bado hajakanusha au kuwaomba msamaha Watanzania kwa kauli hiyo ya kizembe.

Usikose kumuuliza pia kama hadi sasa hajui sababu zinazoifanya Tanzania kuwa masikini maana alinukuliwa akijiuliza swali hilo.Nenda mbali kidogo na kumhoji kama alikuwa hajua kwanini Tanzania ni masikini sasa anafanya nini hapo Ikulu?

Sasa hivi amenzisha hash tag #Mafanikio huko Twitter.Hapo utapata nafasi nzuri ya kujionea waziwazi namna Awamu ya Nne ya Kikwete ilivyoshindwa kuikomboa Tanzania kutoka kwenye umasikini licha ya raslimali lukuki tulizonazo.Hapo Kikwete na wapambe wake wanataja mapato yaliyotokana na utalii na madini.Mkalie kooni na kumhoji kama mapato ndio hayo,kwanini sie bado masikini?Fedha hizo zimeenda wapi kama sio kwenye akaunti za mafisadi?Na kwenye utalii muulize pia kuhusu meno ya tembo yaliyokamatwa huko Hong Kong yakitokea Tanzania.

Kumbuka,usikubali kutumika kwa maslahi ya mtu mwingine.Kumhoji mwanasiasa anayeomba kukuongoza ni haki yako.Usiichezee.Badala ya kujipendekeza kwa RT (Retweets za Kikwete2010) tumia fursa hiyo kumuuliza maswali ya msingi yanayohitaji majibu ya haraka.

PAMOJA TUNAWEZA

13 Jul 2010

Kuna tofauti moja ya msingi katika Twitter na Facebook (social media nazizipendelea zaidi),nayo ni namna watu wawili wanavyounganishwa na huduma hizo.Wakati nikiomba kuunganishwa na mtumiaji wa Facebook,na kukubaliwa inamaanisha nitaweza kuona profile yake na updates mbalimbali,kwenye Twitter habari ni tofauti.Nikiamua "kumfuata" (following) mtu,haimaanishi kuwa mtu huyo automatically naye "atanifuata".

Lakini katika mazingira ya kawaida,na pengine kistaarabu,kama mtu ameamua "kukufuata" huko Twitter,unapungukiwa nini ukirejesha "fadhila" kwa kumfuata mtu huyo?Au ndio usupastaa kwamba wanaokufuata ni wengi kuliko unaowafuata?Ofkoz,inaweza kuwa vigumu "kumfuata" kila "anayekufuata" ukiwa na "wafuasi" maelfu kadhaa lakini si vigumu kama wafuasi wako ni mia na kitu tu.

Naandika haya nikitambua kuwa uamuzi wa mtu kukufuata ni suala la mtu binafsi.Na kwa vile mtu ahajalazimishwa kumfuata mtu mwingine inaweza kupelekea hoja yangu kuonekana haina umuhimu.Nachojaribu kupigia mstari hapa ni ustaarab wetu wa Kiafrika.Katika mazingira ya kawaida,kama jana nilikutana nawe nikakusalimu,leo pia tumekutana nikakusalimu na kesho inakuwa hivyohivyo,basi kistaarabu inatarajiwa kuwa kesho kutwa nawe utaanzisha salamu.Kinyume cha hivyo,tafsiri itakuwa aidha unaringa au huhitaji salamu yangu.Ni katika mantiki hiyohiyo,kama mtu ameamua kukufuata (hata kama wewe ni maarufu mara elfu kuliko huyo mfuasi) basi ni tarajio la mfuasi huyo kuwa nawe utamfuata.Si lazima lakini ni katika masuala ya ustaarab tu.

Kama unaafikiana nami,basi pengine fanya jambo la kupendezesha roho za wale wanaokufuata lakini wewe hujaamua kuwafuata:WAFUATE PIA.Haigharimu chochote,haikupunguzii umaarufu ulionao,na zaidi,itakufanya uonekane huna dharau.

Ni ushauri wa bure tu.

3 May 2010

Waziri Mkuu wa Australia,Kevin Rudd,amekuwa akifuatilia tovuti za ngono (porn sites),kwa mujibu wa kituo cha runinga cha Sky. 


Rudd,hata hivyo,amekuwa 'mfuatiliaji' wa tovuti hizo kutokana na mapungufu katika nyenzo za usalama/udhibiti (setting) katika akaunti yake ya Twitter.Kutokana na mapungufu hayo,kiongozi huyo amekuwa akifuatilia watu kama bloga wa mambo ya ngono,duka linalouza bidhaa za ngono,mwanamama aliye kifua wazi huku amjifunga pingu,na kadhalika.

Msemaji wa Waziri Mkuu ameeleza kuwa tatizo hilo lilitokana na akaunti ya Twitter ya Rudd kufuata wale wote wanaomfuata (auto-follow those who follow him)."Japo Waziri Mkuu anajitahidi kutoa majibu kwa wale wanaosema chochote kwake,kazi hiyo ni ngumu ukizingatia idadi ya watu ni 900,000", alieleza msemaji huyo.

Japo inamhitaji mtumiaji wa Twitter kuangalia kwanza wasifu wa mtu anayeomba kukufuata,kuna kipengele kinachoiwezesha akaunti imkubali moja kwa moja mtu anayeomba kumfuata pasipo haja ya mwenye akaunti kufanya hivyo.Uwezo huo unaonekana kuwa muhimu kwa watumiaji wa Twitter wenye wafuasi (followers) wengi.Katika akaunti yake KevinRuddPM,Waziri Mkuu huyo ni mfuasi wa wana-twitter wengine 200,000.

Wataalam wa teknolojia wanatahadharisha kuwa nyenzo za habari kwa jamii (social media)zinaweza kuhatarisha usalama wa mtuamiaji kama hataokuwa makini."Kuna imani kwamba kwenye vitu kama Twitter unaweza tu kufungua akaunti na mambo yakaenda mwanana",anasema Handsley,makamu mwenyekiti wa kampuni ya Young Media Australia."Tunapaswa kufahamu kwa undani kuhusu usalama wa chanzo husika cha habari kwa jamii kabla ya kuamua kukitumia",aliongeza alipoongea na gazeti la Herald Sun.

Kwa mujibu wa gazeti hilo,baadhi ya wengine 'waliofuatiliwa' na Waziri Mkuu Rudd ni pamoja na tovuti ya kamera-mtandao (webcams) za ngono na mmiliki wa kiota cha watenda ngono wa jinsia moja (gay resort) cha Phuket,Thailand.

Rudd amekuwa mtumiaji mzuri wa teknolojia ya habari huku nyakati nyingine akitumia nyenzo kama Twitter kubainisha sera zake.

Imetafsiriwa kutoka Sky News

5 Jan 2009

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.