5 Apr 2014


Kimsingi, mchakato wa kupata Katiba mpya umegeuka kuwa hukumu ya Muungano wa 'Tanganyika' (Tanzania Bara) na Zanzibar. Mengi yamesahongelewas na nisingependa kuyarudia hapa, lakini suala jipya lililojitokeza ni sahihi za Marehemu Baba wa Taifa na Marehemu Karume.

Kuna taarifa kwamba baadhi ya nyaraka hazina sahihi ya Marehemu Karume, hali inayoweza kuashiria kuwa uamuzi wa Muungano ulifanywa na Nyerere pekee. Japo historia inaeleza tofauti, kwa kawaida, hati ya mkataba huwa na angalau na sahihi za wahusika wawili au zaidi kutegemea mazingira ya mkataba husika.

Lakini hata hiyo sahihi ya Nyerere yenyewe imezua utata. So far, kuna sahihi mbili (yawezekana zipo nyingine). Lakini sio tu sahihi kuwa zaidi ya moja, katika moja ya nyaraka za Muungano kuna maneno yameongezwa. Maelezo yanayotolewa ni kuwa kompyuta ilitumika...bila hata kuuliza kompyuta ilitumika kwa malengo gani, swali la msingi ni je Tanzania- au Tanganyika ilikuwa na kompyuta mwaka 1964?

Licha ya sahihi ya Nyerere, kuna taarifa pia ikwamba hata sahihi ya Katibu wa Bunge wa wakati huo, Pius Msekwa nayo ina walakini. 

Mara kadhaa katika maandiko yangu nimebainisha kuwa haileti maana kujadili muundo wa Muungano pasipo wajjumbe wa Bunge la Katiba kupatiwa nyaraka muhimu zinazohusu Muungano huo. Maelezo yaliyotolewa na wahusika ni kwamba eti kuna nakala moja tu ya moja ya nyaraka muhimu za Muungano, kwahiyo haiwezi kupelekwa Dodoma kwa kuhofia inaweza kupotea. Huu sio utoto tu bali ni ubabaishaji wa hali ya juu. Kwanini wahusika wasichapishe nakala kisha kuzi-certify as true copies of the original?

Anyway, hebu analia katika picha ya hapo juu kuhusu ipi ni sahihi halisi ya Mwalimu Nyerere.

Nihitimishe bandiko hili kwa kuyumkinisha kuwa utata unaojitokeza kuhusu nayaraka muhimu za Muungano unaashiria kwamba kuna mtu flani mahala flani anaongopa (someone somewhere is lying). Tusichojua ni kwanini?

TIME WILL TELL 

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.