10 Sept 2014

Royal sources made clear that there had been no suggestion from anyone in Government or opposition for the Queen to take a public stand
Malkia Elizabeti wa Pili, mtawala wa 'Muungano wa Uingereza' (United Kingodm) ametanabaisha kuwa kamwe hatoingilia hatma ya kura itayoamua iwapo Uskochi iendelee kuwa sehemu ya 'Muungano wa Uingereza' ua iwe taifa huru.

Hatua hiyo ya nadra imetokana na maoni ya baadhi ya wabunge hapa Uingereza kwamba Malkia aingilie katik katika suala hilo.

Waziri Mkuu (First Minister) wa Uskochi anaweza kuingia matatizoni baada ya kauli yake jana kwamba alikutana na Malkia na akaambiwa kuwa mwanamama huyo yupo tayari kuwa Malkia wa Uskochi iliyo huru.

Lakini makazi ya Malkia ya Buckingham Palace yameweka bayana msimamo kwamba Malkia hajihusishi na siasa na walio katika nyadhifa za kisiasa wanapaswa kuhakikisha hali hiyo inabaki hivyo.

Vynazo vimethibitisha kuwa Malkia siku ya kupiga kura- tarehe 18 mwezi huu- Malkia Elizabeth atakuwa katika makazi yake ya faragha kwenye ukanda wa Nyanda za Juu wa Uskochi (Scottish Highlands)

Japo makazi ya Malkia yamesisitiza kuwa mtawala huyo haingilii masuala ya kisasa lakini wachambuzi wanaeleza kuwa huhitaji kuwa mtaalam wa siasa kumaizi kuwa Malkia anatamani 'Muungano wa Uingereza' uendelee, na kutumia swali la kuamsha tafakuri la 'Hivi Baba Mtakatifu (Papa) ni Mkatoliki? (kwa maana ya kuwa ili mtu awe Papa shurti awe Mkatoliki)

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa isivyo rasmi kutoka tovuti ya gazeti la Daily Mail la hapa Uingereza

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.