9 Dec 2014

Wakati Tanzania Bara inatimiza miaka 53 ya uhuru, leo pia ni siku yangu ya kuzaliwa. Naitakia nchi yangu kila la heri na fanaka, na Mweneyzi Mungu aiongoze nchi yetu kwenye njia njema, sambamba na kuiepusha na mabalaa. Kwa mujibu wa mambo yalivyo huko nyumbani, hali si ya kuridhisha sana. Basi ni muhimu tuitumie siku hii muhimu kuiombea nchi yetu kwa kila jema.

Kwangu, siku hii ya kuzaliwa ni fursa nyingine ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia kuongeza mwaka mwingine katika maisha yangu. Nawashukuru sana wazazi wangu Baba Mzee Philemon Chahali na mama yangu mpendwa, marehemu Adelina Mapango (we all miss you so much mom). Pia nawashukuru wanafamilia wenzangu, ndugu, jamaa na marafiki kwa mema yote waliyonifanyia. Natumaini mtaendeleo kuwa nami siku zote za uhai wangu.

Nwashukuru nanyi wasomaji wa blogu hii, marafiki zangu wapendwa ambao nawafahamu kwa kuangalia idadi ya wanaotembelea blogu hii. Japo pengine wengi wenu hatufahamiani personally, lakini mnapochukua muda wetu muhimu kunitembelea hapa, kuvumilia makelele yangu na 'upuuzi' wmingine ninaoandika, ni faraja kubwa mno kwangu. Nawashukuru kwa kuwa sehemu ya familia yangu kiuandishi.

Nimalizie kwa kumwomba Mwenyezi Mungu azidi kunijalia afya njema, maisha marefu, afya njema kwangu, familia, yangu, ndugu, jamaa na marafiki, na niwe na mafanikio katika kila jambo. Amen

1 comment:

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.