18 Jul 2015

MOGADISHU: Kiongozi wa kikundi cha kigaidi cha Al-Shabaab jana Ijumaa alitoa ujumbe wa sikukuu ya Idd Elf Fitr ambapo alitoa wito wa  kupata  magaidi wapya ili 'kuondoa maumivu ya Waislamu' katika eneo la Afrika Mashariki.

Katika taarifa ambayo inaonyesha dhamira ya magaidi hao kusambaza ubaradhuli wao, kiongozi huyo, Ahmed Diriye, ambaye pia hujulikana kama Ahmed Umar Abu Ubaidah, alizionyooshea kideole Kenya, Ethiopia, Djibouti na Uganda.

"Majambia ya Mujahidina yameshatolewa kibindoni na mashambulizi dhidi ya maadui yanaendelea...na tunawataka wapiganaji wetu kuongeza mashambulizi dhidi ya makafiri," alisema katika taarifa iliyowekwa kwenye tovuti ya Waislam wenye msimamo mkali.

"Tunasema kwa jamaa zetu wapendwa wanaoishi kwenye maeneo yaliyo chini ya ukoloni wa Kenya kwamba sisi jamaa zenu hatotuacha kuja kuwasaidia."

"Mnapaswa kufahamu kuwa jihadi ndio njia pekee ya kujikomboa wenyewe kutoka katika unyanyasaji na udhalilishaji mnaokabiliana nao, kwahiyo mharakishe kujiunga na jihadi...na kuyakomboa maeneo yenu kutoka kwa Wakristo."

Diriye alipongeza shambuli la kigaidi katika chuo kikuu cha Garissa, Kaskazini Mashariki mwa Kenya, ambao magaidi wanne wa kikundi hicho waliwaua watu 148, wengi wao wakiwa wanafunzi. Wengi wa magaidi hao walikuwa Waislam kutoka nchini humo.
"Tunawapongeza ninyi na na Waislamu wengini duniani kwa operesheni ya kijasiri katika chuo kikuu cha Garissa," alisema kiongozi huyo wa magaidi, akieleza kuwa shambulio hilo lilikuwa la kulipiza kisasi kwa 'mauaji yaliyoidhinishwa na serikali ya Kenya dhidi ya mashehe na utekaji vijana wa Kiislam' kwenye maeneo ya pwani ya nchi hiyo.ambaye wakazi wake wengi ni Waislam.

"Muda wa Wakristo kufanya unyama bila kuwajibishwa umefikia kikomo," alisema. " Tunaswali kwako Mola kuodnoa maumivu ya Waislam katika Afrika Mashariki nzima - Ethiopia, Uganda na Djibouti."

"Hatotoacha jitihada za kuwasaidia, na milango ya mafunzo katika makambi yetu ipo wazi kuwapokea na makazi yetu yapo wazi kuwakaribisha."

Al-Shabaab, jina lenye maana 'vijana' kwa Kiarabu, waliibuka wakati wa mapambano makali dhidi ya majeshi ya Ethiopia, ambayo yaliingia nchini Somalia mwaka 2006 katika uvamizi ulioongozwa na Marekani kuung'oa utawala wa Muunganowa Korti za Kiislam ambao wakati huo ulikuwa ukitawala mji mkuu wa Mogadishu.

Magaidi wa Al-Shabaab wameendelea kufanya mashambulizi ya mara kwa mara, yenye malengo ya kupina madai kuwa kikundi hicho kinakaribia kushindwa kwenye operesheni inayoendeshwa na majeshi ya Somalia na yale ya Umoja wa Afrika, mashambulizi ya ndege ndogo zinazojiendesha zenyewe (drones) yanayofanywa na Marekani dhidi ya viongozi wa kikundi hicho, sambamba na wapiganani wanaotoroka kutoka katika kundi hilo la kigaidi.
Wakati hivi sasa kundi hilo la kigaidi linaungwa mkono na kundi jingine la kigaidi la kimataifa, Al-Qaeda, hisia zimekuwa zikiongezeka kwamba kundi hilo la Somalia linaweza kuhamisha utiifu wake kutoka kwa Al-Qaeda na kuelekea kwa kundi jingine hatari kabisa la kigaidi kimataifa la Dola ya Kiislam (Islamic States) au ISIS (kama linavyofahamika kwa kifupi).

Wakati flani, Al-Shabaab ilikuwa sumaku ya kuvuatia wapigania vijana wapiganaji kutoka mataifa mbalimbali, lakini mkakati wao kuwavutia wapiganaji wa kigeni umeathiriwa na kushamiri kwa ISIS huko Syria na Iraq, sambamba na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe ndani ya Al-Shabaab.

CHANZO: Imetafsiriwa kutoka tovuti ya eNCA



0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.