Showing posts with label Al-Shabaab. Show all posts
Showing posts with label Al-Shabaab. Show all posts

18 Jul 2015

MOGADISHU: Kiongozi wa kikundi cha kigaidi cha Al-Shabaab jana Ijumaa alitoa ujumbe wa sikukuu ya Idd Elf Fitr ambapo alitoa wito wa  kupata  magaidi wapya ili 'kuondoa maumivu ya Waislamu' katika eneo la Afrika Mashariki.

Katika taarifa ambayo inaonyesha dhamira ya magaidi hao kusambaza ubaradhuli wao, kiongozi huyo, Ahmed Diriye, ambaye pia hujulikana kama Ahmed Umar Abu Ubaidah, alizionyooshea kideole Kenya, Ethiopia, Djibouti na Uganda.

"Majambia ya Mujahidina yameshatolewa kibindoni na mashambulizi dhidi ya maadui yanaendelea...na tunawataka wapiganaji wetu kuongeza mashambulizi dhidi ya makafiri," alisema katika taarifa iliyowekwa kwenye tovuti ya Waislam wenye msimamo mkali.

"Tunasema kwa jamaa zetu wapendwa wanaoishi kwenye maeneo yaliyo chini ya ukoloni wa Kenya kwamba sisi jamaa zenu hatotuacha kuja kuwasaidia."

"Mnapaswa kufahamu kuwa jihadi ndio njia pekee ya kujikomboa wenyewe kutoka katika unyanyasaji na udhalilishaji mnaokabiliana nao, kwahiyo mharakishe kujiunga na jihadi...na kuyakomboa maeneo yenu kutoka kwa Wakristo."

Diriye alipongeza shambuli la kigaidi katika chuo kikuu cha Garissa, Kaskazini Mashariki mwa Kenya, ambao magaidi wanne wa kikundi hicho waliwaua watu 148, wengi wao wakiwa wanafunzi. Wengi wa magaidi hao walikuwa Waislam kutoka nchini humo.
"Tunawapongeza ninyi na na Waislamu wengini duniani kwa operesheni ya kijasiri katika chuo kikuu cha Garissa," alisema kiongozi huyo wa magaidi, akieleza kuwa shambulio hilo lilikuwa la kulipiza kisasi kwa 'mauaji yaliyoidhinishwa na serikali ya Kenya dhidi ya mashehe na utekaji vijana wa Kiislam' kwenye maeneo ya pwani ya nchi hiyo.ambaye wakazi wake wengi ni Waislam.

"Muda wa Wakristo kufanya unyama bila kuwajibishwa umefikia kikomo," alisema. " Tunaswali kwako Mola kuodnoa maumivu ya Waislam katika Afrika Mashariki nzima - Ethiopia, Uganda na Djibouti."

"Hatotoacha jitihada za kuwasaidia, na milango ya mafunzo katika makambi yetu ipo wazi kuwapokea na makazi yetu yapo wazi kuwakaribisha."

Al-Shabaab, jina lenye maana 'vijana' kwa Kiarabu, waliibuka wakati wa mapambano makali dhidi ya majeshi ya Ethiopia, ambayo yaliingia nchini Somalia mwaka 2006 katika uvamizi ulioongozwa na Marekani kuung'oa utawala wa Muunganowa Korti za Kiislam ambao wakati huo ulikuwa ukitawala mji mkuu wa Mogadishu.

Magaidi wa Al-Shabaab wameendelea kufanya mashambulizi ya mara kwa mara, yenye malengo ya kupina madai kuwa kikundi hicho kinakaribia kushindwa kwenye operesheni inayoendeshwa na majeshi ya Somalia na yale ya Umoja wa Afrika, mashambulizi ya ndege ndogo zinazojiendesha zenyewe (drones) yanayofanywa na Marekani dhidi ya viongozi wa kikundi hicho, sambamba na wapiganani wanaotoroka kutoka katika kundi hilo la kigaidi.
Wakati hivi sasa kundi hilo la kigaidi linaungwa mkono na kundi jingine la kigaidi la kimataifa, Al-Qaeda, hisia zimekuwa zikiongezeka kwamba kundi hilo la Somalia linaweza kuhamisha utiifu wake kutoka kwa Al-Qaeda na kuelekea kwa kundi jingine hatari kabisa la kigaidi kimataifa la Dola ya Kiislam (Islamic States) au ISIS (kama linavyofahamika kwa kifupi).

Wakati flani, Al-Shabaab ilikuwa sumaku ya kuvuatia wapigania vijana wapiganaji kutoka mataifa mbalimbali, lakini mkakati wao kuwavutia wapiganaji wa kigeni umeathiriwa na kushamiri kwa ISIS huko Syria na Iraq, sambamba na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe ndani ya Al-Shabaab.

CHANZO: Imetafsiriwa kutoka tovuti ya eNCA



10 Apr 2015



NIANZE makala hii kwa kuomba radhi kwa makala zangu ‘kupotea’ kwa wiki mbili mfululizo. Hali hiyo ilitokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu.
Pia ningependa kutoa salamu za pole na rambirambi kwa ndugu zetu wa Kenya kufuatia shambulio kubwa la kigaidi lililotokea huko Garissa na kuuwa watu kadhaa.Ugaidi umeendelea kuwa moja ya matishio makubwa kwa usalama wa binadamu.
Wakati tukiungana na majirani zetu wa Kenya katika kipindi hiki kigumu, kuna dalili na sababu kadhaa za kiintelijensia na kimazingira zinazonipa wasiwasi kwamba Tanzania yetu inaweza kukumbwa na shambulio la kigaidi huko mbeleni (Mola aepushie). Hapa chini, ninabainisha dalili/ sababu hizo.
Tukio la ugaidi Garissa, nchini Kenya:
Wiki iliyopita, magaidi wa Al-Shabaab walifanya shambulio kubwa la ugaidi katika mji wa Garissa, uliopo mpakani mwa Kenya na Somalia.Shambulio hilo limepelekea vifo vya watu takriban 150 huku taarifa mbalimbali zikionyesha uwezekano wa kuwepo idadi kubwa zaidi ya waliouawa.
Awali, nilikuwa upande wa watetezi wa serikali ya Kenya na vyombo vya usalama vya nchi hiyo katika lawama kwamba walizembea kuchukua tahadhari. Hoja yangu kuu ilikuwa kwamba kupewa taarifa kuhusu ugaidi ni kitu kimoja, kuweza kuzifanyia kazi taarifa hizo na kuweza kuzuwia ugaidi ni kitu kingine kabisa.
Hata hivyo, utetezi huo umepungua baada ya kupatikana taarifa mbalimbali zinazoashiria mapungufu makubwa ya serikali ya Kenya na taasisi za Usalama nchini humo kukabiliana na tetesi walizopewa kuhusu uwezekano wa shambulio hilo la kigaidi.
Tukiweka kando kilichojiri nchini Kenya lakini tukitilia maanani ukweli kuwa nchi hiyo ilitahadharishwa kabla ya tukio hilo, kwa Tanzania hali ni tofauti. Hadi sasa hakuna taarifa rasmi ya uwezekano wa kutokea shambulio la ugaidi.
Hata hivyo, ni muhimu kutambua kuwa Kenya ina ushirikiano mkubwa zaidi na taasisi za kiusalama za mataifa makubwa zaidi ya Tanzania, hasa ikizingatiwa kuwa Marekani, kwa mfano, ina kituo chake cha kijeshi nchini humo (Manda Bay)
Kwa maana hiyo, tahadhari ya Wamarekani kwa Kenya sio tu kwa maslahi ya Kenya bali ya Wamarekani pia.
Hitimisho: Kwa kufanikiwa kufanya shambulio kubwa kabisa nchi Kenya, ikiwa ni takriban mwaka na nusu baada ya kufanya shambulio jingine la ugaidi kwenye supamaketi ya Westgate jijini Nairobi, magaidi wa Al-Qaeda wanaweza kushawishika kupanua kampeni yao ya uharamia hadi Uganda (ambako tayari kuna tishio kama ninavyoeleza hapo chini) na hata Tanzania (kwa sababu nitazobainisha mbeleni katika makala hii)
Uwezekano wa shambulio la kigaidi Uganda:
Machi 25 mwaka huu, Marekani ilitoa tahadhari kwa Uganda kuhusu uwezekano wa shambulio la kigaidi nchini humo. Kama ilivyo kwa Kenya, Marekani ina maslahi yake nchini Uganda ambako inarusha ndege zake za upelelezi (PC 12) kutoka Entebbe, Kwa hiyo usalama kwa Uganda una maslahi kwa Marekani pia.
Hitimisho: Iwapo Al-Shabaab watafanikiwa kutimiza uovu wao kuishambulia Uganda (Mungu aepushe hili), wanaweza kupata motisha wa kutanua zaidi kampeni yao hadi Tanzania hasa kwa kuzingatia kuwa kundi hilo la kigaidi linaziona nchi hizi tatu kama kikwazo kikubwa kwa uhai wake.
Shaka ya ugaidi nchini Tanzania:
Moja ya matatizo makubwa ya kufahamu ukubwa au udogo wa tishio la ugaidi nchini Tanzania ni siasa. Kwa muda mrefu, chama tawala CCM kimekuwa kikiutumia ugaidi kama kisingizio cha kudhibiti vyama vya upinzani na baadhi ya viongozi wake. Kwa minajili hiyo, hata serikali ikitoa taarifa sahihi kuhusu uwezekano wa tishio la ugaidi, kuna uwezekano wa wananchi wengi kudhani hiyo ni siasa tu.
Kana kwamba hiyo haitoshi, mwaka huu Tanzania itafanya uchaguzi mkuu wa Rais na wabunge hapo Oktoba. Japo haijazoeleka sana, historia inaonyesha kuwa angalau katika uchaguzi mkuu mmoja uliopita zilisikika taarifa za 'tishio la usalama' kutoka kwa nchi jirani. Mbinu hii hutumiwa na vyama tawala kujenga hofu ya kiusalama kwa wapigakura, na kuwaunganisha chini ya mwavuli wa chama kilichopo madarakani. Kwa mantiki hiyo, iwapo kutakuwa na taarifa za tishio la ugaidi, yayumkinika kuhisi baadhi ya wananchi wakatafrisi kuwa ni mbinu tu ya CCM kuelekea kwenye uchaguzi mkuu.
Lakini tatizo kubwa zaidi kwa sasa ni imani ndogo ya wananchi kwa serikali ya Rais Jakaya Kikwete na nyingi ya taasisi za serikali yake. Uhaba huo wa imani unatokana na mchanganyiko wa hisia za ushahidi wa matukio yaliyopita. Kutokana na kuandamwa mno na kashfa za ufisadi, kumeanza kujengeka imani miongoni mwa Watanzania kuwa serikali yao ni ya kifisadi pia.
Matumizi mabaya ya 'taarifa za kiintelijensia' yamewafanya Watanzania wengi kuwa na hisia kuwa 'taarifa za intelijensia' ni mbinu ya serikali kuwadhibiti. Mara kadhaa, Jeshi la Polisi limekuwa likipiga marufuku maandamano ya kisiasa au kijamii kwa kisingizio cha 'taarifa za kiintelijensia'.
Hivi karibuni, zilipatikana taarifa za mapigano makali kati ya jeshi la polisi wakishirikiana na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) dhidi ya 'magaidi' kwenye mapango ya Amboni mjini Tanga. Mchanganyiko wa taarifa za kukanganya na imani haba ya wananchi kwa jeshi hilo vilipelekea tukio hilo kuonekana kama 'mchezo wa kuigiza'.
Lakini licha ya kasoro hizo zinazoihusu serikali na taasisi zake, kuna tatizo jingine linalohusu vyombo vya habari vya nchini. Utitiri wa magazeti ya udaku na uhaba wa uandishi wa kiuchunguzi katika 'magazeti makini' umekuwa ukichangia mkanganyiko katika kubaini ukweli na porojo. Mfano mzuri ni tukio hilo la Amboni ambalo kwa kiasi flani liligeuka kama mfululizo 'series' ya mchezo wa kuigiza, huku magazeti ya udaku yakiwa na 'habari' nyingi zaidi ya 'magazeti makini.'
Hali hiyo yaweza kuwa inachangiwa na mahusiano hafifu kati ya taasisi za dola na vyombo vya habari, sambamba na mazoea ya taasisi hizo kutoa tu taarifa pasipo kuruhusu maswali kutoka kwa wanahabari. Ukosefu wa taarifa sahihi, sambamba na ugumu wa kupata taarifa hizo huchangia 'udaku' kuziba ombwe husika.
Tukiweka kando kasoro hizo hapo juu, hadi sasa kuna mambo yafuatayo ambayo yanaweza kuwashawishi magaidi kuvamia Tanzania.
1. Mgogoro wa muda mrefu kuhusu uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi
Japo hadi muda huu suala hili limeendelea kuwagawa Watanzania kwa njia za mijadala na kwa amani, yayumkinika kuhisi kuwa magaidi wanaweza kulitumia kama kisingizio cha kuishambulia Tanzania.
Cha kutia hofu ni ukweli kwamba si tu suala hili limedumu kwa muda mrefu, hasa baada ya chama tawala CCM kuahidi katika ilani yake ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2005 kuwa itaanzisha mahakama hiyo lakini imeshindwa kufanya hivyo hadi leo, bali pia uamuzi usio wa busara wa kuupeleka bungeni Muswada wa Uanzishwaji Mahakama ya Kadhi kisha kuuondoa.
Kana kwamba hiyo haitoshi, majuzi Rais Kikwete alikaririwa akidai kuwa serikali haina mpango wa kuanzisha mahakama hiyo, na badala yake jukumu hilo linabaki kwa Waislamu wenyewe. Haihitaji uelewa wa sheria kujiuliza kwamba kama suala hilo lilikuwa la Waislamu wenyewe, lilipelekwa bungeni kwa minajili gani?
Licha ya mjadala huo wa uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi kuendelea kwa amani, mjadala kuhusu suala hilo umewagawa viongozi wa dini (Wakristo na Waislamu) na kwa kiasi flani umerejesha mgogoro kati ya baadhi ya viongozi wa Kiislam na serikali, sambamba na kuleta sintofahamu miongoni mwa baadhi ya wanasiasa.
Yayumkinika kuhisi kuwa magaidi wanaweza kutumia ‘mgogoro’ huo kama kisingizio cha kufanya uovu wao. Na hii ni juu ya malalamiko ya muda mrefu kuwa Waislam wamekuwa wakibaguliwa na serikali huku Wakristo wakionekana kupendelewa. Uzoefu unaonyesha kuwa vikundi vya kigaidi vya kimataifa vina kasumba ya kuteka hoja za ndani ya nchi na kuigeuza yao, kwa kisingizio cha kupigania Uislam.
2. Vitisho bayana kutoka kwa watu wanaodai ni magaidi.
Hivi karibuni ilipatikana video huko nyumbani ambapo mtu mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Kaisi Bin Abdallah alidai kuwa kundi lao limekuwa na mafanikio katika ugaidi wa kudhuru polisi na vituo vya polisi.
Licha ya 'mapungufu kadhaa' katika video hiyo, ambayo yanaweza kutupa imani kuwa ni porojo tu, yawezekana tishio lililo kwenye video hiyo ni la kweli. Na hili ni moja ya matatizo ya kukabiliana na tishio la ugaidi: kuchukulia taarifa kuwa ni za kweli au za kupuuza.
Hofu kuhusu uwezekano wa matukio ya ugaidi nchini Tanzania ilithibitishwa na kauli ya hivi karibuni ya Rais Kikwete kuwa mashambulizi ya hivi karibuni dhidi ya vituo vya polisi katika maeneo mbalimbali nchini humo yana uhusiano na ugaidi, japo hakubainisha iwapo kuna uhusika wa makundi ya kigaidi ya kimataifa au la.
3. Taarifa za kimataifa:
Hadi muda huu hakuna taarifa za moja kwa moja zinazoashiria uwezekano wa tukio la ugaidi nchini Tanzania. Hata hivyo, bado kuna hali ya tahadhari ya wastani kuhusu uwezekano wa shambulio la kigaidi.
Wakati serikali ya Canada inaeleza kuwa haina 'ushauri unaohusu taifa (Tanzania) zima, inawashauri raia wake kuchukua tahadhari kubwa kuhusiana na ugaidi.
Kwa upande wake, serikali ya Uingereza inatoa angalizo la jumla tu japo inatahadharisha kuhusu tishio la ugaidi wa Al-Shabaab kwa eneo la Afrika Mashariki (ikiwa ni pamoja na Tanzania). Serikali ya Marekani inatoa ushauri wa jumla tu kwa kurejea matukio ya uvunjifu wa amani huko nyuma.
Hata hivyo, ripoti iliyotolewa Jumamosi iliyopita na taasisi ya HTH Worldwide kuhusu ‘hatari’ (risks) zinazoikabili Tanzania, ugaidi unatajwa kuwa ni tishio la kuaminika, japo uwezekano wa kutokea shambulizi la ugaidi ni wa wastani.
Pengine taarifa ya kuogofya zaidi ni ile iliyobainisha uwepo wa jitihada za kundi la kigaidi la ISIS kutaka kujiimarisha katika eneo la Afrika Mashariki, ikiwa ni pamoja na Tanzania. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ISIS inajaribu kujenga ushirikiano na Al-Shabaab kwa minajili ya kuwa na influence katika eneo la Afrika Mashariki.
Taarifa zaidi za kiintelijensia zinabainisha uwepo wa kikundi cha Al-Hijra nchini Tanzania, ambacho kinatajwa kama ‘tawi’ la Al-Shabaab nchini Kenya. Kwa mujibu wa taarifa hizo, kikundi hicho kinakadiriwa kuwa na wafuasi takriban 1,000.
Inaelezwa kuwa kikundi hicho kinafadhiliwa na Waislamu wa nje wa madhehebu ya Wasalafi (Salafist). Habari zaidi zinabainisha kuwa malengo ya kikundi hicho ni kuanzisha jihadi nchini Kenya na Tanzania. Uwepo wa kikundi hicho unadaiwa kusaidiwa na kikundi kingine cha Al-Muhajiroun ambacho kinatajwa kuwa na mahusiano na kikundi kingine cha kigaidi cha Al-Qaeda.
Kadhalika, majuzi zimepatikana taarifa kutoka Kenya kuhusu mwanamke mmoja wa Kitanzania aliyekamatwa na wenzie wawili Wakenya wakijaribu kwenda Somalia kuwa wenza wa magaidi wa Al-Shabaab.
Tukio hilo linaakisi kinachotokea katika nchi mbalimbali za huku Magharibi ambapo mabinti kadhaa wamekuwa wakitorokea Syria kwenda kuwa 'wenza' wa magaidi wa ISIS.
Vilevile, taarifa zilizopatikana muda mfupi kabla sijaandika makala hii zinaeleza kuwa mmoja wa wahusika wa shambulio hilo la kigaidi nchini Kenya ni Mtanzania. Haihitaji uelewa mkubwa wa intelijensia kutambua kuwa kama baadhi ya Watanzania wenzetu wanaweza kwenda kufanya ugaidi nje ya nchi, wanaweza pia kufanya ugaidi ndani ya nchi.
Hitimisho:
Ni vigumu kwa kuwa na hakika ya asilimia 100 iwapo magaidi watafanya shambulio au la. Kwa upande mmoja, magaidi wana muda wote wanaohitaji kabla ya kutimiza azma yao, yaani wanaweza kusubiri kwa muda mrefu, ilhali vyombo vya dola havina faida hiyo kwani vinatakiwa kuwa makini muda wote.
Kuna msemo maarufu kuhusu ugaidi, kwamba wakati magaidi wanahitaji DAKIKA MOJA TU kutimiza uovu wao, vyombo vya usalama vinahitaji KILA SEKUNDE YA DAKIKA kuwazuia magaidi husika.
Na japo uwepo wa taarifa za uhakika kuhusu uwezekano wa shambulio la kigaidi unaweza kusaidia jitihada za kukabiliana na magaidi husika, ukweli mchungu ni kwamba, kuwa na taarifa ni kitu kimoja, uwezo wa kuzitumia taarifa hizo ni kitu kingine.
Wakati huu tunaungana na wenzetu wa Kenya kulaani unyama wa Al-Shabaab, ni muhimu kuchukua tahadhari mahususi ili kuweza kukabiliana na uwezekano wa magaidi hao kushambulia Tanzania.
La muhimu zaidi ni umoja na mshikamano, ambao kwa hakika unapotea kwa kasi, na haja ya haraka kwa serikali kurejejesha imani ya wananchi kwake. Kingine ni umuhimu wa kuweka kando siasa katika masuala nyeti kama haya..
Kubwa zaidi ya yote ni la kitaalamu zaidi. Wakati serikali ya Tanzania imekuwa ikitegemea zaidi misaada ya kimataifa katika kuiimarisha kiuwezo Idara ya Usalama wa Taifa, ni muhimu jitihada za ndani pia zielekezwe katika kuijengea uwezo wa kukabiliana na matishio mbalimbali ya usalama wa taifa letu, ikiwa ni pamoja na hilo la ugaidi.
Kwa uelewa wangu, uwezo wa vitengo vya kuzuwia ugaidi na kitengo cha kupambana na ujasusi unaathiriwa na mapungufu ya kimfumo na kisera, sambamba na nafasi ya maafisa wa Idara hiyo kwenye balozi mbalimbali za Tanzania nje ya nchi 'kubweteka' na hisia ya teuzi zinazodaiwa kufanywa kwa misingi ya undugu, urafiki au kujuana.
Lakini changamoto kubwa zaidi kwa Idara yetu ya Usalama wa Taifa ni kurejesha imani kwa Watanzania. Nimeshawahi kuandika mara kadhaa kwamba kushamiri kwa ufisadi huko nyumbani kunachangiwa na udhaifu wa taasisi hiyo nyeti.
Zama za Idara hiyo ‘kuogopwa’ zimegeuka na kwa kiasi kikubwa taasisi hiyo, ambayo moja ya mafanikio yake makubwa huko nyuma yalikuwa kusimama imara dhidi ya njama na hujuma za utawala wa Makaburu, kwa sasa inaonekana kama sehemu ya mfumo wa kifisadi. Ili Idara yetu ya Usalama wa Taifa iweze kukabiliana na tishio hili la ugaidi inabidi iaminike kwa wananchi.
Mwisho, tishio hili la ugaidi sio la kufikirika. Lipo, na kwa bahati mbaya, mazingira ya kulirutubisha yapo pia. Japo si rahisi kuzuia ugaidi kwa asilimia 100, mikakati madhubuti ya kiintelijensia hususani katika kukabili ugaidi (counterterrorism) inaweza kuwakwaza magaidi kufikiria kuivamia nchi yetu

3 Apr 2015

Takriban watu 150 wameuawa katika shambulizi lililofanywa na kikundi cha kigaidi cha Al-Shabaab, katika eneo la Garisa, nchini Kenya. Katika tukio hilo la kinyama lililotokea saa 11 asubuhi kwenye Chuo Kikuu cha Garisa, magaidi hao waliwapiga risasi na kuwachinja wanafunzi Wakristo.baada ya kuwazidi nguvu walinzi.
Masked gunmen stormed the Garissa University College campus, in Kenya's north-east, yesterday
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Mail la hapa Uingereza, idadi ya waliouawa inafikia 147 na majeruhi ni 79 huku watu 500 wakiokolewa. Wengi wa waliouawa na wanafunzi wa chuo hicho, pamoja na polisi wawili,mwanajeshi mmoja na walinzi wawili.



Kenyan soldiers and police officers pictured at Garissa University College in Kenya where 147 people were murdered by terrorists yesterday

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Kenya, Joseph Nkaissery , alieleza kuwa magaidi wanne walijifunga mabomu, na polisi walipowapiga risasi, walilipuka kama mabomu ambapo vipande vya mabomu hayo viliwahjeruhi polisi.
Kenyan police officers, pictured, take cover across from the university during the terrorist gun attack

Maafisa wa usalama katika eneo la tukio walieleza kwamba mateka kadhaa waliokolewa, na magaidi wanne waliokuwa na bunduki aina ya AK-47 waliuawa.
Kenyan security officials at the scene said dozens of hostages were freed and four of the gunmen were killed
Jana usiku, Kituo cha Operesheni ya Uokoaji Kitaifa kilieleza kwamba idadi ya wanafunzi wote, wazima na waliouawa sasa inafahamika.
Students fled the area, some of them without shoes, after the al-Shabaab terrorists launched their attack

Just last week, the Chief Security Officer at the University of Nairobi feared an attack was imminent and issued a security warning - but it is unclear whether the same information was relayed to Garissa officials 

Students ran for their lives as the terrorists launched their attack on the college campus in Kenya yesterday

Escape: Students pictured fleeing from the university. The death toll rose to 147 as the siege ended last night

Some of the students did not have time to dress as they fled for their lives when faced by the gunmen

Distraught: Paramedics help a woman injured during the attack on the Garissa University College campus

Shambulizi hilo linaelezwa kuwa baya zaidi nchini humo katika miaka 17 baada ya shambulizi jingine kubwa la kigaidi  mwaka 1998 kwenye Ubalozi wa Marekani nchini humo ambalo lilipelekea vifo zaidi ya 200.
Heavily armed soldiers pictured outside the Garissa University College campus where 147 people were murdered

Safety: A student hostage is escorted out of Garissa University College after Kenya Defence Forces ended a siege by terrorist gunmen

A Kenyan soldier runs for cover near Garissa University College's perimeter wall where 147 people have been killed

Rescued: A woman is led to safety from the building where she was held hostage by al-Shabaab terrorists





An injured man on a stretcher is taken to Kenyatta National Hospital following the attack by al-Shabaab terrorists

Medical treatment: An injured man arrived at Kenyatta National Hospital in Kenya's capital, Nairobi following the raid by terrorists



Tukio hilo la jana limetokea katika Juma Kuu, kipindi cha majonzi katika kalenda ya Wakristo. Jana ilikuwa Alhamisi Kuu ambayo kwa mujibu wa taratibu za baadhi ya madhehebu ya Kikristo, ni siku ya maungamo. Leo, Ijumaa Kuu, ni siku ya maadhimisho ya kusulubiwa kwa Yesu Kristo msalabani na hatimaye kufa. Jumapili ijayo ni Pasaka ambapo Wakaristo wanaadhimisha ufufuo wa Yesu Kristo.
A Kenya Defence Forces soldier carries a machine gun outside Garissa University College on April 2 2015

Captured: The Kenyan military launched a major security operation and detained one terrorist trying to escape

A Kenya Defence Forces tank driven outside Garissa University College. Al-Shabaab terrorists raided the campus shortly after 5am local time yesterday, overwhelming guards and killing anyone they suspected of being a Christian

Kenyan police managed to arrest one of the terror suspects, right, after he tried to flee from the campus

The death toll rose to 147 tonight and the siege ended, according to the country's disaster response agency. A total of 79 were injured, 587 were led to safety


Most of those killed were students but two police officers, one soldier and two watchmen are among the dead

Tragedy: Last night, officials confirmed the security operation is now over but the death toll has reached 147

Gunfire: A Kenya Defense Force soldier takes cover near the perimeter wall of Garissa University College

Kenyan soldiers took cover as heavy gunfire continued at Garissa University College in Kenya yesterday

Kenyan security officials at the scene said dozens of hostages were freed and four of the gunmen were killed

A Kenyan soldier takes cover as shots are fired in front of Garissa University College in Garissa town, located near the border with Somalia

Maafisa usalama wa Kenya walieleza kuwa gaidi mmoja alikamatwa wakati anajaribu kutoroka. Kadhalika, serikali ya nchi hiyo imetangaza zawadi ya Shilingi za Kenya Milioni  20 kwa atakayewezesha kukamatwa kwa Mohammed Mohamud, anayejulikana pia kama Dulyadin, au Gamadhere, ambaye anatuhumiwa kupanga shambulizi hilo.

A £145,000 reward has been offered for information leading to the capture of Mohamed Mohamud, who is believed to have masterminded the attack

Wanausalama nchini humo wanaamini kuwa gaidi huyo ni mkuu wa operesheni za kigaidi wa kundi la Al-Shaabab.Inaaminika kuwa gaidi huyo ametumia muda mwingi kuwafunza magaidi watarajiwa kwenye madrasa mbalimbali.Pia anatuhumiwa kuhususika na shambulizi jingine la kigaidi lililotokea Novemba 22 mwaka jana huko Mkka, nchini humo, ambapo watu 28 waliuawa.
A Kenyan soldier takes cover as shots are fired in front of Garissa University College in Garissa town, located near the border with Somalia
Mkuu wa Polisi, Joseph Boinet, alitangaza amri ya kutotembea ovyo kuanzia saa 12 unusu jioni hadi saa 12 unusu asubuhi.katika mikoa minne inayopakana na Somalia kama tahadhari ya kiusalama.

Chuo kilichokumbwa na shambulizi hilo kina takriban wanafunzi 887 wanaoishi katika mabweni sita



Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Collin Wetangula, Makamu Mwenyekiti wa Serikali ya Wanafunzi chuni hapo, alieleza kuwa yeye na wenzake waliposikia milio ya bunduki walijificha kwa kujifungia chumbani.

"Nilisikia milio ya bunduki, lakini hakuna mtu aliyepiga kelele, kwa hofu ya kuwashtua wanaofanya shambulio hilo."

"Watu hao waliokuwa wakifyatua risasi walikuwa wanasema 'sisi ni Al-Shabaab'"

Wetangula alieleza zaidi alisikia magaidi hao wakihoji wanachuo kuhusu dini zao (kama ni Waislam au Wakristo). Alisema, "Ukiwaambia wewe ni Mkristo, walikupiga risasi hapohapo. Kila mlio wa bunduki ulinifanya nijisikie kama nakufa."

"Baadaye tulipochungulia dirishani tuliwaona watu wenye sare za jeshi ambao baadaye walijitambulisha kuwa ni maafisa wa jeshi la Kenya."
Kenyan authorities have airlifted some of the wounded to Nairobi for treatment following the attack yesterday morning

Msemaji wa magaidi wa Al-Shbaab alitangaza kuwa kundi lake linahusika na shambulizi hilo. Sheikh Abdiasis Abu Musab, 'msemaji wa operesheni za kijeshi za Al-Shabaab,' alisema, "Tuliwachambua watu, na kuwaachia huru Waislam.Kuna miili mingi ya Wakristo, na tunawashikilia wengine kadhaa."

Rais Uhuru Kenyatta alieleza baadaye kuwa anaharakisha ajira ya askari 10000 ili kukabiliana na tishio la magaidi hao.
Treatment: Paramedics attend to an injured Kenyan student as she is wheeled into Kenyatta National Hospital in Nairobi
Wiki iliyopita, Afisa Mkuu wa Usalama katika Chuo Kikuu cha Nairobi alitoa tahadhari ya uwezekano wa shambulio la kigaidi lakini bado haijafahamika kuwa iwapo taarifa hizo zilitolewa kwa Chuo Kikuu cha Garisa pia.

Wounded: A man with a leg injury arrived at hospital in Kenya's capital. The death toll has risen to 147

Grace Kai, mwanafunzi wa Chuo cha Ualimu cha Garisa, alieleza kuwa walipewa tahadhari kuwa kuna uwezekano wa kutokea shambulio la kigaidi. Alisema, "Sura ngeni zilionekana Garisa, na kulikuwa na hisia ni magaidi."

"Jumatatu, Mkuu wa Chuo alitupa tahadhari...kwamba kuna sura ngeni zimeonekana maeneo ya chuoni hapo."
Kenyan officials had warned that al-Shabaab were suspected of planning a major assault on the college 
"Kisha Jumanne, tuliruhusiwa kurejea majumbani, na chuo kufungwa., lakini kampasi iliendelea kuwa wazi...na sasa wameshambulia."

CHANZO: The Mail Online


25 Mar 2015


Wiki mbili zilizopita niliandika makala iliyoonya tabia iliyoanza kuzoeleka kwa baadhi ya viongozi waandamizi wa CCM kufanya mzaha kuhusu ugaidi. Kwa muda mrefu sasa, viongozi wa chama hicho hususan Nape Nnauye na Mwigulu Nchemba wamekuwa wakiihusisha Chadema na ugaidi. Lakini tabia hiyo haikuanzia kwa Chadema pekee kwani huko nyumaCUF nayo ilikumbwa na tuhuma kama hizo kutoka kwa CCM.

Katika makala hiyo ambapo nileleza kwa kirefu kiasi kuhusu hatari inayoikabili dunia hivi sasa kutoka kwa vikundi vinavyoongoza kwa ugaidi kwa muda huu, yaani ISIS, Al-Qaeda, Boko Haram na Al-Shabaab, nilitahadharisha kwamba tabia ya CCM kuufanyia mzaha ugaidi, kwa maana ya kuzusha tu 'Chadema ni magaidi au CUF ni magaidi', inaweza kutugharimu huko mbeleni. Nilibainisha kuwa mzaha huo unaweza kuwarahisishia magaidi halisi dhima ya kushambulia nchi yetu, kwani 'tayari tuna magaidi wa ndani- kwa maana ya tuhuma za CCM dhidi ya Chadema na CUF.

Vilevile nilitanabaisha kwamba kuufanyia mzaha ugaidi kunaufanya uzoeleke, uonekane ni kama jambo la kawaida tu ambalo halikauki midomoni mwa akina Nape na Mwigulu.Lakini pengine baya zaidi ni vyombo vyetu vya dola kuwekeza nguvu kubwa kudhibiti 'magaidi hewa' hali inayoweza kuwapa upenyo magaidi halisi.

Kwa bahati mbaya, tahadhari niliyoitoa kwenye makala hiyo inelekea kubeba uzito, baada ya kupatikana taarifa kwamba kikundi hatari kabisa cha magaidi cha ISIS kina mpango wa kujienga na hatimaye kufanya mashambulizi katika ukanda wa Afrika Mashariki, ikiwa ni pamoja na Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa za kituo cha televisheni cha Aljaazera, mawasiliano ya hivi karibuni ya kikundi hicho cha kigaidi yanaonyesha kuwa kinajaribu kujijenga Afrika Mashariki, eneo ambalo limekuwa likisumbuliwa na magaidi wa Al-Shabaab na Al-Qaeda kwa vipindi tofauti.

Hivi karibuni, kikundi cha kigaidi cha Boko Haram cha Nigeria kimetoa ahadi ya utiifu kwa ISIS, hatua iiliyotafsiriwa na wachunguzi wa masuala ya ugaidi kuwa inaweza kuongeza nguvu za ISIS katika maeneo mbalimbali ya bara la Afrika.

Hata hivyo, kitu ambacho hakikufahamika kwa wengi ni kwamba tukio hilo la Boko Haram kuonyesha utii wa ISIS lilitanguliwa wiki chache kabla ya ujumbe uliotumwa kwa kiongozi wa Al-Shabaab , Abu Ubaidah, kumwomba afanye kama walivyofanya Boko Haram (kutangaza utii kwa ISIS)

Ujumbe huo uliwasilishwa na  Hamil al-Bushra, jina linaloaminika kutumiwa na vyanzo viwili vya habari vinavyohusishwa na ISIS.

Katika ujumbe huo, Bushra aliwapongeza Al-Shabaab na kuwahamasisha wafanya mashambulizi Kenya, Ethiopia na TANZANIA.

Soma habari kamili HAPA

23 Sept 2013

Fleeing: A child runs to safety across the shopping mall following the deadly attack in Nairobi, Kenya

Terror: Armed police guide a woman carrying a child to safety at Westgate shopping centre in Nairobi

Nadhani utakuwa umemuona huyu jamaa (kushoto) kwenye picha za TV zinazoeleza kilichotokea na kinachoendelea katika tukio la kigaidi kwenye Mall ya Westgate , jijini Nairobi nchini Kenya. Kwa hakika ninamuona kama mmoja wa mashujaa wakubwa katika harakati za kukabiliana na magaidi na kuokoa maisha ya wahanga wa tukio hilo.Sina hakika kama ni polisi au shushushu lakini picha mbalimbali zinazomwonyesha, zinathibitisha kuwa ni mmoja wa mashujaa wanaoweza kuingia kwenye kumbukumbu za muda mrefu kuhusu tukio hili la kusikitisha. Anaglia baadhi ya picha zinazomhusu.



Kenya Westgate siege

Helping out: British High Commissioner to Kenya, Christian Turner (left) lies on a bed after donating blood, following the overwhelming numbers of casualties from the shooting

Balozi wa Uingereza nchini Kenya, Christian Turner, alikuwa miongoni mwa waliojitolea damu kuokoa maisha ya majeruhi wa tukio hilo. Huu ni mfano wa kuigwa.

BOTTOM LINE IS, tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa wenzetu Wakenya na katika tukio hili kwa ujumla.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.