Showing posts with label BLANDINA NYONI. Show all posts
Showing posts with label BLANDINA NYONI. Show all posts

31 Jan 2012

Blandina Nyoni

Lucy Nkya

Default Kituko Wizara ya Afya, Blandina Nyoni haivi na Lucy Nkya. Hawasalimiani hata wakikutana kwenye kordo

Ndugu zangu hii taarifa nimeipata kutoka kwa wandani wangu aliopo pale Wizara ya Afya. Kwamba Katibu Mkuu wa Wizara Bi Brandina Nyoni haivi na Naibu Waziri wake, Bi Lucy Nkya. Na inadaiwa kuwa hata wakikutana kwenye kordo huwa hawasalimiani. Kinachowazungumzisha ni Madokezo tu. 


Taarifa inasema kwamba ugomvi wao ulitokana na kitendo cha Katibu Mkuu kutaka kumlazimishia kumpa Dereva (Elias Mkumbo) ambae ni Informer wake. Mama Nkya alipotonywa na watumishi wa pale akamkataa huyo Dereva na ali command alitewe dereva aliyekuwa nae kutoka Wizara aliyokuwepo kabla kama sivyo abadilishiwe. Tangu wakati huo Wakuu hawa wa Wizara wamesusiana (Kama wanavyosema watu wa Pwani). 


Blandina Nyoni amekumbwa na matukio mengi ya kususiana na Wakubwa wenzako toka alipokuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii ambapo alikuwa haivi na hasalimiani na Waziri wake Bi Shamsi Mwangunga. Alipohamishiwa Afya mwishoni mwa 2008 pia akagombana na Naibu Waziri wa wakati huo Bi Aisha Kigoda na hadi anaondoka Wizarani hapo bado walikuwa hawaivi. Sijui huyu Mama ni Mtu gani? Maana hata watumishi wake kuazia alipokuwa Hazina, Maliasili na Sasa Afya wamekuwa wamkimkataa kutokana na Uongozi wake Mbovu wa kutojali maslahi halali ya watumishi wake mfano malipo ya likizo, uhamisho, extra duty allowances, etc!
CHANZO: Jamii Forums 

19 Nov 2008


Kwa mujibu wa gazeti la kila wiki la Changamoto,toleo la wiki hii,mahusiano ya kikazi kati ya Waziri wa Maliasili na Utalii Bi Shamsa Mwangunga na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi Blandina Nyoni ni mabovu kiasi kwamba hawapiti mlango mmoja wa kuingilia na kutokea ofisini.

Kwa mujibu wa gazeti hilo,inasemekana chanzo cha uhasama huo ni tofauti za kimtazamo katika utendaji kazi ambapo mmoja wao anadaiwa kuzingatia taratibu na sheria katika utekelezaji wa majukumu yake huku mwenzie akitaka kupindisha kwa sababu anazojua yeye.

Uhasama kati ya vigogo hao unadaiwa kuanza nyuma kabla ya sasa kwani wakati flani wote walikuwa viongozi waandamizi wa Mamlaka ya Majisafi na Maji Taka (DAWASCO).Inaelezwa pia kuwa uhasama huo umepelekea mmoja wao kuwa "anaingizwa mkenge" kwa kupewa taarifa feki za kuwapo kwa nyara za serikali na hivyo kulazimika kulipa dola 70 baada ya kukagua kontena na kugundulika kuwa halikuwa na nyara zozote.

Kumbukumbu zinaonyesha kwamba Wizara hii imekuwa na desturi za migogoro baina ya watendaji wake wakuu ambapo ilisharipotiwa huko nyuma kuhusu mgogoro kati ya aliyekuwa Waziri wakati huo,Anthony Diallo na aliyekuwa Mkurugenzi wa Wanyamapori,Bw Severe,kisha "bifu" kati ya aliyekuwa Waziri,Prof Jumanne Maghembe na aliyekuwa Katibu Mkuu,Salehe Pamba.

SWALI LA KUJIULIZA,MIGOGORO HII SIO DALILI ZA MGONGANO KATI YA WAPINGA UFISADI NA WALEA UFISADI?JEURI YA WALEA UFISADI INATOKA WAPI?UFANISI UTAPATIKANA VIPI IWAPO WATENDAJI WAKUU WANAWINDANA KAMA PANYA NA PAKA?KWA STAILI HII MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA YATAWEZEKANA KWELI?

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.