Showing posts with label MABOMU. Show all posts
Showing posts with label MABOMU. Show all posts

4 May 2009

NA KUNA BOMU JINGINE LA ASKARI WASTAAFU.KILA NISOMAPO HABARI KUWA WASTAAFU WA JESHI WANAZUNGUSHWA KUHUSU MAFAO YAO,NAPATWA NA UOGA FLANI KWAMBA WASIJE KUAMUA KUTUMIA UJUZI WAO WA KIJESHI KUDAI HAKI ZAO.
NA NIPITAPO PALE MWENGE KWENYE FLATS ZA JESHI NA KUANA NAMNA "ZILIVYOCHOKA" NAPATWA NA HOFU NYINGINE SIKU WAUNGWANA HAWA WATAKAPOAMUA KUDAI KWA NGUVU MAISHA BORA KAMA YALE YA VIGOGO KULE MASAKI,MIKOCHENI,OYSTERBAY,NK.TALKING OF OYSTERBAY,NAPATA KUMBUKUMBU YA YALE MAHEMA WANAYOISHI ASKARI POLISI KATIKA "KAMBI" ILIYO JIRANI NA KITUO CHA POLISI OYSTERBAY.
BOMU JINGINE NI HAO MGAMBO AMBAO KULA NA ANASA ZAO ZINATEGEMEA KUVUNJA HAKI ZA BINADAMU ZA WAMACHINGA,WANAODIWA KODI ZA MANISPAA/HALMASHAURI NA WANYONGE WENGINE.MOST OF MGAMBO HAWA HAVE NO IDEA WHATSOEVER KUHUSU HUMAN RIGHTS.WANACHOJUA WAO NI PIGA,NYANG'ANYA,TAIFISHA!HAWA NI VIUMBE HATARI ZAIDI KWA VILE MAISHA YAO KWA KIASI KIKUBWA YANATEGEMEA UBABE WAO DHIDI YA WANYONGE WAO.KWA MFANO,MARA NYINGI LUNCH ZAO NI VYAKULA WANAVYOWAPORA MAMA NTILIE NA VITOWEO WANAVYORUDI NAVYO BAADA YA KUMALIZA KAZI NI VILEVILE WANAVYOWAPORA WANANCHI WANAOJITAFUTIA RIDHIKI ZAO HALALI.
KUNA MTU AMENINONG'ONEZA SOMETHING HE CALLED FACTS ETI HUO MLIPUKO WA MABOMU NI HUJUMA.I DIDNT TAKE HIM SERIOUS KWA VILE ALIKUWA AMEONJA KILEVI KIDOGO.HE WENT FURTHER TO ARGUE KWAMBA VIRUSI (VIRUS) WA HUJUMA WAMEANZA KUSAMBAA KUTOKA KWA MAFISADI KWENDA KWA PROFESSIONALS WALIOSAHAULIKA AU KUTELEKEZWA.REASONS HE CITED,KAMA MZEE WA VIJISENTI AMEJICHOTEA BILIONI ZAKE KADHAA NA BADO HAJAGUSWA,AU MAJAMBAZI WA RICHMOND BADO WANAPETA LICHA YA KUBAINISHWA NA KAMATI YA MWAKYEMBE,NA DOWANS NAO WANAENDELEA NA JEURI YA KUIPELEKA TANESCO MAHAKAMANI LICHA YA HIZO MILIONI MIA NA USHEE PER DAY WALIZOZAWADIWA,WAMILIKI WA KAGODA WAMEENDELEA KUWA GHOSTS WASIOTAJIKA,THEN MTU YEYOTE ANWEZA KUSHAWISHIKA KUWA FISADI,MHUJUMU WA UCHUMI AU USALAMA,AU MLIPUA MABOMU!DRUNK AS HE WAS BUT THIS KINDA MADE SENSE TO ME!
KUNA BOMU JINGINE KUBWA ZAIDI YA HAYO HAPO JUU,AU ZAIDI YA HAYO YALOKWISHALIPUKA.KWA UPANDE MMOJA NI RESERVE ARMY OF LABOUR,INAYOZALISHWA NA UBINAFSISHAJI,KUPUNGUZA MATUMIZI,"KEEP CITY/TOWN CLEAN OPERATIONS" (KAMA HIZO ZA MGAMBO ZINAZOISHIA KUWAFANYA WAMACHINGA WAJIULIZE "TUFANYE NINI ILI TUSIBUGHUDHIWE,AU TUWE WAPORAJI?"),WAKULIMA WALIOFIKIA HATUA YA KUTAFSIRI KUWA KILIMO NI SAWA NA KIFUNGO BCOZ CO-OPS HAZITAKI KULIPA MADENI HUKU WASSIRA NA WIZARA YAKE WAKIWA KWENYE SUINGIZI WA PONO KUHUSU KUTAFUTA MASOKO KWA WAKULIMA,NA MAKUNDI KAMA HAYO.KWA UPANDE MWINGINE NI WANANCHI WALALAHOI WANAOSIKIA NAMNA MAFISADI WANAVYOWADHIHAKI KWA PRESS CONFERENCES HUKU WAKITETEWA NA BAADHI YA VIONGOZI,WANANCHI WALIOCHOSHWA NA DANADANA ZA KUMWEKA WAZI MMILIKI WA KAGODA,WALIOKATISHWA TAMAA NA AHADI BAADA YA AHADI KUWA MAISHA BORA YAKO NJIANI (AS WE APPROACH THE GENERAL ELECTION,THEY WOULD KEEP ON REMINDING US THAT WE ARE NOW APPROACHING THE MAISHA BORA DESTINATION,EVERYBODY SHOULD REMAIN SEATED TILL WE ARRIVE i.e. BAADA YA GENERAL ELECTION,MEANING RETURNING THEM TO POWER AND GOING BACK TO SQUARE ONE.IF THEY BOTHER GIVING EXCUSES AS TO WHY IT'S FEBRUARY 2011 AND WE ARE YET TO ARRIVE AT MAISHA BORA,THEY WOULD PROBABLY SAY "OH,TUMEPOTEA NJIA.MSIHOFU TUTAFIKA MUDA SI MREFU...."
MABOMU HAYA NILIOBAINISHA KWENYE STORI HII NI HATARI ZAIDI KULIKO HAYO YANAYOLIPUKA HUKO MBAGALA.YATAKAPOLIPUKA,SI TUME YA MKUU WA MAJESHI WALA NGONJERA ZA "TUTALIPA FIDIA" ZITAKAZOWEZESHA KUREJESHA HALI KWENYE UTULIVU.THE TIME IN NOW.IT'S NOW OR NEVER!

ANYWAY,HEBU TUSIKIE HADITHI ZA ROSTAM KUHUSU TUHUMA ZILIZOTOLEWA (NA REGINALD MENGI) DHIDI YAKE NA WAHINDI WENZIE KWAMBA WAO NI MAFISADI PAPA.

Rostam amlipua Mengi, amwita nyangumi wa ufisadi


Ramadhan Semtawa na Salim Said


MFANYABIASHARA wa jijini Dar es salaam, Reginald Mengi aliwabatiza wafayabiashara wenzake watano jina la "mapapa wa ufisadi", na sasa mmoja wa waliotuhumiwa amejibu mapigo kwa kumbatiza jina la "nyangumi wa ufisadi".


Rostam Aziz, ambaye ni mmoja wa wafanyabiashara watano waliotuhumiwa na Mengi kuwa mapapa wa ufisadi, jana alitoa mlolongo wa tuhuma za ufisadi dhidi ya mwenyekiti huyo mtendaji wa makampuni ya IPP, na kueleza kuwa atawasilisha vielelezo kwa vyombo husika ndani ya saa 48 ili Mengi aanze kuchunguzwa.


Mapigo ya Rostam, ambayo yanazidi kupandisha joto la vita hiyo ya maneno, yametokana na tuhuma nzito ambazo Mengi alizitoa Aprili 23 wakati alipotaja wafanyabiashara watano akitaka wadhibitiwe mapema, akiwemo mbunge huyo wa
Igunga. Tofauti na Mengi ambaye hakutoa vielelezo na kusema yuko tayari kupandishwa kizimbani ili ukweli udhihirike, Rostam aliorodhesha tuhuma nyingi na kuahidi kuzikabidhi kwenye vyombo vya serikali ili hatua zichukuliwe. Huku akimtaja Mengi kwa majina yote matatu kila wakati, Rostam, aliwaambia waandishi jana akisema: "... nataka niweke wazi kwamba tuhuma zote zilizotolewa na Mengi dhidi yangu ni za uongo na ni upuuzi mtupu. Tuhuma hizo ni mwendelezo wa wimbo ule ule ambao amekuwa akiuimba kwa muda mrefu sasa na tayari nilikwishazitolea kauli huko nyuma.


"... nimeamua kuitisha mkutano huu ili kuwaeleza, na kupitia kwenu kuwaelimisha Watanzania, wamjue Reginald Abraham Mengi katika sura yake halisi na dhamira yake chafu na ovu, na kumtambua kwamba mtu huyu ni nyangumi wa ufisadi katika nchi hii," alisema Rostam katika moja ya aya zake za utangulizi. Nyangumi ni samaki wa baharini aliye mkubwa kuliko papa. Rostam alianza kwa kuorodhesha matukio 10 ya ugomvi ambayo anadai Mengi aliuanzisha dhidi ya watu mbalimbali, kuanzia maaskofu hadi kikundi cha uchekeshaji, wakati kwa mujibu wa Rostam maslahi ya Mengi ya kibiashara yalipoingiliwa na baadaye kuyageuza kuwa ni ugomvi wa nchi nzima.


"Sasa ameanzisha ugomvi na mimi baada ya kuona kwamba mimi nimekuwa mshindani wake mkubwa katika umiliki wa vyombo vya habari hapa nchini, anataka kuufanya ugomvi wa nchi nzima," anaeleza Rostam. Akiorodhesha tuhuma za ufisadi dhidi ya Mengi, Rostam alidai mwenyekiti huyo wa IPP alianza kuifilisi nchi kwa kushiriki kwenye vitendo vilivyochangia kuifilisi Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) na kusababishwa iuzwe "kwa bei poa".


Alidai kuwa Mengi, akitumia kampuni yake ya Anche Mwedu Ltd katika miaka ya themanini, alichukua mkopo wa fedha NBC na amegoma kulipa hadi leo, huku akilazimisha suala hilo lifikishwe mahakamani. Rostam alidai kuwa mkopo wa kwanza uliotolewa kupitia hati ya maandishi ya makubaliano, ulifikia jumla ya Sh3.2 bilioni na kwamba hadi Januari mwaka 1996 ulifikia riba ya Sh 1.7 bilioni.


Alidai mkopo wa pili chini ya kampuni hiyo ulikuwa wa mpango wa Loan Agreements na ulihusu jumla ya Sh386,746,631.06 hadi kufikia Januari 1996. Akiongeza kudai kuwa mkopo wa tatu ulikuwa chini ya utaratibu wa udhamini wa serikali (government guarantee) ambao ulikuwa wa jumla ya Sh1,803,137,210 hadi kufikia Januari 1996. Rostam alidai kupitia utaratibu mwingine, Mengi alichukua mkopo mwingine ambao ulihusu jumla ya Sh417.6 milioni hadi kufikia Januari 1996.


"Jumla ya fedha zote za NBC ambazo amekuwa akidaiwa Mengi kupitia kampuni yake ya Anche Mwedu Limited (AML) hadi kufikia Januari 1996 zilikuwa ni Sh 5.8 bilioni, fedha hizi hadi kufikia sasa 2009 pamoja na riba zinafika takriban Sh28 bilioni," alidai Rostam huku akitaka akaunti za benki ambazo mikopo hiyo ilipitia. "Hivi ndivyo Mengi alivyochangia kuifilisi NBC, benki ya wananchi masikini wa Tanzania. Fedha hizi zilizochukuliwa na Mengi Sh28 bilioni zinaweza kujenga shule za sekondari 100 ambazo zingeweza kuwanufaisha watoto wa kimaskini wa Tanzania." Rostam pia alidai kuwa Mengi aliteketeza Sh2.5 bilioni kwa kutumia kampuni ya uwekezaji ya wazalendo ya NICO, kwa kununua hisa za kiwanda cha Interchem Pharma Ltd kinachomilikiwa na familia yake ambacho Rostam alidai kuwa Mengi alijua kuwa kingekufa.


"Huku akijua hali mbaya ya kiwanda hicho alitumia nafasi yake kuziteketeza Sh2.5 bilioni fedha za Watanzania masikini wasiopungua 22,000 wenye hisa NICO kwa kuifanya inunue asilimia 51 ya hisa. Kiwanda hicho sasa kimewekwa kwenye orodha ya kufilisiwa baada ya kushindwa kujiendesha chini ya mwaka mmoja tokea Mengi kuizamisha NICO," alisema. Rostam, ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu na Kamati Kuu ya CCM, pia alidai Mengi kwa kutumia mpango wa Mfuko wa Kuagiza Bidhaa kutoka Nje (Commodity Import Support-CIS), alichukua fedha nyingi kupitia msaada wa nchi wafadhili, lakini hadi jana alikuwa hajazilipa.


Rostam alikiri kwamba wafanyabiashara wengi akiwemo yeye walikopa, lakini wamelipa na wanaendelea kulipa hadi sasa na kuongeza kwamba Mengi "anayejidai ana uchungu na Watanzania amekuwa akiwaongezea umasikini kwa kuchota fedha hizo baadaye kuruka na kukataa kuzilipa". Rostam pia alitoa mchanganuo huo wa fedha za CIS ambazo alidai Mengi alizipata na kutaja nchi zilizotoa, akianza na Norway ambayo alidai mwaka 1988 hadi 1989 iliisaidia kampuni ya IPP kupitia kampuni ya Anche Mwedu kupata Krona 6milioni, na baadaye kupitia kampuni hiyo hiyo ilipata Krona 4 milioni.


Alidai mwaka 1991/92, Japan ilisaidia Bonite Bottlers kuchukua Yen 160 milioni na baadaye ikasaidia Medicare kupata Yen 115 milioni na Canada mwaka 1988/89 ikasaidia Anche Mwedu dola za nchi hiyo 0.5milioni. Pia alidai mwaka 1988/89 Italia ilisaidia Anche Mwedu kupata Lira 1.7milioni, Japan 1997 ilisaidia Anche Mwedu Yen 20milioni na Japan tena 1994 ilisaidia Bonite Bottlers kupata Yen nyingine 160 milioni.


Pia alidai Tume ya Uchumi ya Ulaya (European Economic Commission-EEC), katika kipindi cha mwaka 1988/89 ilisaidia Bonite Bottlers kupata EEU 0.5199. "Fedha hizi zilizo katika sarafu tofauti za kigeni zikibadilishwa kwa shilingi za Tanzania na riba kwa miaka yote tokea zilipochukuliwa zinafikia mabilioni ya shilingi," alisema Rostam. "... badala ya kurejesha fedha hizi... Mengi alizitumia kujitajirisha."


Pia alidai kuwa Mengi aliingia ubia na serikali katika umiliki wa kiwanda cha Tanpack Industries Ltd, lakini bila ya kumjulisha mbia wake (serikali) alitumia dhamana ya kiwanda kukopa Sh600 (sic) kutoka benki ya NBC na "kuzitumia kwa njia anazozijua yeye". "Benki hiyo ilipochachamaa kutaka ilipwe fedha zake, Mengi alitaka Tanpack ilipe lakini serikali ikakataa kulitambua deni hilo... Matokeo ya ufisadi huo wa Mengi, Tanpack ikafilisiwa na kufa," alidai Rostam. Miongoni mwa matukio ambayo Rostam alidai Mengi alikorofishana na watu mbalimbali ni pamoja na zabuni ya ubinafsishaji hoteli ya Kilimanjaro (sasa Kempiski).


"Alianzisha ugomvi na aliyekuwa Waziri wa Utawala Bora Mheshimiwa Wilson Masilingi baada ya kushindwa zabuni ya ubinafsishaji wa hoteli ya Kilimanjaro, akataka kuufanya kuwa ugomvi wa nchi nzima," alidai Rostam. "Katika kudhihirisha jinsi alivyo na chuki na visasi kutokana na kuikosa tu hoteli hiyo, amekuwa hakanyagi na hata kushiriki shughuli yoyote inayofanyika katika hoteli hiyo." Kuhusu kutajwa kwenye ufisadi katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), Dowans na tuhuma nyingine, Rostam alisema "hizo zote nimekwishazitolea maelezo... ni porojo tu hakuna hata moja ninayohusika nayo".


Ni vema Watanzania wakafahamu kwamba kila anapokabiliwa na matatizo au anapotenda maovu, kimbilio lake la haraka la kujifichia limekuwa ni kusaka huruma kwa wananchi kwa kutaka aonekane ni sehemu yao na kwamba anaonewa kwa kuwatetea wao. Ukweli ni kwamba amekuwa akifanya hivyo ili kutafuta hifadhi na kinga akijua ana madhambi mengi."


Akijibu tuhuma chache kati ya hizo huku akikataa kuzungumza kwa kirefu, Mengi alisema "mafisadi papa wana uwezo mkubwa sana siyo tu kwa mali za umma bali hata kutunga uongo kama ilivyofanywa na Rostam Aziz leo (jana)".


"Naomba nimpe Rostam Aziz ushauri wa bure kama kweli anataka kujisafisha ama kuondokana na shutuma zinazomkabili za ufisadi aende mahakamani ikiwezekana kesho (leo) asubuhi," alisema Mengi.


"Hata baada ya kukutana na waandishi wa habari leo, hoja ya kushutumiwa kama fisadi papa inabakia pale pale. Watanzania wanasubiri kwa hamu kubwa kusikia kwamba Rostam Aziz ameenda mahakamani kwa sababu Watanzania wengi hasa wanyonge wana hasira nyingi dhidi ya ufisadi."

CHANZO: Mwananchi

LET'S HOPE SOPHIA SIMBA NA KAPTENI MKUCHIKA WATAMKOMALIA ROSTAM AS THEY DID TO MENGI ALIPOTOA TUHUMA DHIDI YA MAFISADI PAPA.I CANT SEE SOPHIA SIMBA SAYING "WATOTO WA MJINI WANASEMA ROSTAM AMECHEMKA" AS SHE DESCRIBED MENGI'S STATEMENT.

SOONER OR LATER HAWA MAFISADI WA KIASIA WATAINGIA IKULU KAMA RAIS KAMA WENYE UCHUNGU WA DHATI NA NCHI YETU HAWATAAMKA SASA.WAMESHAIFANYA NCHI HII KUWA IKO MIFUKONI MWAO,WANATUPUUZA NA KUONGEA CHOCHOTE WANACHOJISKIA KUSE,A,SIMPLY BECAUSE OF JEURI YA FEDHA ZAO ZA KIFISADI.COULD YOU EXPECT MHINDI MWENYE ASILI YA KITANZANIA KUFANYA HIVYO INDIA AU YEMEN,OR WHEREVER THESE FISADIs ORIGINATE FROM?


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.