Showing posts with label Slimcony. Show all posts
Showing posts with label Slimcony. Show all posts

23 Jun 2012

MNYIKA HAKUKOSEA

Mara ya kwanza niliona mnyika amekosea sana kumwita rais Dhaifu, hii ni kutokana na ukweli kuwa kanuni za bunge hazimruhusu, lakini pia ameyasema yale mbele ya watanzania wote ambao wapo wenye mapenzi thabit kwa rais. Lakini kumbe rais amemruhusu mnyika aseme maneno yale

Hivi ni nani hajawahi ona watoto wa darasa la kwanza wanafunga barabara kwa kuwa mwenzao amegongwa mpaka matuta yawekwe, na siku hiyo hiyo matuta yanawekwa? Tumemfundisha nini mtoto huyu? Tumemfundisha serikali yako ni dhaifu lakini ukiishikia kiboko inatekeleza hapo hapo

Wakati wa mkapa wanafunzi udsm waligoma, mkapa akafunga chuo mwaka mzima, hatukusikia tena mgomo mpaka 2007 wakati wa kikwete, tuliposikilizwa tulichogomea, tuligoma kwa kila kitu hata kama hatukustahili

Kitendo cha mtu kusimama mbele ya bunge akapata courage ya kusema rais dhaifu, akarudia na kurudia peke yake inaprove kama rais ni dhaifu

USHAURI WA BURE KWA RAIS: 
Haiwezekani sovereign country tunaambiwa kuna muwekezaji ana passport tano, serikali imemshindwa, KWELI? Serikali ya watu mil 40, jeshi, police, na TISS, inaandikwa gazetini imemshindwa mtu mmoja? Vaa mkono wa chuma baba


Hakuna uhuru usio na mipaka mheshimiwa kikwete. He who wishes to be obeyed must know how to command, uhuru ukizidi sana tunaharibu nchi. Unatuachia saaaana mpaka tunaanza kukukosea heshima

Madaktari wamegoma, tukaambiwa rudini kazini haraka au tutawafukuza wote tutaleta wanajeshi wafanye kazi, then kesho tunawaita tunakaa nao mezani, baba watakupanda kichwani washajua una udhaifu, unawaogopa..

Machiavelli anasema If an injury has to be done to a man it should be so severe that his vengeance need not be feared..
Kwa mfano watoto wanagoma lazma matuta yawekwe, waagize walimu wao wawatandike viboko watoto warudi darasani, then baada ya mwezi weka tuta kuzuia ajali kwa kuwa hapo mwanzo walikaa miaka bila tu.
Tunagomagoma kila kitu kwa sababu unaturuhusu, lakini pia haujali.. Wanafunzi wagome, madokta wagome, walimu wagome, hivi nani anawapa kiburi? Hawa madokta nani anawapa kiburi cha kugomea serikali?

Men are so simple and so much inclined to obey immediate needs that a deceiver will never lack victims for his deceptions
Mtembelee Slimcony katika blogu yake inayopatikana HAPA

11 Jun 2012


Pichani ni shoga maarufu Bilali Mashauzi ambaye ni nadra kukosekana kwenye sherehe za akinadada maarufu Tanzania


SUNDAY, JUNE 10, 2012


MSIMAMO WANGU KUHUSU USHOGA

umeibuka mjadala mkubwa leo twitter kuhusiana na group la facebook la kudai haki za mashoga tanzania. i saw this coming, Mashoga wapo, walikuwepo na wataendelea kuwepo regardless tumewakubali au tumewakataa.

kwanza niseme Imani yangu ya dini, mwenendo wangu wa maisha na jamii ninayoishi nayo hainiruhusu kukubali ushoga. Natamka kuwa siukubali ushoga kwa kuwa kiimani ya dini yangu ni dhambi, lakini pia katika mfumo wa maumbile ya mwanadamu ni kinyume.

Lakini pia Sikubali uzinzi, uasherati, ushirikina, wizi pamoja na dhambi nyengine ambazo kwa utamaduni wa mtanzania ni makosa na dini zote tunazoamini Tanzania ni makosa hali kadhalika.

jambo linalonifanya niandike makala hii ni kuweka wazi kama hata Leo mashoga wakiandamana barabarani kudai Haki zao au nikisikia serikali imeruhusu ndoa za jinsia moja, nitaumia moyoni kwa kuwa kwa imani yangu si sahihi lakini sitatoka kuungana na WANAFIKI kupinga haki za mashoga

Nimetumia neno wa WANAFIKI kwa kuwa watanzania wengi ni WANAFIKI. kati yenu, nani dini yake inaamini uasherati na uzinzi ni sahihi? kipo kitabu cha dini kinaruhusu Uzinzi? je utamaduni wa Mtanzania unaruhusu Uzinzi? na je wewe mwenyewe unaamini Uasherati na Uzinzi ni sahihi?

kama dini yako hairuhusu uzinzi, wewe mwenyewe unaamini uzinzi na uasherati si sahihi, na utamaduni wako unakataa uzinzi na uasherati, UMEFANYA NINI KUHUSU SHERIA YA TANZANIA KAMA UKIKAA NA MWANAMKE/MWANAUME ZAIDI YA MIAKA MIWILI INAITWA NDOA? nguruwe huli ila mchuzi wake unakunywa?

Sisi wenyewe, ndugu zetu, jamaa na marafiki tunasifiana uzinzi, tunafanya uzinzi, tuna facebook groups za uzinzi, kitu ambacho kitamaduni na kidini si sahihi, lakini tukisikia shoga tunapiga kelele.. huo ni unafiki

Wapo waislamu wenzangu ambao ni walevi wa pombe lakini Nguruwe hawali kwa kuwa ni Haramu, pombe ni halali? mlevi ataingia peponi kwa imani yako? Baba Yangu ana msemo "ukiamua kula nguruwe, chagua aliyenona" meaning ukiamua fanya dhambi wewe fanya tu kwa kuwa kwa mungu hakuna dhambi ndogo

Niwakumbushe kwa mungu kuna njia mbili, Ama PEPONI au MOTONI. naamini kutokana na Mafundisho yangu kwamba Shoga, Mzinzi, Mwizi, Muasherati, Muuaji pamoja na dhambi nyengine wataingia moto mmoja hivyo basi ukiamua kataza maovu, acha kwanza wewe na kemea maovu yote bila kubagua kwa kuwa hata usipofanya ushoga ukafanya wizi, utakuwa hujajinasua na moto

sikatazi watu kupinga USHOGA na hata nikikataza mimi sio Mtume wala Rais na wala neno langu sio Sheria ila nasema Siungani na nyie Kwenye kupinga haki ya Mashoga kuoana wakati mmekalia kimya uzinzi, uasherati, na ushirikina ambavyo vyote havikubaliki kwa utamaduni wa mtanzania wala kwa dini tuanzoamini watanzania

*********HAYO NI MAONI YANGU NA NDIO MSIMAMO WANGU*****



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.