29 Dec 2007


Kapteni wa timu ya soka ya Motherwell ya Scotland,Phil O'Donnell,amefariki dunia muda mfupi baada ya kuanguka uwanjani katika mchezo wa Ligi Kuu ya hapa dhidi ya Dundee United.Mchezaji huyo aliyeanguka wakati anabadilishana nafasi na mchezaji mwenzie (substitution),alitibiwa kwa muda mfupi uwanjani hapo kabla ya kupelekwa hospitalini,na hatimaye kupatikana habari kuwa amefariki.Katika mechi hiyo iliyofanyika kwenye uwanja wa Fir Park,mjini Motherwell,timu ya marehemu huyo ilishinda kwa mabao 5-3,na kufanikiwa kushika nafasi ya tatu nyuma ya Celtic na Glasgow Rangers. 

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.