7 Oct 2008

Mwaka:1992
Mahala: Ruvu JKT
Miss Independent: Binti mrembo wa haja.Lakini kikwazo ni kwamba ni mtoto wa Mkuu wa Kikosi (CO).Na kwa wale ambao hawakuwahi kukanyaga JKT,CO ni Mungu-mtu wa Kikosi.You can imagine what would be the consequence ya "kuziingiza" kwa Miss Independent ambaye ni Mkuu wa Kikosi.

Mwaka: 1995
Mahala: Chuo flani (location withheld)
Miss Independent: Mmoja wa mabosi wa chuo hicho.Unajua kuna warembo ambao nadhani Mola alitumia siku nzima kuwa-design na siku nyingine nzima kuwaumba.Sheria za mahala hapo ziko wazi: speak to the boss only when they speak to you.

Mwaka: 2008
Mahala:Dar es Salaam.
Miss Independent: Kumwita huyu binti mrembo ni kutomtendea haki.Angeweza kuonewa donge hata na malaika.Hakuna neno linaloweza kuelezea urembo wake.Kikwazo ni kwamba anatoka familia yenye kujiweza mno.Hapo mahala pake pa kazi alikuwa anaondoka na tips za haja nyingi zikiwa in foreign currencies,achilia mbali fedha zisizohesabika alizokuwa akipewa na wale wanaoamini kuwa dawa ya kumpata mrembo yeyote ni fedha.Lakini they say when all luck is gone miracles happen in strangest form.This episode had a happy ending just like Ne-yo couldnt believe his ears when Miss Independent,Gabriele Union,apologized and....see the clip below



0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.